Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Monday, February 27, 2023

MZEE MBEZI AWAKUBALI MAKOCHA 3 WA KAGERA SUGAR.

Kutoka kulia ni Kocha Mkuu wa Kagera Sugar Mecky Mexime, Kocha Msaidizi wa timu hiyo Ulimboka Mwakingwe, Mdau wa Soka Mkoani Morogoro Mzee Mbezi na mwisho ni Kocha wa Makipa wa Kagera Juma Kaseja kwa pamoja wakipozi mbele ya Kameea za kisasa za Mrandao huu

 


 

               Na Dustan Shekidele,Morogoro.

 

Mzee Omary Mbezi Mkazi wa Kichangani Manispaa ya Morogoro amevunja ukimya na kutoa lake la Moyoni kwamba anawakubali vilivyo makocha watatu wa timu ya Kagera Sugar.

Mzee Mbezi[Pichani mwenye kanzu] ambaye ndiye aliyetuzia kile Kiwanja tulichomjengea nyumba yule ndugu yetu Mlemavu Mohamed Matama.

 

Mara baada ya gemu ya  Ruvu Shooting na  Kagera Sugar iliyopigwa kwishoni mwa wiki  Uwanja wa Jamhuri Morogoro kukamilika kwa  Kagera kuwanyuka wenyeji wao Maafande wa Ruvu bao 1-0

 

 Mzee huyo shabiki ‘lia lia’ wa Mtibwa Sugar alishuka jukwaani kwa kasi na mkuvaa Mwandishi wa Mtandao huu akisema” Shekidele nawakubalisa sana makocha wale watatu wa Kagera najua unawamudu hivyo naomba msaada wako kawakusanye wote watu njoona hapa nipige nao pocha ya kumbuku”alisema Mzee huyo.

 

Mwandishi wa Mtandao huu yeye ni nani apigane na ombi na Mtu mzima huyo hivyo aliingia uwanjani na kuwakusanya makocha hao   akawapeleka kwa Mzee huyo na kuwapiga Picha.

 

Makocha hao ambao wote ni wakazi wa Kata ya Kihonda Maghorofani Manispaa ya Morogoro waliotimkia Kagera kutafuta Maisha kutoka kulia ni kocha Mkuu wa Kagera Sugar Meck Mexime, Kocha Msaidizi Ulimboka Mwakingwe[mwenye kanzu Mzee Mbezi, Kocha wa Makipa Juma Kaseja na wa mwisho kushoto ni Shabiki Kindaki ndaki wa Mnyama Simba Afande Mdoe.

Sunday, February 26, 2023

HUZUNI YATAWARA MAAFANDE RUVU SHOOTING WAKIPOKEA KICHAPO.

Baada ya mwamuzi kumaliza mchezo baadhi ya wachezaji wa Ruvu Shooting walijitupa chini kwa uchungu wa kufungwa nyumbani na Kagera Sugar
Wachezaji wawili wa Kagera sugar wakimfariji mchezaji wa Ruvu Kassim Suleman[aliyeketi chini]
Nahodha wa Ruvu Zuberi Daby akiinamisha kichwa chini kwa uchungu baada ya Mwamuzi kumaliza mchezo huo juzi.
Juma Kaseja [Kulia] akimfariji kocha msaidizi wa Ruvu.

 

 


 

                    Na Dustana Shekidele,Morogoro.

 

Huzuni imetawara baada ya Maafande wa Ruvu Shooting kupokea kichapo cha bao 1-0 dhidi ya wageni wao Kagera Sugar kwenye mchezo wa ligi kuu uliopigwa juzi uwanja wa Jamhuri Mkoani hapa.

 

Kichapo hicho kimeifanya timu hiyo ya Ruvu  kutoka  Mlandizi Mkoa wa Pwani kuendelea kuburuza mkia kwenye msimamo wa ligi hiyo inayoelekea ukingoni wakiwa na Pointi 17 huku Yanga inayoongoza ligi hiyo ikiwa na Pointi 65.

 

 Baada ya Mwamuzi kumaliza mchezo huo  baadhi ya wachezaji wa Ruvu walijiangusha chini kwa uchungu kwa kichapo hicho kinacho wasafishia njia ya kushuka daraja.  

 

Kufuatia hali hiyo baadhi ya wachezaji wa Kagera Sugar waliacha kushangilia ushindi huo na kubeba jukumu la kuwafariji wacheaji hao wa Ruvu.

 

Hali kadharika  Kocha msaidizi wa Kagera Sugar Juma Kaseja alitinga kwenye benchi la Ruvu na kumfariji kocha msaidi wa timu hiyo.

 

 Miongoni mwa mikakati ya maafande hao wa Ruvu ilikuwa kushinda michezo yote ya nyumbani wakipigania kutoshuka daraja, hivyo kupoteza mchezo huo muhimu nyumbani ndio sababu ya wachezaji hao kujawa na machungu moyoni.

 

 Baada ya mchezo huo Ruvu wanakwenda Mbeya kucheza mechi mbili ya kwanza watakipiga na Mbeya City huku gemu ya Pili wakikipiga na Tanzania Prisons timu zote hizo ziko kwenye janga la kushuka daraja.

 

Ruvu wakitoka Mbeya watareja nyumbani Morogoro kukipiga na ‘Wana ramba ramba’ Azam Fc inayopigania kushika nafasi tatu za juu.

 

Kwa mpangilio wa ratiba hiyo miujiza ya Mungu pekee ndio  inayohitajika kuinasua timu  ya Ruvu kujinasua na janga la kushuka daraja.

 

                               

 

 

 

Saturday, February 25, 2023

JAHAZI LA MAAFANDE WA RUVU SHOOTING LINAZIDI KUZAMA.

                                   Kikosi cha Ruvu Shooting
                              Kikosi cha Kagera Sugar
Wamuzi pamoja na Mech Kamishina[Kamisaa wa Mchezo] wakiwa katika picha ya pamoja na Manahodha wa timu zote mbili
Mashambuliaji wa Kagera Yusuf Mhilu akigombea Mpira na beki wa Ruvu


Mshambuliaji wa Ruvu Baraka Mtuwi [kulia] akitafuta m,binu wa kumtoka beki wa Kagera Meshack Abrahama




Baada ya mbinu zake kufeli kufuatia kubannwa  vilivyo na beki Meshack,
Bao la wazi kiungo fundi wa Ruvu Zuberi Daby Mkazi wa Kichangani Morogoro akiruka juu  kufunba bao huku kipa wa Kagera Ramadhan Chalamanda akipuyanga na kuliacha gori wazi.

Hata hivyo Daby alishindwa kufunga bao hilo kufuatia kuukosa mpira huo wa juu na kusababaisha mashabiki wa timu hiyo kubaki midomo wazi.




Bao la Kagera lilianzia hapa, Hamis Kiiza kulia akiunyatia mpira mbele ya beki wa Ruvu
Kiiza kafanikiwa kunasa mpira huo na kufunga bao la ushindi akimuacha kipa wa Ruvu lsihaka Hakimu akidaka nyasi za uwanja wa Jamhuri huku mpira ukitinga wavuni kama unavyoonekana Pichani mpira huo ukinasa kwenye nyavu

                Hamisi Kiiza 'Diezo[ akishangilia bao hio
                            .....Akipongezwa na wenzie




Furaha ya ushindi unapelekea wachezaji wa Kagera kubebena juu na jenga Mlima kama huo wa Uluguru unaoonekana pichani

....Wachezaji wa Kagera wakibusu mguu wa Kiiza uliofunga bao hilo la ushindi

Hamisi Kiiza akipozi mbele ya kamera pekee za Mtandao huu zilizokuwa nyuma ya gori la Ruvu

Hamiis Kiiza akichungwa na beki wa Ruvu

 


Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

Jahazi la Maafande wa Ruvu Shooting ya Mkoani Pwani linazidi kuzama baada ya jana kukubari kichapo cha bao 1-0 nyumbani dhidi ya wageni wao Kagera Sugar.

 

Wanajeshi hao wa Jeshi la Kujenga Taifa’JKT’ kutoka Mlandizi Mkoani Pwani walioamua kuutumia Uwanja wa Jamhuri  Morogoro kufuatia uwanja wao kukosa vigezo vya kutumika kwa michezo ya ligi kuu Tanzania Bara wanashika mkia kwenye ligi kuu wakiwa na alama zao 17.

 

Kwenye gemu hiyo ya Jana ‘Wajeda’hao walipambana kufa na kupota kusaka ushindi lakini walibanwa maeneo yote na Wakatamiwa hao kutoka Mkoani  Kagera hadi hadi dakika ya 89 timu hizo zilikuwa sale ya 0-0.

 

Wakati Mwamuzi  akijiandaa kupuliza kipenga cha kumaliza mchezo huo dakika ya 90 Mshambuliaji wa Kagera Sugar Hamis Kiiza’Diego’ raia wa Uganda  alipeleka majozi kwa Maafande wa Ruvu Shooting baada ya kufunga bao hilo pekee dakika hizo za mwishoni mwa mchezo.

 

Kama kawaida Mtandao huu umekusanya matukio kibao kwenye gemu hiyo ikiwemo tukio la wachezaji wa Kagera Sugar kuwabembeleza wachezaji wa Ruvu waliokuwa wamejiinamia baada ya mcheo huo kutamatika.

 

Kwa matukio yote hayo  endelea kuwa jirani na Mtandao Pendwa wa shekidele Muda wote.

 

 Kwa sasa fungua Profaili la Mtandao huu ushuhudia matukio mbali mbali ya mchezo huo ikiwepo picha ya bao hilo pekee.

Friday, February 24, 2023

TAA ZA BARABARANI M0RO ZAENDELEA KUHUJUMIWA.




 


 

             Na Dustan Shekidele,Morogoro.

 

Taa za barabarani Manispaa ya Morogoro zinazopendezesha Mji zinazidi kutoweka baada ya kukumbwa na hujuma mbali mbali zikiwemo kuibiwa na kugongwa na magari.

 

Juzi Mwandishi wa Mtandao huu Majira ya asubuhi akitokea maeneo ya Nane nane alikatiza barabara Mpya ya Kolla na kushuhudia taa mbili  zikiwa chini jirani na kituo cha Mafuta.

 

Mwanahabari huyo alitimiza majukumu yake ya Uandishi  kwa kuzipiga Picha taa hizo kisha kufanya mahojiano na Majirani wa eneo hilo kwa lengo la kujua taa hizo zimekubwa na kadhia gani, mashuhuuda hao walifunguka haya.

 

”Mara nyingi kunapokuwa na misafara ya Viongozi kwenye barabara ile ya Dar Magari mengi yakiwemo Malori hutumia njia hii ya Kolla, hivyo juzikati kuna Lori  lenye mzigo mkubwa baada ya kupishana na Lori lingine lilizidi kushoto na Kontena hilo likaziangusha taa hizi mbili”walisema mashuhuda hao ambao ni madereva wa boda boda wanaoegesha Pikipiki zao nje ya baa ya Vuga jirani na kituo cha Mafuta.

 

Walipoulizwa wao kama wananchi na taa hizo ni Mali ya wananchi zinazowasaidi kuwamulikia nyakati za usiku wamechukua hatua gani kuhusiana na tukio hilo la kihalifu? boda boda hao walijibu.

 

” Broo sisi tuchukue hatua gani kweli mwenye Lori baada ya kuzigonga taa hizi mbili alisimama kwa muda lakini baada ya kuona hakuna mtu yoyote anayemfuta na kumueleza lolote alipiga gia kaondoka, hatujua kama amekwenda kwenye mamlaka kulipa taa hizo au amekimbia”

 

Chaajabu siku iliyofutaa Majira hayo hayo ya asubuhi Mwanahabari huyo alikatiza tena eneo hilo na kushuhudia taa nyingine  ikiwa chini jirani eneo la  Maegesho ya Malori Kando kando ya barabara kuu ya Moro-Dar jirani na Uwanja wa Maonyesha ya Wakulima Nane Nane.

 

Moja ya kazi ya Uandishi wa habari ni pamoja na Upelelezi endelevu hivyo Muda huu wa asubuhi najianda kupita tena eneo hilo kuchunguza kama kuna taa nyingine imeangushwa chini au la.

 

 Uchunguzi wa awari uliofanywa na Mtandao huu umebaini taa moja gharama yake ni Shilingi Milioni 3.

 

lkumbukwe barabara hii inyaoelekea makaburi ya Kolla inayoanzia eneo la Nane nane barabara Kuu ya Moro-Dar na kuishia barabara ya zamani ya Dar ikikatiza eneo la Bingwa  imejengwa kwa kiwango cha lami 2018.

 

Mwaka uliofuta 2019 Vibaka walivamia eneo la Makaburi ya Kolla na kuiba Taa kadhaa ambapo Jeshi la Polisi lilifanya doria nyakati za usiku na kufanikiwa kuwakamata vibaka hao na kuwapeleka mahakama kwa kesi ya uhujumu  uchumia.

 

Baada ya Jeshi la Polisi kufanya kazi hiyo nzuri matukio hayo ya wizi wa taa hizo za solla umekoma kwa sasa taa hizo zinapukutika kwa kugongwa na magari.

 

Mtandao huu unawakumbusha TARURA kutinga eneo hilo la tukio zilipo taa hizo na kuzifunga tena zisije zikaibiwa.

Tuesday, February 21, 2023

MAADHIMISHO YA SIKU YA WAPENDANAO DUNIAN’VALENITINE DAY’WALEMAVU WABANA VIONGOZI WAO AHADI YA BIMA YA AFYA.

Bi Pili Mohamed akiulizwa swali juu ya ahadi ya Bima ya Afya kwa wanachama wa cahma hicho cha Walemavu




Mkurugenzi wa MODICO Ngungamtitu akimjibu Bi Pili
 


 

Na Dustan Shekidele,Morogoro.

 

WALEMAVU kupitia Taasisi yao ya Morogoro Disability Devolopment and lmfomation Center Organization, ikiwa na maana ya Taasisi ya Maendeleo na Upashaji Habari kwa Watu  wenye Ulemavu[MODICO] wametoa sauti kali wakiwakumbusha Viongozi wao juu ya Bima zao za Afya.

 

 Hali hiyo imetokea kwenye hafla ya Siku ya Wapendanao ‘Valentine Day’iliyofanyika Februari 14 kwenye ukumbi wa Young Women Christian Association [Y.W.C.A.]Uliopo jirani kabisa na geti kuu la hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro ambapo siku hiyo Walemavu hao kupitia umoja wao huo wa MODICO waliamua kujinadalia sherehe ya kuonyeshana Upendo wenyewe kwa wenyewe kwenye kilele cha siku hiyo ya wapendao duniani.

 

Kwenye hafla hiyo Viongozi wa MODICO walitoa nafasi ya wanachama wao kuliza maswali kwa Viongozi wao baada ya nafasi hiyo kutolewa Walemavu wengi walinyoosha vidole wakiomba nafasi ya kuliza maswali ambapo  Bi Pili Mohamed alikuwa wa kwanza kupewa nafasi hiyo aliuliza swali la ahadi ya Bima za Afya waliohadiwa toka Mwaka jana na Viongozi wa Manispaa ya Morogoro.

 

 Akijibu swali hilo Mkurugenzi Mkuu wa MODICO Othuni Ngungamtitu alidai kwamba nao wanapigwa danadana na Viongozi wa Manispaa  akiwaomba wanachama wake hao walemavu kuendelea kuwa na uvumilivu wakati juhuzi zao za kulifuatilia jambo hilo zikiendelea.

 

Baada ya kikao hicho Mwandishi wa habari hizi alifanikiwa kuzungumza na Mkurugenzi huyo ambapo aliendelea kufafanua jambo hilo kwa kusema.

 

“ Wanachama wangu wanahaki ya kuuliza ishu hiyo ya Bima ya Afya kwa jazba, pale ndani nimeshindwa kufafanua zaidi lakini kwa vile umeniuliza acha nikupe ukweli ni kwamba  April 12 2022 [Mwaka jana] tulikaa kikao chetu cha kwanza kilichohudhuriwa na wanachama 51

 

Kwenye kikao hicho tuliwaalika Vigogo wa Manispaa kutoka Vitengo mbali mbali a ambapo alifika Afisa wa Maendeleo ya Jamii TASAF, alifika pia Afisa wa kitengo cha Bima ya Afya Manispaa, alikuwepo Afisa anayeshungulikia Mikopo ya asilimia 2 ya watu wenye ulemavu kutoka Manispaa.

 

Kwenye kikao hicho Walemavu wenzangu alimuomba Afisa huyo wa Bima ya Afya kuwasaidi kadi za bima ya Afya ambapo dada huyo alikubali ombi hilo mbele ya kikao hicho lakini cha ajabu kila nikimpigia simu  anadai  swala hilo ameshalifikisha kwa Mkurugenzi wa Manispaa hiyo anasuburi majibu”alisema Mkugurunzi huyo wa MODICO.

Kwa sauti ya upole Mtandao huu unaomba wahusika wote wa Bima  ya Afya kuyatazama maombi ya ndugu zetu hao  kwa jicho la huruma.

 

Ingia kurasa za facebook za Dustan Shekidele na ile ya shekidele Mkude Simba uangalia Clip Video za tukio hili A-Z

Thursday, February 16, 2023

MKURUGENZI WA TAASISI YA WALEMAVU AFUNGUKA ISHU YA WATOTO OMBA OMBA KULAWITIWA


 Kaiumu Mkurugenzi Mjuu wa NODICO Bi Stella Kisala akizungumzia ishu hiyo, msiki Mubashara kwenye Clip Video kwenye facebook za Dustan Shekidele na Shekidele Mkude simba

 

 

 

Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

Maadhimisho ya siku ya wapendanao dunia’Valentine Day’Taasisi ya Walemavu ya Morogoro Disability Devolopment and  lmformation Center Organization’MODICO’imefanikiwa kuonyesha Upendo kwa Watoto 30 wanaoishi kwenye mazingira magumu kwa kuwatoa mtaani na kuwapeleka shuleni.

 

Akizungumza kwenye hafra ya kusheherekea Valentine Day waliojiandalia wenyewe kupitia taasisi yao ya MODICO wakiwa na lengo la kuonyeshana Upendo wenyewe kwa wenyewe Siku hiyo ya Wapendanao, kaimu Mkurugenzi wa  MODICO Stella Kisala alifunguka mazito juu ya watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu akigusia ishu ya Ulawiti huku akidai wameshafanikiwakuwanasua watoto 30 wanaoishi kwenye mazingira magumu.

 

 Msikie Mkurugenzi huyo akifunguka mazito juu ya tukio hilo  kwenye kurasa za facebook za Dustan Shekidele na ile ya Shekidele mkude simba

 

 

 

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...