Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Tuesday, February 21, 2023

MAADHIMISHO YA SIKU YA WAPENDANAO DUNIAN’VALENITINE DAY’WALEMAVU WABANA VIONGOZI WAO AHADI YA BIMA YA AFYA.

Bi Pili Mohamed akiulizwa swali juu ya ahadi ya Bima ya Afya kwa wanachama wa cahma hicho cha Walemavu




Mkurugenzi wa MODICO Ngungamtitu akimjibu Bi Pili
 


 

Na Dustan Shekidele,Morogoro.

 

WALEMAVU kupitia Taasisi yao ya Morogoro Disability Devolopment and lmfomation Center Organization, ikiwa na maana ya Taasisi ya Maendeleo na Upashaji Habari kwa Watu  wenye Ulemavu[MODICO] wametoa sauti kali wakiwakumbusha Viongozi wao juu ya Bima zao za Afya.

 

 Hali hiyo imetokea kwenye hafla ya Siku ya Wapendanao ‘Valentine Day’iliyofanyika Februari 14 kwenye ukumbi wa Young Women Christian Association [Y.W.C.A.]Uliopo jirani kabisa na geti kuu la hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro ambapo siku hiyo Walemavu hao kupitia umoja wao huo wa MODICO waliamua kujinadalia sherehe ya kuonyeshana Upendo wenyewe kwa wenyewe kwenye kilele cha siku hiyo ya wapendao duniani.

 

Kwenye hafla hiyo Viongozi wa MODICO walitoa nafasi ya wanachama wao kuliza maswali kwa Viongozi wao baada ya nafasi hiyo kutolewa Walemavu wengi walinyoosha vidole wakiomba nafasi ya kuliza maswali ambapo  Bi Pili Mohamed alikuwa wa kwanza kupewa nafasi hiyo aliuliza swali la ahadi ya Bima za Afya waliohadiwa toka Mwaka jana na Viongozi wa Manispaa ya Morogoro.

 

 Akijibu swali hilo Mkurugenzi Mkuu wa MODICO Othuni Ngungamtitu alidai kwamba nao wanapigwa danadana na Viongozi wa Manispaa  akiwaomba wanachama wake hao walemavu kuendelea kuwa na uvumilivu wakati juhuzi zao za kulifuatilia jambo hilo zikiendelea.

 

Baada ya kikao hicho Mwandishi wa habari hizi alifanikiwa kuzungumza na Mkurugenzi huyo ambapo aliendelea kufafanua jambo hilo kwa kusema.

 

“ Wanachama wangu wanahaki ya kuuliza ishu hiyo ya Bima ya Afya kwa jazba, pale ndani nimeshindwa kufafanua zaidi lakini kwa vile umeniuliza acha nikupe ukweli ni kwamba  April 12 2022 [Mwaka jana] tulikaa kikao chetu cha kwanza kilichohudhuriwa na wanachama 51

 

Kwenye kikao hicho tuliwaalika Vigogo wa Manispaa kutoka Vitengo mbali mbali a ambapo alifika Afisa wa Maendeleo ya Jamii TASAF, alifika pia Afisa wa kitengo cha Bima ya Afya Manispaa, alikuwepo Afisa anayeshungulikia Mikopo ya asilimia 2 ya watu wenye ulemavu kutoka Manispaa.

 

Kwenye kikao hicho Walemavu wenzangu alimuomba Afisa huyo wa Bima ya Afya kuwasaidi kadi za bima ya Afya ambapo dada huyo alikubali ombi hilo mbele ya kikao hicho lakini cha ajabu kila nikimpigia simu  anadai  swala hilo ameshalifikisha kwa Mkurugenzi wa Manispaa hiyo anasuburi majibu”alisema Mkugurunzi huyo wa MODICO.

Kwa sauti ya upole Mtandao huu unaomba wahusika wote wa Bima  ya Afya kuyatazama maombi ya ndugu zetu hao  kwa jicho la huruma.

 

Ingia kurasa za facebook za Dustan Shekidele na ile ya shekidele Mkude Simba uangalia Clip Video za tukio hili A-Z

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...