Mwandishi wa Mtandao huu akiwa juu ya Milima hiyo ya Uluguru akiangalia shamba a matunda ya kizungu ya Kauberi. Mwandishi huyo alipanda juu ya Milima hiyo lliopo Manispaa ya Morogoro na Usafiri wake wa Pikipiki.
.....Mwezi ukichomoja Milima ya Uluguru Majira ya saa 12 na nusu Jioni
......Mpiga picha wa Mtandao huu alipiga picha hii akiwa chini ya Milima ya Uluguru Mtaa wa Area Five Nane nane Manispaa ya Morogoro
Mkurugenzi wa Shirika hilo Gration Mbelwa [kushoto] akiwa na Katibu Mkuu wa Chama Cha Boda boda Mkoa wa Morogoro Francis Kayombo [Kati mwenye frana nyeupe ni Mjumbe wa Bodi ya shirika hilo Hussein Ngurungu ambaye ni mchezaji wa zamani wa Pan Afrika na Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars.
Ifahamike Mzee Ngurungu ameitumikia timu hiyo ya Taifa kwa miaka 12 mfurulizo rekodi hiyo aliyoiweka miaka ya 80 mpaka 90 haijavunjwa na mchezaji yoyote mpaka sasa.
Kamati ya Mashindano hayo
Na Dustan Shekidele,Mogogoro.
KATIKA hali ya kurejesha ubora wa Milima ya Uuguru ambayo ni chanzo kikuu cha maji yanayosambaa Mikoa ya Morogoro, Pwani na Dar es salaam.zaidi ya miche 14500 ya Miti inatarajiwa kupandwa juu ya Milima hiyo ikiwa ni jitihada za serikali kuleta mabadiriko juu ya matumizi ya Nishati safi na utunzaji wa Mazingira.
Shughuri hiyo iliyoandaliwa na Shirika isilo la kiserikali la Mother Of Mercy linakwenda sambamba na michuano ya Mpira wa Miguu itakayoshirikisha timu 32 kutoka Kata zote 29 za Manispaa ya Morogoro.
Akizungumza na Waandishi wa habari Mkurugenzi wa Shirika hilo Bw Gration Mbelwa amesema mbali na Mashindano hayo yaliyopewa jina la Nishati safi Cup pia kutakuwa na mshindano ya Boda boda.
Akifafanua zaidi mbele ya Waandishi wa habari Mbelwa amesema.
“kila timu itakayoshiriki mashindano hayo itapanda miche 500 nia ni kurudisha hali ya hewa kuwa salama huku lengo ni uhamasishaji wa wananchi juu ya matumizi ya Nishati safi” amesema Mkurugenzi huyo na kuongeza kudadavua jambo hilo.
“Licha ya michuano ya Mpira wa miguu kutakuwa na mashindano ya bodaboda ambapo mshindi wa kwanza tutamkabidhi bodaboda mpya huku mshindi wa pili akinyakua kitita cha milioni 1 na mshindi wa tatu ataondoka na laki 5,na kila mshiriki wa bodaboda atapanda mti mmoja kwenye Milima hiyo”alimalizima kusema Mkurugenzi huyo.
Ifahamike miaka ya 70 Milima hiyo ya Uluguru ilikuwa na Mandhari nzuri huku ikitiririsha Maji sehemu mbali mbali za Milima hiyo.
Kufuatia hari hiyo Mwanamuziki Maarufu barani Afrika Mwenyeji wa Morogoro Hayati Mbaraka Mwinshehe aitunga wimbo wa kusifu Manzari nzuri wa Milima hiyo.
Kuanzia Miaka ya 2000 Milima hiyo ilianza kupoteza uzuri wake kufuatia baaadhi ya wenyeji wanaoishi juu ya Milima hiyo kuchoma Moto kwa kile kichotajwa kuandaa mashamba yao wanayolima juu ya Milima hiyo kando kando ya Mito hiyo inayotiririsha maji kuelekea Mikoa hiyo ya Pwani, Dar es salaam na Morogoro.
Baada ya kushamili kwa Vitendo hivyo vya uchomaji Moto aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Morogoro Miaka hiyo Mhe Dkt Nibuka Mzeru kwenye moja ya Michango yake Bungeni aliiomba serikali kuwahamisha wananchi wanaoishi juu ya Milima hiyo.
Kauli hiyo Mzeru ambaye ni Mluguru Og ilipigwa Vikari na waluguru wanaoishi juu ya Milima hiyo.wakiitaka serikali kama itakubari ushauri huo basi zoezi hilo la kuhamisha wananchi wanaoishi juu ya Milima lifanyike nchi nzima.
Baadhi ya wananchi wa wamelipongeza shirika hilo kwa kupanda kiwango hicho kikubwa cha miti kwenye Milima hiyo.
“ Binafsi nalipongeza sana shirika hilo kwa jambo hilo zuri wanalokwenda kulifanya ushauri wangu kwao wahakikishe miti hiyo inakuwa hivyo wanaopoipanda imwagiliwe maji ili isife kama unavyojua mvua vimekata jua ni kali”amesema Juma Athumani
No comments:
Post a Comment