Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Sunday, November 27, 2022

PADRI AWAPA MAKAVU WATU MSIBANI

                               Padri Elia akitoa karipio hilo

 


 

Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

 

PADRI wa kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro Padri Elia, katikati ya wiki hii amewapa Makavu baadhi ya watu wenye tabia ya kutoa mamilia ya pesa kwa marehemu  huku wakikacha kutoa msaada wa matibabu akiwa mgonjwa.

 

 Padri huyo ‘Janki’ alitoa kalipio hilo kwenye sehemu ya mahubiri yake aliyoyatoa kwenye msiba wa Marehemu Tonny Ntukula aliyeanza kuugua ugonjwa wa figo toka Mwaka 2021 hadi alipofariki dunia kwa ugonjwa huo juzikati Novemba 21-2022.

 

“Jambo jema na lenye faraja  kwa Jamii na mbele za Mungu  ni yule mtu anayetoa msaada wa Matibabu kwa Mgonjwa, kuna baadhi ya watu Mgonjwa anapohitaji Msaada wao wa pesa za kununua dawa wanakwepa lakini mgonjwa huyo huyo akifariki  watu  hao wanajitokeza kwa wingi wakishindano kutoa pesa nyingi za rambi rambi nahisi hizo pesa hazina msaada mkubwa kwa marehemu huyo zingekuwa na  msaada pale alipokuwa akiupigania uhai wake pale kitandani ”alisema Padri huyo na kupigiwa makofi  na baadhi ya waombolezaji waliofulika kwa wingi kwenye msiba wa Mpendwa wetu Tonny ‘Bonge’.Ntukula.

 

 Katika kukadhia kalipi hilo Mwenyekiti wa Kigango cha Mji Mpya Mzee Cosmas Damiani alipigia Msumari kwa kutoa ushahidi wa kweli wa tukio hilo.

 

“Padri umesema kweli mimi ninaushahidi wa  kweli wa jambo hilo,siku za nyuma nilikuwa na uguza mgonjwa wangu na pesa za matibabu zilihitaji laki mbili ili tuokoa maisha yake lakini kwa bahati mbaya pesa hizo zikuzipata kwa wakati hivyo  mgonjwa wangu akafariki dunia.

 

 Chaajabu kwenye msiba huo watu mbali mbali wakiwemo waliokuwa na taarifa za ugongwa huo walijitokea na kunipa rambi ramba za pesa kiasi cha milioni 2 na nusu sasa nikajiuliza pesa hizo wangenipa wakati ule wa ugonjwa  zingesaidi kwa kiwango kikubwa kuokoa maisha ya Mgonjwa wangu.

 

 Hakuna shaka yoyote kwamba baadhi ya watu wanakufa kwa kukosa msaada wa pesa za matibabu”alisema Mzee Damiani ambaye ni mmoja wa Vigogo wa kanisa Kuu la Mt Patrick Jimbo la Morogoro.

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...