Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Friday, April 3, 2026

MAJAJI 2 WAHUDHURIA IBADA YA KUMUOMBEA KIGOGO WA SUA MAREHEMU DKT MBILU.

         Mchungaji Dkt Rhoda Chamshama akiongoza ibada hiyo
Katibu Mkuu wa  KKKT Usharika wa Mji Mpya Mshana akimuaga Mzee wake wa kanisa
Shabiki wa Simba akimuada Mdau mkubwa wa Soka hayati Mbili
.... Shabiki wa Yanga naye akitoa heshima zake za Mwisho
Kundi la baraza a Wazee usharika wa Mji Mpya kwa pamoja wakipita mbele ya jeneza wakimuaga mwenzao aliye twaliwa na bwana baada ya kumaliza kazi

....Inauma sana aishee hiki ni kipengele kigumu, Mhe Regina Futakamba akiwaogoza wanaye kupita mbele ya jeneza kumuaga mpendwa baba yao
...Mtoto  wa marehemu aliyeshika msalaba akiwaongoza waombezaji kutoka ndani ya kanisa baada ya ibada kutamatika juzi
Wazee wa kanisa wakiingiza mwii wa mwenzao kwenye gari tayari kwa safari ya kwenda kumpunzisha kwenye nyumba yake ya milele
                            Watoto wakiwa na shada a maua
                              .... Nje ya kanisa ni vilio tu
....Mtoto wa mwisho wa marehemu toka tukiwa kwenye mkesha nyumbani kwa SUA usiku kucha alimlilia mpendwa baba yake, pichani akibembelezwa na dada yake
                          Hayati Dkt Mbilu enzi za uhai wake
              Mke wa Mrehemu Mhe Futakamba aitka kanisani
Matalumbenda kutoka KKKT Usharika wa Kolla wakiimba baada ya kutoka kanisani




                      Na Dunstan Shekidele.

WAHESHIMIWA Majaji wawii wa Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro  na Mahakama ya Rufaa  wameshiriki lbada  ya kumuombea na kumuaga Kigogo wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine’SUA’ Dkt Zenu John Mbilu[53]iliyofanyika juzi kanisa la KKKT Usharika wa Mji Mpya mkoani hapa.

 

Hayati Mbilu aliyekuwa Mteknojia Mkuu wa Mahabara [SUA], Kiongozi wa kanisa KKKT Usharika wa Mji Mpya na Mdau Mkubwa wa Soka Mkoani Morogoro alifariki  March 30 akiwa njiani kuelekea Muhimbili baada ya kupewa Rufaa kutoka Hospital ya Rufaa Morogoro,

 

 Akizungumza kwenye Ibada hiyo kaka wa Marehemu  alisema.

 

Mdogo wake alianza kuugua March 27  wakampeleka hospital ya SUA na kwamba March 29  hali yake iliendelea kuwa mbaya hivyo akapewa Rufaa ya kwenda hospital ya Mkoa.

 

Amesema huko pia hali iliendelea kuwa mbaya  akapewa Rufaa nyingine kwenda hospital ya Taifa Muhimbili, wakiwa njiani  Mpendwa wetu Dkt Mbilu alifariki dunia.

 

 Hayati Mbilu aliyekuwa akiishi Mtaa wa Kididimu SUA ameacha Watoto 3  Mjane Bi, Regina Futakamba ambaye ni Mheshimiwa  Makimu Mwandamizi Mkoania Morogoro.

 

 HAYATI MBILU LICHA YA ELIMU YAKE HAKUWA MJIVUNI ALIJICHANGANYA KWENYE JAMII ZOTE.

Mwandishi wa habari hizi anayemjua vizuri Dkt Mbilu ana uthibitisho wa hilo kwa haya anayobainisha ambayo yameungwa mkono na Viongozi wa dini akiwemo Mchungaji Sifuni Dunia aliyehubiri kwenye lbada hiyo iliyoongozwa  na Wachungaji wawii Mchungaji Kiongozi wa Ushariki huo Dkt Rhoda Chamshama aliyehamia usharika huo takrinai Miezi 2 akitokea Usharika wa KKKT Kolla akichukua nafasi ya Mchungaji Dunia.

 

kwenye Mahubiri hayo Mchungaji Dunia alisema,

 

”lshi duniani ukiwa na huruma na shida za wengine ukijua kwamba siku moja utakufa, mimi kama mchunganga nashuhudia haya ndio maisha aliyoishi Dkt Mbilu”alisema Mchungaji huyo na kuongeza

 

“Dkt Mbilu alikuwa Mzee wa kanisa kwa zaidi ya Miaka 10 na kwamba kwenye ibada ya 3 asipoonekana utajua tu.

 

Jitafakari wewe ukifa watu watashuhudia nini kwenye maisha yako?  

 

Kwa upande wake Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kilimo Cha Sokoine[SUA] Profesa Amadus Muhairwa akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Chuo hicho Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba amesema wamepoteza mtumishi mahiri na kwamba kwenye msiba huo Uongozi wa Chuo umetoa kitu kidogo ambacho hakukitaja kwa sabubu anadai akilingani na thamani ya uhai wa mtumishi wao, 

         

Dkt Mbillu alikuwa mdau Mkubwa wa Soka Mkoania Morogoro ikumbukwe wakati timu ya Burkina Faso  ikishirki ligi daraja la kwanza ilikubwa na Ukata Mkubwa na Dkt Mbilu alijitosa  kuwasaidia.

 

Kwa wema huo kwenye uchaguzi Mkuu wa timu hiyo wanachama walimfuata na kumuomba agombee nafasi ya uwenyekiti, Dkt Mbilu alikubali ombi hilo na kuchanguliwa kwa kura nyingi,

 

Baadae Burkinafaso ‘Wana Kisiki cha Mpigo’ walishuka daraja wakati Dkt Mbilu akiwa nchini Ghana kikazi.

 

Mawenzi Market iliyokuwa ikishiriki pia daraja a kwanza walivutiwa na uongozi wa Dkt Mbilu hivyo nao walimumba kujiunga na timu yao Dkt Mbilu alikubari kujiunga na Mawenzi ambayo wakati huo kipa wao namba Moja alikuwa Yona Amosi ambaye kwa sasa ni Kipa namba Moja wa Pamba Jiji ya Mwanza na timu ya Taifa ya Tanzania.

 

Baadae Mawenzi ikauzwa kwa Mwanasiasa kutoka Mkoani Singida, nyota ya Dkt Mbilu ilizidi kung’ara wadau wa soka walimuomba kuingia kwenye uchanguzi wa chama cha Soka Wilaya ya Morogoro huko nako alichaguziwa kwa kushindo.

 

 Hata hivyo Kufuatia kutingwa na majukumu ya kikazi yaliyopelekea kusafiri mara kwa mara ndani nje ya nchi Dkt Mbilu aliamua kujitoa kwenye uongozi.

 

kufuatia mchango wake kwenye soka takribani siku mbili Mtandao huu umeshuhudia Grop la Whatssap la  chama cha soka Wilaya wakiomboleza kifo cha Dkt Mbilu huku kiongozi wa Grop hilo akitoa ratiba za mazishi mara kwa mara.

 

 Hayati Mbilu Mgosi Kutoka Tanga  ambaye pia alikuwa mdau mkubwa wa Mtandao pendwa wa Shekidele amezikwa April 1 kwenye Mji wake uliopo Kasanga nje kidogo ya Mji wa Morogoro jirani na Bwawa la Mindu.

 " Bwana ametoa na Bwana ametwaa jina lake ihimidiwe" 

             Tangulia kamanda tutaonana baadae

Monday, March 30, 2026

A-Z UJENZI NYUMBA YA MLEMAVU MATAMA SEHEMU YA MWISHO.

Matama akimshukuru Mungu huku akimuombea Dua Shekidele Kwa kumsimamia Kwenye jambo lake.
 Matama akilipia kiwanja kwa Mwenyekiti wa Mtaa kulia ni muuzaji wa kiwanja hich Mzee Omar Mbezi

Bi Maua Said mke wa Matama naye aishiriki kusomba maji na kujaza kwenye pipa tayari kuanza ujenzi wa Msingi
                       Matama akiwa mbeke ya mjengo wake
lnjinia hayati Mzee Hussein na msaidizi wake wakichra ramani ya nyuma ya Matama
Matama akishuhudia hayati Mzee Hussein akichora ramani ya nyumba yake
                                         .....Shekidele akichimba msingi
                                               ......Matama akitoa udongo
                                Mungu ni mwema.nyumba imepauliwa
   Injinia  Hayati Mzee Hussein amekamilisha ujenzi wa msingi

                      ......Matama akiwa nje ya nyumba yake
Nyumba iliyojengwa na watu wa Mungu wadau wa Mtandao Pendwa wa Shekidee yenye nyumba 3 sebure,Jiko imekamiika hii hapa Mtanda huu unawashukuru watu wote walioguswa na changamot za ndugu yetu Matama na kuamua kuta michango iliyofanikisha kukamilika kwa nyumba hii
 
                  Na Dunstan Shekidele,Morogoro
NAFUNGA stori hii ya kumbukizi ya Ujenzi wa nyumba ya Mlemavu Mohamed Matama kwa kuwashukuru wote walioisikia sauti ya Mungu na kuniunga mkono kwenye jambo hili.
 
Kipekee niwashukuru wadau wote wa Mtandao Pendwa wa Shekidele pande zote za dunia ambapo wengi wao walituma pesa kutoka nje ya nchini na ndani ya nchini wakichangia ujenzi huo.
 
Pia navishukuru vyombo vya habari vilivyoniunga mkono kwenye harambee ya ujenzi wa nyumba hiyo, vyombo hivyo ni Global Publishers, TBC Taifa na Abood Media ambayo kupitia kipindi kilichokuwa kikiongozwa na Zuberi Mkalaboko walimuita Matama studio na kufanya naye mahojiano Live. 
 
      HAYATI MZEE HUSSEIN MUNGU AKUBARIKI.
 
Baada ya kuona ninavyopambana na ujenzi huo, lnjinia Mzee Hussein ambaye kwa sasa ni marehemu alinifuata na kunieleza hivi.
 
“ Shekidele nimeona unavyompambani ule Mlemavu Munngu atakubariki nami kama fundi nitakusapoti kwenye jambo hilo nitachora ramani na kujenga msingi bure ninachokuomba ni nauli kutunulia chakula mimi na msaidizi wangu na kutafuta vijana wa kuchimba msingi”alisema hayati Mzee Hussein pichani mwenye kofia.
 
Mwandishi wa habari hizi alimshukuru Mzee huyo na kutekeleza maagizo hayo, hilo la kuchimba msingi tulikosa pesa kwa wakati huo hivyo Shekidele na Mlemavu huyo walifanya kazi hiyo huku mke wa Matama Bi Mau Said akifanya kazi ya kusombelea maji.
 
Mungu Mkubwa ndani ya Mwaka mmoja tulipata pesa ya kununua kiwanja na kukamilisha nyumbani hiyo ambapo kwa sasa Mpendwa wetu Matama anaishi na mkewe huku chumba chao kikiwa na choo ndani[Master]
 
Juzi nilifika kwenye nyumba hiyo iliyopo kata ya Kichangani jirani na Karakana kuu ya Reli nikakutana na Mzee Omari Mbezi aliyetuuzi kiwanja hicho akisema.
 
“ Shekidele ubarikiwe sana kwa sasa sisi majirani wa Matama tunafura kubwa kila siku mpira tunaangalia bure nyumbani kwake nyakati za usiku watoto wetu wanakwenda kuongalia Filamu zinazirushwa Azam Two”
 
Mtandao huu unawashukuru wote waliochangia ujenzi wa nyumba hii malipo yenu mtayakuta kesho kwa Mungu namini hakuna mtu aliyefirisika kwa kumsaidia mwenye uhitaji. 
 
Nakili kutoka kwenye sakafu ya moyo wangu kwenye ujenzi wa nyumba hii sikutoa hata senti tano vitu nilivyotoa ni Taaruma yangu ya Uandishi wa habari, Nguvu zangu, vifaa vya ujenzi kama vile mapita ya maji na mbao za Linter, Muda wa mwaka mzima wa usimamizi wa nyumba hii na mafuta ya pikipiki kuzunguza mitaani Mwaka mzima. 
 
Ninachojivuni ni kwamba nimekamilisha kazi niliyotumwa na Mungu na nimeweka alama ya kuwa Mwandishi pekee Tanzania niliyetumia kazi yangu ya Undishi wa habari kumjengea nyumba ya kisasa Mlemavu Matama pichani anayemuombe dua Mwandishi wa habari hizi

Sunday, March 29, 2026

HII KALI MLEMAVU ANGUA KILIO BAADA YA KUTAPELIA MSAADA WA PESA ALIOPEWA NA RPC.





 

                    Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

MSANII Staa wa nyimbo za lnjiri nchini  Bahati Bukuku amehubiri kupitia wimbo akisema ‘Dunia haina huruma’.

Kweli kuna baadhi ya watu hapa duniani hawana huruma, wakati Mwandishi wa habari hizi akipambana kusaka pesa za kumjengea nyumba Mohamed Matama ambaye ni Mlemavu wa Miguu.

Matapeli wametumia fursa hiyo kumtapete mlemavu huyo  elfu 50 alizopewa msaada na aliyekuwa kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro’RPC’ SACP Urlch Matei.

           PICHA HILO LILIKUWA HIVI.

Mbali na kuendesha harambee  kwenye Mtandao Pendwa wa Shekidele,Mwanahabari huyo pia alizungunza na Mlemavu huyo kwa viongozi na na Mtajiri wa Mkoa wa Morogoro kuomba msaada.

 

 Dunstana Shekidele na Matama walitinga Ofisi wa RPC Matei Ghorofa ya kwanza kwa kuwa Ghorofa hilo halina lifti Mlemavu huyo kwa Ujasiri alitambaa na kupanda ngazi mpaka juu ya ghorofa hilo.

Mungu ambariki sana RPC Matei tulipofika tu ofisini kabla ya kumueleza shinda yetu RPC huyo alisema

” Du huyu jamaa kapandaje ngazi shekidele ungenipigia simu nije huko chini tuzungumze mbona kuna ofisi nyingi kuliko kumpa adhabu ndugu yetu huyo ya kupanda huku”

Mwanahabri huyo alimuomba msamaha ‘Big Bos’ huyo wa Polisi Mkoa Morogoro na Moja kwa Moja  alimueleza shida za Mlemavu huyo ambapo RPC Matei aliguswa na kumkabidhi Msaada wa elfu 50 huku akisema

“ Shekidele ubarikiwe sana kwa kazi hii unayoifanya kwa sasa ninakiasi hichi kidogo naomba mkipokee mwisho wa mwenzi nitachangia kiasi kingine “alisema RPC huyo.

Kabla hayatimiza ahadi yake hiyo RPC Matei halihamishiwa Mkoa wa Mbeya, Mtandao huu unazidi kumuombe baraka nyingi  na wote waliochangia ujenzi wa nyumba hiyo.                                   UTAPELI SASA.

Matama ni muunini wa dini ya kiislamu aliyejaliwa kuswali swala 5 hivyo wakati tunatoka Polisi muda wa kwenda Msikiti ulifika.

 

Baada ya kutoka Msikiti njini alikutana na Matapeli wanaofuatilia habari za harambee ya ujenzi wa nyumba yake kwenye Mtandao wa Shekidele, Magazeti na Redio.

Matapeli hao wakamsimamisha na kumueleza  hivi.

“Tunaona Shekidele anakupambani sana bosi wetu ameona habari zako hivyo ametutuma tukutafute  akuchangie mabati na Cement sasa kama una lakini moja tupe tukodi gari sasa hivi twende na wewe ukavibebe vitu vyako”

Matama aliwaambia  kwa muda huo alikuwa na elfu 50 tu Matapeli hao wakajifanya kumpigia simu bosi wao, baada ya kukata simu hiyo ya uongo wakamueleza Matama kwamba bosi wao ametuma elfu 50 hivyo awape hiyo 50 waende kwa wakala wakatoe wakodi gari wampitie waende kuchukua vifaa hivyo.

Matama  amezama msukoni na kuwakabidhi pesa, wajomba wamelala mbele wakimuacha matama akiendelea kusubiri kwa zaidi ya masaa 2 bila mafaniko.

Ndipo alipoamua kumpigia simu Shekidele huku akiangua kilio Mwanahabri huyo alipofika  awari alibeba jukumu la kumbembeleza na kumueleza maeneo ya faraja  aliokaa sawa nikamruhusu erejee nyumbani tuonane kesho.

Saturday, March 28, 2026

SEHEMU YA PILI MLEMAVU MATAMA KUJENGEWA NYUMBA NA MUNGU.









               Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

SEHEMU ya kwanza ya habari hii ya kumbukizi ya Mlemavu Mohamed Mtama kujengewa nyumba na Mungu imeruka juzi kwenye Mtandao Pendwa wa Shekidele,Leo tunaendelea na sehemu ya pili.

Wakati mazungumzo  na Mlemavu huyo ya kuibiwa baiskeli  na Vibaka [Mateja] wakaenda  kuuza vyuma chakavu yakiendelea aliomba kwenda chooni kujisaidia.

Choo kilikuwa umbali wa takribani  mita 20 kutoka kilipo chumba chake na kwamba kipindi hicho kilikuwani kipindi cha Mvua za Masika.

 

Mwandishi alishangaa kuona Matama anasindikizwa na mkewe alipouliza, Matama alisema Choo chao kina changamoto nyingi  hivyo kwa hali yake lazima apate msaada wa mkewe.

Mwanahabari huyo alitoka nje na kushuhudia Matama akitambaa na mikono kabla ya kufika chooni alizama kwenye dimbwi la maji machafu.

Kwenye kimfereji hicho wapangaji wenzie waliweka kidaraja cha mbao kuvuka kuelekea Maliwato[Chooni].

Inauma sana Aisee,Choo hicho nimeezekwa na mabati chakavu hivyo kufuatia mvua kubwa ndani kimejaa tope zito lillochanganyika na kinyesi.

Bi Mau Said Mwenye mapenzi ya kweli kwa  Mume’we  alimfungulia Mlango akatambaa na mikonono akaingia kwenye choo hicho kilichojaa tope lililochanganyika na kinyesi.

Ama kwa hakika hali hiyo iliniumiza  Moyo wa Mwandishi wa habari hizi na kwamba ndani ya muda mfupi alisikia  sauti ya Mungu  ikimuagiza kumnunulia baiskeli na kumjengea nyumba kupitia kazi yake ya Uandishi wa habari.

Mwanahabari huyo alitii sauti hiyo na moja kwa moja akamjulisha  Matama kuhusiana na agizo hilo nililopewa na Mungu.

Kama tunavyojua kila kitu kinakwenda na ushahidi hivyo Mwandishi huyo alimuomba Matama ampige picha  aklwa kwenye mazingira hayo magumu na hatarishi kiafya.

Matama alikubali ombi hilo hivyo Mwanahabari huyo aliacha kazi zote na kufanya kazi hiyo aliyotumwa na Mungu ambapo alianzisha harambee ya kumnunua baiskeri na kumjengea nyumba mpendwa wetu huyo harambee hiyo niliifanya kwenye Mtandao pendwa wa Shekidele na kwenye vyomba mbali mbali vya habari.

Wadau wa Mtandao huu wanakumbuka vizuri harambee hiyo,ambapo wengi wao walichangia ujenzi huo huku  wengine walitupatia Cement na wengine Mabati ambapo vitu hivyo tulivisafirisha kwa usafifi wa baiskeli ya Matama na Pikipiki ya Mwandishi wa habari hizi  kwenda kuvihifadhi kwenye chumba cha Matama.

 Mungu awabariki wote mliochangia  mmeweka alama ambayo mtakufa nayo hata kama ulinunua tofari moja.

Mungu Mkubwa ndani ya Miezi miwili Mwanahabari huyo alipata Pesa  za kununua baiskeri na kiwanja.

Wengi walichangia baada ya kuguswa walipoziona  picha za Matama zilisokwenda sambamba na habari ya kusigitisha.

 Mwenyekiti wa Mtaa wa saadan hayati Hassan Msungi pichani mwenye suti  alichangia Loti moja la Mchanga na kuruhusu tofari 300 za msingi zifyatuliwe nyumbani kwake.

 Baadae zitaruka picha za nyumba hiyo toka msingi mpaka kukamilika hivyo endelea kuwa jirani na Mtandao huu muda wote.

 

Thursday, March 26, 2026

WEMA ALIOFANYA HAYATI MSUNGI KWA MLEMAVU MATAMA HUU HAPA.


Matama na mkewe wakizungumza na Mwandishi wa habari. 

Matama akitabasau na kuendelea na baishara yake baada ya kupata baiskeli mpya.
Matama akimbaidhi pesa hizo Mwenyekiti wa Mtaa kulia ni Mzee Omari Mbezi aliyetuzia kiwanja hicho.
Shekidele na Matama wakiwa kwenye Pikipiki wakienda kununua Kiwanja.
       Shekidele akimkabidhi Matama Milioni moja na Nusu
            Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

KABLA ya kutaja wema aliofanya aliyekuwa Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Saadan Hayati Hassan Msungi kwa Ndugu yetu Mohamed Matama ambaye ni Mlemavu wa Miguu, nieleze kwa ufupi sababu za Mwenyekiti huyo kuguswa na kutoa msaada huo.

Matama anayeishi Mtaa wa  River Side Kata ya Mwembesongo jirani kabisa na Mtaa wa Saadan anaendesha Maisha yake kwa biashara ya kuuza Maji Mitaani na kwenye viwanja wa Mpira akitumia usafiri wa baiskeli.

 Takribani Miezi miwili Mwandishi wa habari hizi hajamuona Matama Mtaani wala kwenye viwanja wa Mpira jambo ambalo si kawaida yake.

  Hali hiyo ilimsukuma Mwandishi huyo  kwenda nyumbani kwake kumjulia hali na kujua kipi kinamsibu.

 Alipofika alimkuata Matama amejikunyata na Mkewe Bi Maua Said na alipoulizwa kulikoni haonekani alijibu.

“ Shekidele kwanza ubarikiwe sana kwa moyo wako wa huruma,kilichonifanya sionekani mtaani kwa muda mrefu ni Vibaka[ Mateja] wameiba miguu yangu kama unavyojua baiskeri yangu haingia ndani mlango ni mdogo  miaka yote inalala hapo Nje.

Sasa Mwezi uliopita Mateja hao wamekuja na Misumeno wameikata kata  na kwenda kuuza  vyuma chakavu kulipokucha mimi na mke wangu  tumeshuhudia mabaki ya vyuma ilituumiza sana  kwa sasa mimi na mpendwa mke wangu hatuna uwezo wa kupata laki moja na Nusu  kununua baiskeri nyingine ndio maana umeona sielewi nipo tu nyumbani” alisema Matama kwa sauti ya kinyonge.

Alipoulizwa kwa sasa anapataje pesa ya matumizi?

Alijibu.” Kukicha mke wangu anakwenda kufanya kazi ya kufua kwenye majumba ya watu akilipwa elfu 4 au 5 tunanunua chakua maisha yanaenda”

Kuptia Mwandishi wa habari hivi Mungu amefanya jambo Matama amepata baiskeri mpya kama hiyo haitoshi amenunua kiwanja na kujenga nyumba kubwa ya kisasa, nini kimetokea endelea kuwa jirani na Mtandao huu muda wote.

                         


 

 

 

 

 

 

Wednesday, March 25, 2026

UCHAGUZI SERIKALI ZA MTAA FAMILIA YA MSUNGI UPINZANI WAO NI KAMA ULE WA SIMBA NA YANGA.



Kassim kushoto akipinga kauli ya Ally [kati mwenye koti] kulia ni Wazee wakifuatilia mahojiano haya.

 
                    Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

 MWENDELEZO wa Stori ya Familia ya Msungi na hii imetokana na kifo cha Mpendwa wetu Mwenyekiti wa zamani wa Mtaa wa Saadan Kata ya Mwembesongo, hayati Hassan Msungi aliyefariki wiki iliyopita kwenye ajari iliyotokea Nane Nane eneo la Jordan mkoani hapa.

Jana Mtandao huu ulishia kwenye kipengele cha Mwenyekiti wa sasa wa Mtaa huo Ally Msungi ambaye alinyakua kiti hicho kwa leseni ya CCM baada ya kumbwaga kaka yake,Hayati Hassan Msungi aliyeongoza mtaa huo kwa vipindi viwili kwa leseni ya Chama cha Wananchi CUF toka Mwaka 2009 mpaka 20014.

 

Kwenye uchaguzi  wa Mwaka 20019 CCM Kata ya Mwembesongo waliamua kumteua Ally Msungi kupambana na kaka yake.

Wiki iliyopita baada ya mazishi ya Hassan Msungi Mwandishi wa habari hivi alimtaka Ally  kueleza namna alivyomshinda kaka yake aliyekuwa kipenzi cha wana Mtaa huo.

                 MSIKIE ANACHOSEMA.

“ Kila kitu ni kwa zamu kaka  baada ya kuongoza  wa vipindi viwili, uchaguzi wa 2019 niliamua kuingiza timu  kupambana naye nikipeperusha bendera ya chama dume  CCM”Alisema Msungi na kuongeza.

“Mwisho wa siku nilimshinda  mpaka sasa naendelea kuongoza mtaa ambapo uchaguzi wa mwaka juzi 2024 nilishinda tena kwa kishindo”alimalizia kusema.

Hata hivyo Kauli hiyo ilipingwa vikali na Kassim ambaye ni mdogo wao wa mwisho.

“ Sio kweli Shekidele kumbuka uchaguzi wa 2019 wagombea wengi akiwemo kaka Hassan walieguliwa ndipo huyu kaka Ally alipopata nafasi ya kupita bila kupingwa wangeingia wote kwenye sanduku la kura kaka Ally ungepigwa asubuhi na mapema”alisema

 

Mtandao huu ulipomuliza Ally ni kweli alivyosema Mdogo wake  alijibu.

“ Ni kweli lakini kabla ya kaka kuegeliwa kilipigwa kwenye kampeni za awari za nyumba kwa nyumba labla hayati kaka yangu kueguliwa na tume ya uchaguzi”Alisema Ally huku akiangua kicheko.

Mwandishi. Hebu tueleze siku mlivyokabidhiana ofisi ilikuwa je?

 

Ally. Haa Shekidele siunajua kaka yangu dini ilimkaa sana kiukweli alinikabidhi ofisi vizuri na nikili kwenye uongozi wangu pale nilipokwama nilimfuata na alinipaushirikiano mzuri sana.

 

Mtandao huu ni shuhuda Ally[Pichani aliyekaa] amefuata nyayo za kaka yake ambapo kwa sasa wananchi wa Mtaa wa Saadani huwaambi kitu juu ya utendaji mzuri wa  Mwenyekiti wao huyo.

Baadae tutamalizi stori hii kwa kueleza wema aliofanya hayati Msungi[Pichani aliyesimama] wakati Mwandishi wa habari hizi alipoendesha harambee ya kumjengea nyumba Mlemavu wa Miguu Mohamed Matama.

                         


MAJAJI 2 WAHUDHURIA IBADA YA KUMUOMBEA KIGOGO WA SUA MAREHEMU DKT MBILU.

         Mchungaji Dkt Rhoda Chamshama akiongoza ibada hiyo Katibu Mkuu wa  KKKT Usharika wa Mji Mpya Mshana akimuaga Mzee wake wa kanisa S...