Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Saturday, April 30, 2022

MICHUANO YA UNDER TWENTY 2022 MORO.

Kikosi cha Moro Kids Vijana wanaodaiwa kuwa na Umri chini ya Miaka 20
Kikosi cha Black Viba Vijana wanaodaiwa kuwa chini ya Umri wa Miaka 20











 Super Sub Messi wa Vibandani akiinvgia uwanjani kuchukua nafasi ya Mtu
 


 BLACK Viba’Weusi wa Vibandani’ walivyoihenyesha Moro Kids kwenye Michuano ya Vijana Chini ya Miaka 20 ’Under Twenty’yanayoendelea kutimua vumbi Uwanja wa Saba saba Manispaa ya Morogoro.Picha zote na Dunstan Shekidele,Morogoro

Thursday, April 28, 2022

KIGOGO MRFA ATOA NENO MICHUANO YA VIJANA CHINI YA MIAKA 20.


Katibu Mkuu wa MRFA Mch Kimbawala akizungumza na timu shirikia mara baada ya kuzindua mashindano hayo. Picha no 3 ni Makundi 4 ya timu shiriki wenyeji na waalikwa.
 
Baadae Picha za matukio ya gemu ya ufunguzi kati ya Moro Kids na Black Viba zitaruka hewani hivyo endelea kuwa jirani na Mtandao huu muda wote


 


                    Na Dunstan Shekidele,Morogoro. 
 
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Soka Mkoa’MRFA’ Mch. Emmanuel Kimbawala ameupongeza Uongozi wa Chama Cha Soka Wilaya ya Morogoro’MDFA’ kwa kutii maagizo ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania’TFF’ ya kuzitaka wilaya zote nchini kuandaa michuano ya Vijana na Soka la Wanawake kwenye Maeneo yao.
 
Akizungumza kwenye Ufunguzi wa Michuano hiyo inayofanyika uwanja wa Saba saba Manispaa ya Morogoro Mchungaji Kimbawala alisema.
 
“Naupongeza Uongozi wa Chama cha Soka Wilaya ya Morogoro kuandaa mashindano haya ambayo ni maagizo kutoka TFF waliotupatia sisi Viongozi wa Mkoa na sisi tukatoa maagizo kwa wachini yetu kwa maana ya Wilaya”alisema Kimbawala na kuongeza. 
 
“ Kwa upande wenu nyinyi Vijana hii ni fursa ya kuibua Vipaji vyenu kwa sasa mpira unalipa vizuri na niwaibie siri kuna mawakala kibao wanafuatilia mashindo haya”alisema Katibu huyo ambaye kitaaluma ni Mwalimu.
 
Michuano hiyo ya Vijana chini ya Miaka 20 inayojulikana kwa jina la ‘Under Twenty Legue’ inashirikisha timu 25 huku timu 4 zikitoka Wilaya nyingine baada ya maombi yao kuomba kushiriki ligi hiyo kukubaliwa na kamati ya ligi. 
 
Timu hizo ni Pwani Sporty Foundation na Ruvu Shooting kutoka Mkoa wa Pwania. Kilombero Soccer Net kutoka Wilaya ya Kilombero na Mtibwa Sugar Kutoka Wilaya ya Mvomero.

Wednesday, April 27, 2022

KATIBU MKUU MRFA AZINGIA MICHUANO YA VIJNA CHINI YA MIAKA 20'


 

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Soka Mkoa wa Morogoro’MRFA’ Mchungaji Emmanuel Kimbawala leo Jioni amezindua Michuano ya Vijana wenye Umri chini ya Miaka 20[Under 20].
 
Uzinduzi wa Michuano hiyo unaoshirikisha timu kutoika Mikoa ya Morogoro na Pwani inafanyika katika Uwanja wa Saba saba Manispaa ya Morogoro. 
 
Katika Mchezo wa Ufunguzi Vijana wa Black Viba kutoka Kata ya Mbuyuni eneo la Vibandani wameichapa timu ya Moro Kids kwa bao 1-0. 
 
Habari zaidi na Picha za matukio mbali mbali ya ufunguzi wa Michuano hiyo zitaruka hewani hivi Punde hivyo endelea kuwa jirani na Mtandao huu muda wote. 
 
Picha kushoto Katibu huyo akikagua timu ya Black Viba
Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

Tuesday, April 26, 2022

WAMASAI WADAI HAJI MANARA AMEVAA VAZI LA KIMASAI LA KIKE.


Mwandishi wa Mtandao huu[kushoto] akimpongeza Kiongozi Mkuu wa Kabila la Wamasai anayeongoza wamasai wa Mikoa ya Morogoro. Dodoama. Singida, Manyara na lringa Mara.

 

 Shughuri hiyo ya kumsimika Kiongozi huyo Mkuu wa kabila la Wamasai mwenye cheo cha ‘Raibon’ alifanyika Wilayani Kilosa.

Hafra  hiyo ilifanyika kwenye zizi la Ng’ombe ilihudhuriwa na Viongozi wa Chama cha Mapinduzi na Serikali ya Mkoa wa Morogoro.

 

Akiwemo Mkuu wa Mkoa na aliyekuwa katibu Mkuu wa CCM Mkoa wa Morogoro Shaka.  A. Shaka ambaye kwa sasa ni Katibu Mwenyezi wa CCM Taifa.

 

Mara baada ya kusimikwa kiongozi huyo alipewa ulinzi Mkali wa Jeshi la Polisi chini ya OCD wa Kilosa kulia aliyevaa Kaunda Suti.



 ....Mwandishi wa Mtandao huu kushoto akisalimiana na baba yoyo


 

Na Dunstan Sherkidele,Morogoro.

 

BAADHI ya Wamasai wameibuka na kudai  vazi la Kimasai ambalo Msemaji machachari wa Yanga Haji Manara alilivaa jana ni la Kike.

 

Wakati Mwandishi wa Mtandao huu anamsikiliza Haji Kupitia Luninga kwenye baa moja aliyopo pande a Mji Mpya ambayo inamilikiwa na Mmasai akihamasisha mashabiki wa Yanga kujitokeza kwa wingi kwenye gemu yao dhidi ya Simba itakayopigwa Jumamosi  Saa 11 jioni.

 

Alijitokeza Kijana mmoja wa kimasai  akidai vazi la kimasai alilovaa Haji ni la Kike, baada ya kusikia hivyo Mwandishi wa habari hizi alimsogelea Kijana huyo alipotakiwa kuthibisha jambo hilo alisema.

 

“Mimi ni Yanga damu siwezi kumnanga msemaji wa timu yangu lakini ukweli ni kwamba Vazi hili alilovaa Haji ni la Kike na sehemu kumbwa ya mapambo hasa hilo la kichwani na shingoni ni mapambo ya Mama yoyo labda hilo Pambo la mkononi pekee ndio  la Kiume kama huamini Shekidele mulize Mmasai yoyote atakuthibitishia hilo”alisema Kijana huyo aliyejitambulisha kwa jina Moja la Moses.

 

 

 Juhudi za Mwandishi wa Mtandao huu za kumpata Haji Manasa kuzungumzia jambo hilo ziligonga Mwamba ingawa juhuzi za kumtafuta bado zinaendelea ili tupate ufafanuzi kutoka kwake.


Sunday, April 24, 2022

UJUMBE WA NENO LA MUNGU LEO JUMAPILI YA APRIL 24.



 


 

“Basi wekeni Mbali Uovu  wote na hila yote na unafiki na husuda na Masingizio yote.  

 

Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa  yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu” Maneno Matakatifu kutoka 1Petro 2. 1-2.

 

Neno hilo la Mungu linatufundisha yafuatayo,tuache Uovu, Pili tudumu kwenye Wokovu tutakapoimaliza safari yetu ya hapa duniani.

 

Kumbe basi tunakumbushwa kwamba Pesa zetu, Mali zile watoto wetu au ndoa zetu haziwezi kutupeleka Peponi bali Wokovu ndio pekee utakao tupeleka Peponi.

 

 

Usijidanganye kwamba Kuishi nyumba Moja na Askofu, Padri au Mchungaji kutakupa tiketi ya kufika Pepoli ‘No’, Matendo yako mema ndio yatakayokupa kibali cha kufika Peponi.

 

Pia usijidanganye kwamba  kuolewa na Askofu au Mchungaji ndoa hiyo itakupa kibali cha kufika Peponi hapana, nakukumbusha matendo yako Mema ndiyo pekee yatakayo kufikisha kwenye Pepo ya Mwenyezi Mungu. 

 

Hali kadharika Kuwa kiongozi wa dini Askofu, Padri, Mchungaji, Mwinjilisti, Kasisi, Katekista au Palishiweka cheo hicho hakikupi tiketi ya kufika Peponi Matendo yako Meme ndio pekee yatakayofikisha kwenye Uzima wa Milele.

 

 

Tena nyinyi viongozi wa dini mkienda kinyume na Wokovu mtahukumiwa zaidi mtaingizwa Jehanamu na kutupwa kwenye moto mkali Biblia ilionya.

’Ole wao  watakao kuwa Vugu vugu Moto si Moto baridi si baridi.’

 

Ninayo yakemea kwa wenzangu nayakemia pia kwenye nafsi yangu, nami najichana ‘Live’ najipiga ngumi kwenye mshono.

 

 

 Shekidele nisijidanganye kwamba kitendo  cha kuruhusu kanisa kujengwa  eneo la nyumba yangu kitanipa  tiketi ya kufika Peponi hapana.

 

 Japo namini hilo  nalo ni jambo jema laki Pekee  haliwezi kunipa kibari cha kufika Peponi natakiwa kuendeleza mema zaidi siku zote za maisha yangu mpaka hapo Mungu atakapo kata punzi yangu ya kuishi hapa chini ya jua.

 

Miaka ya hivi karibuni Uongozi wa Kanisa la Tanzania Assemblies Of God’T.A.G Jimbo la Morogoro walifika nyumbani na kuomba kujenga Kanisa nje ya nyumba yangu na mimi bila kinyongo niliwakubaria kwa moyo mmoja ambapo mpaka sasa huduma inaendelea kwenye kanisa hilo.

 Wiki iliyopita kulifanyika Mkutano Mkubwa wa lnjiri nje ya kanisani hilo ambapo kuna uwanja mkubwa.

Mungu atusaidie tusitumie nguvu na akili nyingi  kuyatafuta na kuyatamani Maisha ya dunia.

 Kwa Neema zake atuongoze tutumie akili na nguvu nyingi kuyatafuta  Maisha ya Mbinguni ambayo tunaamini ndio maisha marefu zaidi tofauti na maisha ya hapa duniali  yaliyojaa shida na damu nyingi.

 

Wednesday, April 20, 2022

KUMBUKIZI.




 


Dogo mwenye umri wa miaka 15 [kwa sasa ana miaka 20] Junior ,Msara kutoka Dar alikuwa kivutia kwenye mashindano ya Pikipiki yaliyofanyika uwanja wa Saba Saba Mkoani hapa sikuu ya ldd Mosi ya Mwaka 2017.
 
Miaka hiyo ya nyumba Mratibu wa shoo ya kuruka Moto wa Pterol kwa kutumia Pikipiki Athuman Mahita kila sikuu ya ldd aliandaa shoo hiyo akishirikisha madereva wakali kutoka Dar.Morogoro na Mmoja kutoka DR Congo. 
 
Toka Mwaka 2020 shoo hiyo haikufanyika na kwamba aliyekuwa Mratibu Mkuu wa Shoo hiyo Athuman Mahita kwa miaka ya hiivi karibuni hajaonekana Mkoani hapa hivyo tunahisi amehama Mkoani Morogoro.
 
Wiki ijayo ni sikuu ya ldd wanamoro tulitamani michezo hiyo miwepo tupata sehemu ya Mtoko kwani sisi wengine sio watu wa Grosary ukituona huko tuko kikazi Mlala Nje si si vinginevyo.

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...