Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Sunday, July 31, 2022

UJUMBE WA MUNGU KWETU SISI WANADAMU


 

WAGALATIA  5-17

“Kwa sababu Mwili hutamani,ukishindana na roho na roho kushindana na mwili,kwa Maana hizi  zimepingana, hata hamwezi kufanya Mnayotaka” Hilo ndilo neno letu la leo Jumapili ya Julai 31.

 

 Ujumbe huyo wa Mungu unatufundisha kwamba kuna vita kubwa ya matamanio kati ya Mwili na Roho.

 

Tunapaswa kuyashinda matamanio ya Mwili ili tubaki kuwa na roho safi jambo ambalo litatupa tiketi ya kufika Peponi.

 

 Kuna baadhi ya watu wanakosema wakisema nafanya mema ili niende mbinguni nawakumbusha kwamba sote tutakwenda mbinguni  sisi wenye dhambi na tusio na dhambi.

 

 

Tukifika huko matendo yetu ndio yatakayotuingia Peponi au  Jehanamu ya Milele,hukumu hiyo itatenganisha, Mafuta na Maji, Magugu na Ngano, wenye dhambi na wasio na dhambi.

 

Kumbe basi matendo yetu ndio yatakayotupeleka Peponi au Motoni hivyo hata  uzikwe na jeneza la dhahabu kama matendo yako yatakuwa ya dhambi hilo jeneza au wengi wawatu waliokuja kukuzika hayo hayata badilisha hukumu ya Mungu juu ya matendo yako uliyoyafanya ukiwa hai.

 

 

Baada ya kupita hukumu hiyo isiyo na upendeleo wenye dhambi tutatupa jehanamu kwenye hukumu ya Milele na wenye haki tutaweka Poponi kwenye raha za Milele.

 

 Natambua roho iradhi  kuyashinda matamanio lakini Mwili ni dhaifu, hivyo  nakusia na kuihusisi pia nafsi yangu tusikubali tushindwa na matamanio ya Mwili yatakayotuingia kwenye hukumu ya Milele.

 

Tamaa zinazo zungumzia hapo ni pamoja na  tama za mwili, Mali na dhuruma

Saturday, July 30, 2022

KUMBUKIZ YA BABA WA TAIFA MWL NYERERE.

Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akiwa na usafiri wa baiskeli
Mwandishi wa Mtandao huu akiwa mtaani na usafiri wake wa baiskeli
 

KUMBUKIZI.
Rais wa awamu ya kwanza Tanzania, Hayati Julius Kambarahe Nyerere ama kwa hakika alikuwa si mtu wa kujikweza’Kujimwambava’ kujilimbikizia Mali licha ya kuwa na madaraja makubwa ya Urais.
 
Pichani Mwalimu Nyerere akiendesha baiskeri ikiwa ni njia moja wapo ya yeye kufanya mazoezi ya Viungo.
Pichani Kulia Mwandishi wa Mtandao huu amerithi jambo hilo kwa hayati Mwalimu Nyerere kwa kutembelea usafiri wa baiskeri.

Wednesday, July 27, 2022

KWA USAJIRI HUU WA MARCELO COASTAL UNION WAMERAMBA DUME.

Mfadhiri wa Coastal Union Tajiri Nassoro Salum Binslum[kushoto] akimkabidha mkataba  Marcello mara baada ya kusainiwa na pande zote mbili

 Marcello akiambaa ambaa na Mpira na guu lake la shoto


 

 Na Dunstana Shekidele,Morogoro.

 

 

Wakati dirisha kubwa la Usajiri likielekea Ukingoni timu kongwe nchini Coastal Union ya Jijini Tanga’ Wanamangushi’ a.k.a Wagosi wa Kaya’  wiki end iliyopita wamefanikiwa kumsajiri beki chipukizi Omary Mbaruku Maarufu Marcello kutoka timu ya daraja la kwanza ya Fountain Gate ya Jijini Dodoma.

 

 lfahamike Marcello kabla ya kujiunga na Fountain Gate Miaka miwili iliyopita alikuwa akiitumikia timu ya Mawenzi Market ya Mkoani Morogoro iliyokuwa akishiriki pia ligi daraja la kwanza, hivyo wadau wa soka Mkoani Morogoro akiwemo Mwandishi wa habari hizi wanamfahamu vizuri Mchezaji huyo.

 

 

Hivyo kwa kinywa kipana pasina shaka yoyote Coastal kunasa saini ya mchezaji huyo Mwenyeji wa Visiwa vya Pemba Zanzibar anayemudu vyema kucheza beki ya kushoto wameramba dume.

 

Wakati akiwa Mawenzi Mwandishi wa Mtandao huu alimfuatilia  mchezaji huyo anayetumia mguu  wa kushoto,mwenye  kasi ya ajabu ya  kupanda na kushuka huku akimwaga Krosi kali kwenye lango la wapinzani.

 

 

 

 

Kufuatia hali hiyo Mashabiki wa Mawenzi walimpachika jina la Marcello wakimlinganisha na aliyekuwa beki kisiki  wa Real Madrid ya Hispani anayecheza beki ya kushoto anayetumia pia mguu wa kushoto Marcello Vieira Da Salva Raia wa Brazil.

 

 

Baada ya kujiunga na Coatal Union Jumapili iliyopita siku iliyofuata [Jumatatu] Mwandishi wa Mtandao huu alimtwangia simu Marcello.

 

 

“ Shekidele ni kweli jana nimejiunga na Coastal  kwa Mkataba wa Miaka 2  kwa sasa niko Kambini Tanga na timu yangu hiyo Mpya”alisema mchezaji huo na kuendelea kufunguka.

 

 

“Kwa mafanikio haya ya kusajiriwa na timu kubwa ya Coastal  inayocheza ligi kuu, kipekee namshukuru Mwenyezi Mungu, Ndugu  zangu, Mkurugenzi wangu wa Fountain Gate  Jaftet Makau na Viongozi wa Mawenzi Market, wachezaji wenzangi wa Mawenzi na mashabiki wote wa Mawenzi.

 

     

Kipekee nivishukulu vitu vya soka vilivyoibua Kipaji changu toka nikiwa mdogo.

 

Vituo hivyo ni Kisa cha nyumbani Pemba na Taasisi ya Mseti Foundation ya Jijini Dar.

 

  Nitakuwa mchoyo wa fadhira nisipokushukuru wewe Shekidele Mwandishi bora wa habari za michezo umekuwa karibu sana na mimi licha ya kuhama Morogoro ubarikiwe sana”alisema  Marcello.

 

 Ahadi yangu kwa umma wawatanzania ndani ya miaka hiyo 2 Coastal watamuuza beki huyo kwa pesa ndefu  kwa timu kubwa nchini, hilo linaweza kushindikana kama Omary Marcello anabadilika kitabia na kulewa sifa za mafanikio.

 

 

Na amini hilo haliwezi kutokea kwa sababu  namfahamu Omary ni Mcha mungu Mzuri mwenye hofu na Allah, si Mjivumi na wala sio mlevi, hana Mambo Mengi ya tamaa za Mali na Mapenzi ni Mtu Smart.

 

Mtandao huu unamuombe kila lenye kheri kwenye mafanikio yake ya kucheza ligi kuu kwa mara ya kwanza kwenye histori ya maisha yake.

 

 

Dirisha kubwa la Usajri nchini lilifunguliwa Julai 1 na linafungwa Julai 31 huku pazia la ligi kuu likirajiwa kuzinduliwa Agost 13 kwa mchezo wa ngao ya Jamii kwa mpambano wa watani wa Jadi Simba na Yanga. huku ligi hiyo ikitarajiwa kuanza Agost 17.

              

Tuesday, July 26, 2022

KUMBUKIZI MSANII WASTARA WA SAJUKI

Wastarav wa Sajuki akiomba kura kwenye kampenzi za uchaguzi mkuu wa Mwaka 2015

 Mwandishi wa Mtandao huu kulia akizungumza na Wastara wa Sajuki


Hii ni miaka 7 iliyopita kwenye uchaguzi Mkuu wa Tanzania mwaka 2015 WASTARA wa Sajuki alijitosa kugombea Ubunge viti Maalumu kupitia leseni ya Chama Cha Mpinduzi'CCM' Mkoa wa Morogoro.

 

 

Pichani Wastara  akiomba kura kwa wajumbe kwa unyenyekevu mkubwa. Hata hivyo licha ya Unyenyekevu huo Wastara hakufanikiw akutinga mjengoni Dodoma baada ya kura zake za ndio kuwa chache hazikutosha kumpela Mjengoni.

 

 


 

Sunday, July 24, 2022

HII SI MIPASHO NI MANENO YA MWENYEZI MUNGU KUPITIA KITABU KITAKATIFU CHA BIBLIA.


 

Mwandishi wa Mtandao huu akizungumza na Mtumishi wa Mungu Mambo ya kiimani na Askofu wa KKKT Jimbo la Morogoro Jacob Ole Mameo, mara baada ya kukamilika kwa lbada KKKT Usharika wa Mji Mpya.

 

 

                    MATHATO 7-1-5

 

KUWAHUKUMU WENGINE.

 

“Msihukumu Msije mkahukumiwa ninyi.

Kwa kuwa hukumu ile  muhukumuyo.

ndio mtakayo hukumiwa na kipimo kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa.

 

 

Basi mbona wakitazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako,na boriti  iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe hujaiangalia.?

Au utamwambiyaje  nduguyo  niache  nikutoe kibanzi  katika jicho lako   na kumbe mna boriti ndani ya jicho lako mwenyewe.?

 

 

Mnafiki wewe,itoe kwanza ile boriti katika  jicho lako mwenyewe  ndipo utakapoona vema kukitoa kile kibanzi katika jicho la ndugu yako.” Hilo ndilo neno letu la Jumapili ya Julai 24.

 

 

Sina cha kuongeza kwenye neno hilo limejitosheleza ninachoweza kusema ni kwamba Mwenye Masikio na asikie asiye na Masikio………]

                   


MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...