Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Wednesday, November 30, 2022

KUMBUKIZI YA MNUSO




Hii ni miaka 10 iliyopita Mtangazaji Marufu wa Radio One Tumie OmariPichani mwenye rangi mikononi ‘Piko’ siku kwenye Send Off yake iliyofanyika Morogoro na kuhudhuri na Waandishi wenzaka wa Mkoa wa Morogoro. Akiwemo Hamida Shariff anaye tafuna kipaja cha kuku.

 

Picha no 2 Hamida anayepiga kazi gazeti la Mwananchi akicheza Taarab na Mwandishi mwenzake Ratifa Ganzel anayepiga kazi Magazeti ya Uhuru na Mzalendo kwa sasa Ratifa  ni diwani wa Viti Maalumu kwa leserni ya CCM Picha zote na Dunstan Shekidele


 

UDAKUZI SPESHO.   MBOGA MAJI WA IHEFU AIBUKIA MTO JANGWANI DAR.


 

 

Na Mdakuzi Dunstan Shekidele,Morogoro.

 

KWELI Maisha ya Soka la Tanzania ni kama Gwaride nyuma geuka wa Mwisho anakuwa wa kwanza na wakwanza anakuwa wa Mwisho.

 

Hali hiyo imetimia jana baada ya timu inayoshika mkia kwenye ligi kuu Tanzania Bara lhefu Fc ‘Wana Mbogo Mji’ wenye maskani yao katikati ya Mashamba ya Mpunga Wilayani Mbarali Mkoani Mbeya kuwafunga Wananchi’Yanga’ Wanaoongoza ligi hiyo kwa kuwachapa bao 2-1.

 

Ushindi huo umewatoa Mkiani lhefu na kupanda  nafasi 3 juu kupitia ngazi ya Yanga inayotajwa kuwa na kikosi chenye wachezaji wa dhamani kubwa kuliko timu yoyote nchini.

 

Gemu hiyo iliyomilikiwa na lhefu kwa takribani dakika zote 90 imepigwa  uwanja wa Highland Estate unaomilikiwa na Wana Mbogo Maji hao wanaonolewa na kocha wa zamani wa Yanga Juma Mwambusi’Mnyambara’mzaliwa wa Mbeya.

 

 Kipigo hicho nimevunja mbwembwe za wana yanga hao kupigiwa makofi kila walipocheza mchezo wa ligi kuu wakifurahia rekodi yao ya kutokufungwa mchezo yoyote’Unbeaten 49’ mfurulizo toka ligi ya msimu uliopita na kuweka rekodi mpya kwenye ukanda huu wa Afrika Mashariki na kati ikiwa timu pekee iliyocheza michezo  49 bila kufungwa.

 

Kwa masigitika Makubwa  Mbwembwe zao hizo ziliisha jana kwenye msitu wa mashamba ya Mbunga Mbarali,baada ya kufungwa na wakulima hao wa Mpunga  waliokuwa wakiburuza mikia kwenye ligi hiyo.

 

 Matokeo hayo ya kikatili  kwa Yanga yanasindikizwa na msemo wa wahenga unaosema kuna Majira Saa Mbovu nayo inasema Kweli.

 

Jana tetemeko la Mayele lilizimwa na Zoluba kali lililozalishwa na upepo mkali kutoka kwenye Mashamba ya Mpunga ya Mbarali ambapo Mayele alionekana kama joka la kibisa lisilokuwa na sumu mdomoni.

        

Licha ya kuwapa makavu wananchi kwenye Udakuzi hapo juu lakini pia nitakuwa mnafika kama wanafiki wengine kama sita dhamini mafanikio ya timu hiyo ya kunyakua ubingwa wa Ligi kuu, Ngao ya Jamii na F.A Cup.

 

 Kama hiyo haitoshi Yanga hao hao wameshangaza Afrika baada ya kuwafunga Waarabu wa Tunisia nyumbani kwao bao 1-0 na kukata tiketi ya kuingia makundi kombe la Shirikisho barani Afrika ambapo ratiba ya makundi hayo inatarajiwa kupangwa Desemba 12.

 

lfahamike baadhi ya wachezaji wa Klabu hiyo ya Tunisia iliyofungwana Yanga kwa sasa tunawashuhudia wakiitumikia timu yao ya taifa ya Tunisia kwenye fainali za Kombe la Dunia hivyo yanga sio timu ya kumchezo mchezo imewapiga watu wa viwango vya kombe la dunia sio timu nyingine zimetinga makundi kwa kuzifunga timu vya viwango vya Afrika.

 

 

lkumbukwe  licha ya kufungwa jana timu hiyo yenye Maskani yake Makutano ya barabara za Mitaa ya Twiga na Jangwani Kariakoo Dar bado inaongoza ligi hiyo ikiwa na Point 32 huku akiwa na mchezo  mmoja wa Kiporo dhidi ya Tanzania Prisons utakaopigwa keshokutwa Novemba 5 Kwa Mkapa Dar.

 

 Baada ya kiporo chao cha Mihogo kuwachachia jana na kulazimika kulishwa viporo vya sahani 2 za Wali kutoka mashamba ya Mpunga Mbarali Mbeya, kwa sasa Yanga wako kwenye mahesabu makali ya kupasha moto kipora chao hicho cha keshokutwa dhidi ya Wajera jera hao wanaopiga pira Gwaride’.

 

Namalizia Udakuzi huu kwa kuwatia moyo Mashabiki wa Yanga siku zote Mwanamke mwenye watoto adui yake namba moja ni yule Mwanamke Mgumba ambaye hafurahi kuona mwanamke mwenzake anawatuma watoto zake dukani  huku yeye hana mtoto hata mmoja wa kumtuma dukani.

 

Shekidele hana hatia nimeamua kuandika Udakuzi huo kufuatia kichapo hicho cha Yanga kufuatia baadhi ya mashabiki timu hiyo walikuwa na ngebe kali kwa mashabiki wa timu nyingine wakijinasibu kwamba watifikisha mechi 100 bila kufungwa.

 

  

Monday, November 28, 2022

BONDIA CHEKA AOPOA DEMU WA KIZUNGU UJERUMANI.

Bondia Cosmas Cheka akiwa na Mchumba'ke wa kizungu

Cheka akiumwagilia Moyo viwanj vya Ujerumani na Mpenzi wake wa kizungu





 


                Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

BONDIA Maarufu wa ngumi za kulipwa nchini Cosmas Cheka anayeishi nchini ujerumani kwa sasa amefanikiwa kumiliki  demu wa kizungu zaia wa Ujerumani.

 

Cheka ambaye ni Mdau Mkubwa wa Mtandao Pendwa wa shekidele alimtambulisha Mpenzi wake huyo kwa Watanzania wenzake alipofanya  Mahojiano Maalumu  na Mtandao huu leo asubuhi kupitia Ukurasa wa Facebook  wa Dustan Shekidele.

 

Alipotakiwa kutana jina la Mchumba’ke huyo Cheka alisema Mtarajiwake wake huyo anaitwa Casselin Phil raia wa Ujeruamani aliyeangukia kwenye penzi zito la mtoto wa Kimakonde ‘Chinga kutoka Mtwara aliyekulia Mkoani Morogoro.

 

 Alipoulizwa hapo Ujerumani anaishi Mji gani na kwamba anampango wa kurejea nyumbani au ametekwa mazima na mtoto huyo mzuri wa Kijerumani Cheka alicheka kisha akajibu.

 

“ Shekidele kwanza nikupongeze kwa kazi nzuri unayoifanya ya kutupa habari moto moto watanzani wengi wanaoishi huku Ujerumani ni wadau wakubwa wa Mtandao wako.

 

Binafsi  bila kuingia kwenye Mtandao wako naona kama sijashiba habari kwani napata habari za kusisimua za Tanzania hasa za nyumbani Morogoro kupitia Mitandao yako.

 

Nikijibu Maswali yako hapa Ujerumani naishi Mji wa  Berlin na huyu Shemeji yako, kuhusu kurejea  nyumbani lazima nirejee ingawa si kwa siku za  hivi karibuni kwani bado nipo nipo sana huku”alisema Cosmas ambaye ni mdogo wa damu wa bondia Maarufu nchini Francis Cheka’SMG.’

 

 Mara baada ya mahojiano hayo Cosmas alimtumia Picha kibao Mwandishi wa habari hizi akiwa na mkewe huyo Mteule.

Mtandao huu unamuombea kwa Mungu amfanyie wepesi Mtanzania mwenzetu,Mwana Morogoro mwenzetu kwenye mipango yake mbali mbali ya kimaisha.

 

Angalia Picha mbali mbali za Cosmas Cheka akiwa viwanja mbali mbali vya Ujerumani akiwa na My wake wa kitasha.

 

Akichanganya rangi Black and White.

 

Mitandao Pendwa ya shekidele inawasomaji wengi pande zote za dunia zikiwemo nchi za Ujerumani, Marekani. Blazil. China , Ufaransa Uarabuni. Denmack, Canada Japan.lndia nk

 

Sunday, November 27, 2022

CHEDEMA, CCM WASHIRIKI MAZISHI YA DEREVA WA MALORI.

Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Morogoro Moses akifunguka kikao cha Mafunzo ya Mawakala wa Chadema Digital mOctoba 16 mwaka huu
Gari lililobeba viongozi wa Chedema Jimbo la Morogoro likiwa eneo la Msibani
Mwenyekiti kiti  wa Chadema wilaya ya Morogoro [Mwenye koti na jezi ya Simba ndani akitoa heshima zake kwa marehemu kaka yake
Mjane wa marehemu Bi Maimuna ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Kata ya Mkundi
MNec Aziz Abood[mwenye shati la mistari stari] akiwasili kwenye msiba huo huku akisindikizwa na kundi la Makada wa CCM.

 Mwenye gauni la kitenge aliyeweka mikono tumboni ni Bi Geloda Kimilila ambaye ni Mama mzazi wa Mwenyekiti  huyo wa Chadema akiwa mbele ya jeneza la Mpendwa Mwanaye ambaye ni mtoto Pekee wa kiume wa Marehemu kaka yake


 

            Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

 

VIONGOZI Wakuu wa  Vyama Vikuu vya Siasa nchini Chama Cha Mapinduzi’CCM’ na Chama Cha Demokrasia na Maendele ‘Chadema’ Jimbo la Morogoro wiki iliyopita waliweka kando itikadi zao na kushirikiana kwa pamoja kumzika dereva Maarufu wa malori nchini Marehemu Tonny Ntukula.

 

Viongozi hao wa CCM na Chadema wameunganisha na Familia hiyo ya marehemu ambapo baadhi ya wanafamilia hao wamegawanyika wengine ni Viongozi wa CCM na wengine ni Viongozi wa Chadema.

 

Mdogo wa Marehemu Moses Kimilila ni Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Morogoro huku Mke wa Marehemu Bi Maimua Semambua ni Mwenyekiti wa CCM Kata ya Mkundu huku dada wa Marehemu Sophia Ntukula pia akiwa Mjumbe wa serikali ya Mtaa wa River Side Kata ya Mwembesongo kwa leseni ya CCM.

 

Baadhi ya Vigogo wengine wa CCM walioshuhudiwa na Mwandishi wa Mtandao huu kwenye msiba huo ni Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Taifa ‘M -NEC’ Aziz Abood Katibu wa CCM Kata ya Mkundi na Diwani wa Kata ya Mkundi kwa leseni wa CCM Seif Chomoka.

 

Binafsi nahifahamu vizuri familia hiyo ya Ntukula niliyoishi nayo kwa miaka mingi Mtaa mmoja wa Makaburi B Kata ya Mji Mpya, Mama wa Mwenyekiti huyo wa Chadema  Bi Geloda  Kimilila  anazaliwa tumbo moja na Marehemu Agustino Ntukula baba mzazi wa Marehemu Tony.

 

 lfahamike pia familia hiyo akiwemo Mwenyekiti wa chadema na Sophia Ntukula na Magreth Ntukula wote ni wadau wakubwa wa Mitandao Pendwa  ya shekidele www.shekideletz.blogspot.com. lnstagran facebook ya Shekidelemkudesimba na Dustan shekidele.

 

Hivyo baada ya kusoma habari hizo kwenye Mitandao hiyo yenye wasoma wengi pande zote za dunia, Mwenyekiti huyo wa Chadema Kamanda Moses ni niongoni mwa wanafamilia waliompigia simu Mwandishi wa Mtandao huu akimpa shukrani kwa kushiriki mazishi ya mpendwa wao sambamba na kutumia mitandao yake kuripoti matukio yote ambapo watu waliokuwa mbali walipata taarifa za msiba huo A-Z kupitia Mtandao huo wa shekidele.

        

 


PADRI AWAPA MAKAVU WATU MSIBANI

                               Padri Elia akitoa karipio hilo

 


 

Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

 

PADRI wa kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro Padri Elia, katikati ya wiki hii amewapa Makavu baadhi ya watu wenye tabia ya kutoa mamilia ya pesa kwa marehemu  huku wakikacha kutoa msaada wa matibabu akiwa mgonjwa.

 

 Padri huyo ‘Janki’ alitoa kalipio hilo kwenye sehemu ya mahubiri yake aliyoyatoa kwenye msiba wa Marehemu Tonny Ntukula aliyeanza kuugua ugonjwa wa figo toka Mwaka 2021 hadi alipofariki dunia kwa ugonjwa huo juzikati Novemba 21-2022.

 

“Jambo jema na lenye faraja  kwa Jamii na mbele za Mungu  ni yule mtu anayetoa msaada wa Matibabu kwa Mgonjwa, kuna baadhi ya watu Mgonjwa anapohitaji Msaada wao wa pesa za kununua dawa wanakwepa lakini mgonjwa huyo huyo akifariki  watu  hao wanajitokeza kwa wingi wakishindano kutoa pesa nyingi za rambi rambi nahisi hizo pesa hazina msaada mkubwa kwa marehemu huyo zingekuwa na  msaada pale alipokuwa akiupigania uhai wake pale kitandani ”alisema Padri huyo na kupigiwa makofi  na baadhi ya waombolezaji waliofulika kwa wingi kwenye msiba wa Mpendwa wetu Tonny ‘Bonge’.Ntukula.

 

 Katika kukadhia kalipi hilo Mwenyekiti wa Kigango cha Mji Mpya Mzee Cosmas Damiani alipigia Msumari kwa kutoa ushahidi wa kweli wa tukio hilo.

 

“Padri umesema kweli mimi ninaushahidi wa  kweli wa jambo hilo,siku za nyuma nilikuwa na uguza mgonjwa wangu na pesa za matibabu zilihitaji laki mbili ili tuokoa maisha yake lakini kwa bahati mbaya pesa hizo zikuzipata kwa wakati hivyo  mgonjwa wangu akafariki dunia.

 

 Chaajabu kwenye msiba huo watu mbali mbali wakiwemo waliokuwa na taarifa za ugongwa huo walijitokea na kunipa rambi ramba za pesa kiasi cha milioni 2 na nusu sasa nikajiuliza pesa hizo wangenipa wakati ule wa ugonjwa  zingesaidi kwa kiwango kikubwa kuokoa maisha ya Mgonjwa wangu.

 

 Hakuna shaka yoyote kwamba baadhi ya watu wanakufa kwa kukosa msaada wa pesa za matibabu”alisema Mzee Damiani ambaye ni mmoja wa Vigogo wa kanisa Kuu la Mt Patrick Jimbo la Morogoro.

Saturday, November 26, 2022

UDAKUZI SPESHO.   MWANAUME AVUNJA BANDA LA MAMA NTILIE BAADA YA KUMFUMANIA.


Mdakuzi wa Mtandao huu[kulia] akipakia mbao hizo huku wakiangua vicheko wakati akisimuliwa tukio hilo na TOT.
Mbao hizo zikiwasili nyumbani wa Mdakuzi


 Mwandishi wa Mtandao huu akiwa Mikuni ba usafiri wake wa Pikipiki ya Mwendo kasi

 

Na Mdakuzi Dunstan Shekidele,Morogoro

 

AMANI ya Mwenyezi Mungu na iwe juu yenu.

 

Ama baada ya salamu Mdakuzi wa Mtandao Pendwa wa Shekidele anakurambisha Udakuzi wa Mwanaume mmoja [jina kapuni] akidaiwa kubomoa banda la chakula alilomjengea Mchepuko wake baada ya kumfumani akiibanjua amari ya 6 na dereva wa boda boda  ndani la banda hilo lililojengwa wiki iliyopita kwa gharama kubwa.

 

 Mara baada ya kutoke kwa valangati hilo lililojaza Nzi kibao mtaani hapo baadhi ya Nzi hao walimjuliza Mtakuzi ambaye alitinga eneo la tukio na kukuta tayari banda hilo la Mama Ntilie limeshavunjwa.

 

“Shekidele umechelewa  Jamaa baada ya kumfumania mpenzi wake ndani ya banda hili kamua kulivunja ambapo mabati mapya na mbao mpya kaenda kuziuza bei ya kutupa kwa yule jamaa anayefanya biashara ya kuuza vifaa ya ujenzi vilivyotumika pale Mji Mpya jirani na kituo cha Polisi ukifika pale yule jamaa ambaye alishiriki kubomoa banda hili atakupa habari kamili ya tukio hili”alisema shuhuza mmoja aliyeomba hifadhi ya jina lake lisitaje popote.

 

 Baada ya kurambishwa Ubuyu huo Mbichi kabisaa uliokolea rangi  Mdakuzi wa Mtandao huu alipiga gia Pikipiki yake ya Mwendo kasi hadi kwa muuza vifaa hivyo vya ujenzi aliyefahamika kwa jina la TOT.

 

Alipotakiwa kuelezea tukio hilo awari TOT alionekana kukwepa kulizungumzia, baada ya kuligundua hilo Mdakuzi wa Mtandao huu aliyehitimu shahada ya Udakuzi nchini Kiuba alitumia mbinu za kishushu na TOT akifunguka kila kitu msikie akisimulia A-Z fumanizi hilo.

”Shekidele ni kwetu tukio hilo limetokea jana hawa wanawake zetu baadhi yao ni washenzi kuna jamaa yangua anafamilia yake lakini kama unavyojua tena alikuw ana mahusiano ya kimapenzi na mchepuku wake ambao unafanya biashara ya chakula’Mama Ntile’ hivyo kama unavyojua msimu wa mvua umeanza na lile banda lilikuw abovu bovu limeelezwa na maboksi.

 

Hivyo Jamaa uangu kaamua kusambaza upendo kwa kuvunja banda hilo bovu na kujenga banda lingine imara akinunua mabati mabya na mbao za kenchi mpya zilizopakwa dawa ya kuzuia kuliwa na wadudu.

 

 Chaajabu baada ya banda hilo kukamilika baadhi ya wambea walimtonya jamaa kwamba kila siku Mama Ntilie huyo akimaliza chakula hujifungia ndani ya banda hilo na dereva mmoja wa boda boda.

 

Jamaa yangu juzi usiku katoloka kwa mkewe kaenda kwenye banda hilo na kukuta boda boda iko nje huku mlango wa banda hilo ukiwa umefungwa kwa ndani”alisema TOT na kuendelea kumwaga utamu wa tukio hilo.

 “Jamaa aligonga mlango mwanamke huyo bila kujua kwamba anayegoma ni Bwana’ke kwa vile alishazoe kwamba kwa muda huo Kichwa chake hicho kinakuwa kwa mkewe alifungua mlanga na machoyake yakukutana na sura ya Bwana’ke huyo ambaye alimuliza swali moja tu kwamba nilikujengea banda hili ili ilifanye gest ya kuingiza mabwana nazo?.

 

 Mbona awari lilivyokuwa wazi hukufanya ushenzi huu ndani ya banda hivyo kesho nalivunja banda hili nachukua vifaa vyangu huyu boda boda wako akujenge banda lingine muendelee kufanya usheni wenu kwa uhuru.

 

 Kweli kesho yake jamaa kaita wale wale mafunzi waliojenga wakalivunja banda lile na kuja kuniuzia mabati na mbao mabati yote nimeshayauza asubuhi zimebaki hizi mbao tu”alimalizia kusema TOT

 

Mdakuzi wa Mtandao huu alizinunua mbao hizo kwa bei chipa  kazipakia kwenye Kitoyo na kuzipeleka nyumbani wake kuzitumia kuezekea banda la kuku.

Nilipofika nyumbani wakati naendelea kushusha mbao hizo nikawasha Luninga nikachomeka Frash yenye wimbo wa taarabu ulioimbwa na Marehemu lssa Kijoti unaosema ‘kanunua simu kampa demu walivyoachana kamnyang’anya.’

 

 Mara nyingi napendelea kusikiliza wimbo huo nikiwa na hudhuni kubwa kwani kifo cha Kijoti nilikishuhu ambapo wakati kundi lao la  Five Star Morden Taarabu likitokea jijini Mbeya kwenye shoo walipofika ndani ya Mbugha ya wanyama ya Mikumi usiku mnene kuna Lori lililobeba mbao liliharibika eneo la barabara.

 

Huku Kijito akiwa ameketi siti ya Mbele kwenye basi ndogo aina ya Coaster ililigonga Lori hilo kwa nyuma na mbao hizo zilimtoboa tumbo Kijito na kutenganisha mwili wake kiwili wili na semu ya miguu.

 

Wasanii wengi wengi walikuga kwenye ajari hilo lakini kwa mapenzi ya Mungu rafiki yangu Ally Juma Mgona Maarufu Ally J aliyeketi siti ya nyuma ya basi hilo ni miongoni mwa watu wachache walionusurika kwenye ajari hiyo. Mara baada ya kutoka ajari hiyo Mwandishi wa Mtandao huu alipigia gia Pikipiki yake ya Mwendo kasi hadi eneo la tukio kwenye kukusanya habari alipofika alishuhudia  ajari hiyo Mwanzo mwisho huku baadhi ya wananchi wa kitongoji cha Doma walidaiwa kukwapua baadhi ya vitu vilivyokuwa ndani ya basi hilo.

                            


 

 

Thursday, November 24, 2022

ABOOD ATOA ONYO KWA MATAPELI WANAOWATAPELI PESA WAFIWA KWENYE MSAADA WA MABASI YAKE YA KUZIKIA.

Moja ya basi la Abood likiwe msibani maeneo ya Mawenzi  Morogoro.
Mh Abood[kulia] akimpa Pole Zamoyoni Mogella alitevaa miwani ya giza.
....Mh Abood na Mogella akipozi mbele ya camera za Mtandao huu mara baada ya tukio hilo
    Mh Abood akitoa onyo hilo Msibani hapo.

 Mzee lbrahim Mangwende ambaye ni babu mzaa mama wa Winga wa Namungu Shiza Kichuya naye akimpa Pole Mogella aliyeketi chini mwenye nguo nyeusi ni mke wa Zamoyoni Mogella.Picha


            Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

TAJIRI anayetajwa kuwa namba moja mkoani Morogoro ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mh Abdulaziz  Mohamed Abood ‘Maarufu Aziz Abood’ juzi ametoa onyo kali  kwa matapeli wanaowatapeli pesa wafiwa kwenye  mabasi yake anayoyatoa msaada kwa wafiwa.

 

Mh Abood alitoa Onyo hilo kwenye Msiba wa Mpwa wa Mchezaji nyota wa zamani wa timu ya Simba na Taifa Stars Zamoyoni Mogella’Golden Boy’marehemu Tonny Aguston Ntukula aliyefariki Novemba 21 na kuzikwa Novemba 23 kwenye Makaburi ya Bingwa Morogoro.

 

Baada ya kukamilika kwa lbada ya kumuombea Marehemu huyo iliyofanyika nyumbani kwao Mtaa wa River Side  Kata ya Mwembesono Mkoani hapa,baada ya kukamilika kwa lbada hiyo Muongozaji  alimkaribisha Mbunge huyo kuwasalimia wananchi wake sambamba na kutoa rambi rambi zake kwa familia ya marehemu.

 

Mara baada ya kuwapa pole kasha  kukabidhi rambi rambi zake kwa familia Mh Abood alisema.

 

”Naomba nitoe angalizo kwa wananchi wote wa Manispaa ya Morogoro kama mnavyofahamu kwa miaka mingi sasa nimekuwa na utamaduni wa kutoa mabasi yangu bure kwenye misiba.

 

 Nafanya hivi sio kwa sababu ya Ubunge  hapana nafanya hivyo nikitekeleza agizo la Mwenyezi Mungu la kututaka wanadamu tusaidiane kwenye shida na raha.

 

 Nasigitika kusema baadhi ya watu wasio na huruma wanatumia fursa hiyo kuwatapeli wafiwa, siku za hivi karibuni kumeibuka matapeli ukitokea msibani  kuwatapeli wafiwa wakiwataka wachangie elfu hamsini za mafuta”alisema Abood kwa Jazba na kuendelea kusema.

 

”Hao ni matapeli mtu yoyote akikuambia hivyo toa taarifa tumkamate, natoa mabasi bure kwenye misiba yote pia hata ukiwa na shughuri  nyingine inayokusanya watu wengi kutoka eneo moja kwenda lingine pia natoa mabasi bure bila gharama yoyote hata huyo dereva anayekuja analipwa na ofisi yangu ubwabwa wanaokula waombolezaji na yeye mumpe huo huo”alimalizia kusema tajiri huyo na kupewa zawadi ya makofi kutoka kwa umati mkubwa wawatu uliofulika kwenye msiba huo

 

lfahamike Mh Abood Kipenzi cha wanamorogoro anayemilikia Mabasi, Malori, Viwanda na Vyombo vya habari, alianza kutoa msaada huo wa mabasi ya kuzikia zaidi ya miaka 20 kabla  hajawa mbunge ambapo kwa mara ya kwanza alichaguliwa kuwa mbunge wa Jimbo la Morogoro mwaka 2010 akiendelea kutetea kiti hicho mpaka sasa


 

TAJIRI ABOOD AONGOZA MAMIA YA WANANCHI MORO KUMZIKA DEREVA WA MALORI.


Mjane wa marehemu Bi Maimua ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM tawi la Mkundi

Padri Elia akimwagia maji ya baraja jeneza lililobeba mwili wa mpendwa wetu Tonny Ntukula

                      Marehemu Tonny enzi za Uhai wake
...Mh Abood mwenye shati la mistari stari akiwasili eneo la msiba huku akisindikizwa na madaka kibao wa CCM

Mhe Abood kulia akisalimiana na Zamoyoni Mogella waoshuhudia tukio hilo ni babau wa shiza Kichuya Mzee lbrahim Mangwende mwenye bagharashia kichwani na mwenye nguo nyeusi ni mke wa zamoyoni Mogella

Mhe Abood kushoto na Zamoyo Mogella wakipozi mbele ya kamera za Mtandao Pendwa wa Shekidele, kwenye msiba wa Tony Ntukula jana jioni

Mh Diwani wa Kata ya Mkundi ambaye pia Mkurugenzi Mkuu wa Chuo Cha Uandishi wa habari Morogoro Mh Seif Chomoka akishukuru baada ya kutambulishwa kwenye msiba huo.


 

Mh Abood akizungumza kwenye Msiba huo
......

 akimkabidhi rambimbi baba mdogo wa marehem


Mwenyekiti wa tawi kuu la Yanga Mkoani Morogoro lssa Kitukwa maarufu lssa Chabala alikabidhiwa kitengo cha kijiko akitabasamu baada ya kuiona kamera ya Mtandao huu


Sophia Ntukula ambaye pia ni Mjumbe wa serikali ya Mtaa wa River Side akipokea rambi rambi kutoka kwa watu mbali mbali

Mchezaji nyota wa zamani wa Simba Reli na timu ya Taifa Zamoyoni Mogella mwenye miwani akisalimiana na Mzee lbrahim Mangwende ambaye ni babu wa shiza Kichuya. aliyeketi chini ni mke wa Mogella  

Mchezaji wa Shujaa Mbaraka Denis akimsarimia Mzee lbrahim Mangwende ambaye ni babu mzaa mama wa mchezaji wa zamani wa Simba Shiza Kichuya ambaye kwa sasa anakipiga Namungo wa Lindi

Baadhi ya wachezaji wa zamani walishiriki mziba huo beki wa zamani wa Reli ya Morogoro Ally Kaliati Kidevu[mwenye shati nyeusi.

Winga wa zamani wa Reli ya Julius Ngawambala
Gari lililobeba viongozi wa Chadema Jimbo la Morogoro
                Katibu wa CCM Kata ya Mkundi akizungumza
...Baada ya katibu huyo kuzungumza wasaidizi wake walimkabidhi bahasha ya Pole mwenye kiti wao wa tawi la Mkundi Bi Maimuna


Nauma sana wanafunzi wa kidato cha kwanza shule ya sekondari Mkundi wamejichangisha na kupata kiasi cha shilingi elfu 40 walizomkabidhi dent mwenzao aliyefiwa na mpendwa baba yake.

Dent huyo baada ya kupokea pesa hizo aliangua kilio huku akiwakumbatia wanafunzi wenzake kwa kumfariji kwenye kindi hiki kigumu cha kuondokewa na mzazi wake.

 

Baadhi ya waombolezaji walishindwa kujizuia na kujikuta wakiangua vilio kwa sauti ya juu baada ya kushuhdia tukio hilo.


...Bint wa kwanza wa marehemu anayesoma kidato cha kwanza shule ya sekondari kata ya Mkundi
Baadhi ya wanafunzi wakimuaga baba mzazi wa mwanafunzi mwenzao
,,,,,Ndugu wa Mareheme akisaidia kwenda kutoka heshima zake za mwisho kwenye mwili wa mpendwa wao

.....Baada ya ibada kwisha mwili uliingizwa kwenye gari tayari kwa safari ya kuelekea makaburini

Mh Abood akiongoza msululu wa magari kuelekea makaburini

 

 

         Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

 

TAJIRI anayetajwa kuwa namba moja mkoani Morogoro ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini  Mh Aziz Abood jana ameongoza Mamia ya wananchi kumzika  dereva Maarufu wa Magari Makubwa Mkoa wa Morogoro Marehemu Tony Agustino Ntukula[42].

 

Marehemu Tony aliyewahi kuendesha Malori kwenye Kampuni kubwa ya Ujenzi wa barabara ya NCC na kampuni ya Ujenzi wa Reli ya Mwendo Kasi ya Bam Enteboton  Yapi Markezi alifariki dunia Novemba 21 na kuzikwa kwenye Makaburi ya familia yao yaliyopo Bingwa Manispaa ya Morogoro.

 

Kabla ya kwenda kumpunzisha kwenye nyumba yake ya Milele Umati Mkubwa wawatu ukiongozwa na Makada wa CCM na wachezaji Maarufu wa zamani wa soka akiwemo Zamoyoni Mogella walishiriki ibada ya kumuombea Marehemu ilitofanyika nyumbani kwao Mtaa wa River Side Kata ya Mwembesongo.

 

lfahamike Mke wa Marehemu Bi Maimuna Semandua ni Mwenyekiti wa CCM Tawi la Mkundi, dada wa Marehemu Bi Sophia Ntukula ni Mjumbe wa Seriali ya Mtaa wa River Side kwa leseni ya CCM na baba wa Marehemu Hayati Agustino Ntukula enzi za Uhai wake alikuwa mchezaji mahiri wa timu ya Shujaa ambayo inaundugu na timu ya Simba ya Jijini Dar.

 

Kwa sasa tawi kuu la Simba la Mkoani Morogoro linajulikana kwa jina la tawi la Shujaa.

 

 Hivyo Mwandishi wa Mtandao huu aliwashuhudia baadhi ya wachezaji nyota wa zamani kwenye msibani huo baadhi yao ni  Zamayoni Mogella aliyewahi kuzitumikia timu za Reli Moro, na Simba, Julius Ngawambala, Ally Kidevu[Reli] na Mbaraka Dens aliyeitumikia Shujaa. Watu wengine mashuhuri walioshuhudia na Mwandishi wa Mtandao huu ni Mkurugenzi Mtendaji wa Chuo cha Uandishi wa habari Morogoro’MSJ’kilichopo Mkundi  Seif Chomoka ambaye pia ni Mh diwani wa Kata ya Mkundi aliyeutumia Ustahiki Meya kwa takribani wiki Moja kabla ya uondolewa kwa sababu zinazodai za kikanuzi za Uchaguzi. Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi Mh Chomoka alisema amesigitishwa sana na kifo hicho cha Mume wa kiongozi wake wa Chama kwenye Kata hiyo ya Mkundi.

 

”Shekidele Mke wa Marehemu ni Mwenyekiti wangu wa tawi la CCM Mkundi hivyo Msiba huu ni wetu sote”alisema Big Boss huyo wa Chuo cha Uandishi wa habari Morogoro.

 

Watu wengine mashuhuli walionaswa na Mwandishi wa habari hizi ni Viongoiz wa Chadema Jimbo la Morogoro

 

Kama kawaida Mtandao huu umekusanya matukio kibao kwenye Msiba huo ikiwemo tukio la Mh Abood kuwashukia watuwanaowatapeli wananchi kwenye msaadawake wa mabasi ya kuziki.na tukio la Pili la Padri kuwa makavu watu wanatoa pesa nyingi kwenye msiba ili hali kabla ya marehemu kufariki dunia hawakujitokea kutoa pesa za matibabu wakati taarifa za ugonjwa walikuwa nazo.

 

     WASIFU  WA MAREHEMU.

Wasifu wa marehemu uliosomwa na baba mdogo wa marehemu ulidai kwamba Marehemu Tonny alizaliwa Septemba 17-1980 Mtaa wa River Side.

 

 Baada ya kuhitimu  shule ya msingi na Sekondari Mwaka 1996 alijiunga na Chuo cha Ufundi Stand VETA katika fani ya udereva wa Magari Makubwa na kuhitimu mafunzio hayo 1999.

 

Wasifu huo umezidi kubainisha kwamba Marehemu ameanza kuugua ugongwa wa Figo toka Mwaka 2021 hadi alipokutwa na umauti kwa ugongwa huo Novembe 21-2022.

 

Marehemu ameacha Mjane mmoja na watoto wawili. Katika kupokea rambi rambi wanafunzi wa Kidato cha Kwanza Shule ya Sekondari Mkundi wanaosoma darasa moja na mtoto wa kwanza wa marehmu waliliza watu wengi baada ya kutangaza kujichangia kiasi cha shilingi elefu 40 na kumkabidhi dent mwenzao kama pole kwa kufiwa na Mpendwa baba yake.

 

Baada ya kupokea pesa hizo mtoto huyo aliangua kilio na wawakumbatia wanafunzi hao waliovaa sale za shule ambali tukio hilo kwenye picha hapo chini.

  

Bwana ametoa na Bwana ametwa jina lake lihimidiwe.

Tangulia kamanda Tony Bonge tutaonana baadae nafarijika nilifika mara kwa mara kukujua hali wakati ukiwa kitandani ukiendelea kupigania uhai wako.

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...