Katibu Mkuu wa KKKT Usharika wa Mji Mpya Mshana akimuaga Mzee wake wa kanisa
Shabiki wa Simba akimuada Mdau mkubwa wa Soka hayati Mbili
.... Shabiki wa Yanga naye akitoa heshima zake za Mwisho
Kundi la baraza a Wazee usharika wa Mji Mpya kwa pamoja wakipita mbele ya jeneza wakimuaga mwenzao aliye twaliwa na bwana baada ya kumaliza kazi....Inauma sana aishee hiki ni kipengele kigumu, Mhe Regina Futakamba akiwaogoza wanaye kupita mbele ya jeneza kumuaga mpendwa baba yao
...Mtoto wa marehemu aliyeshika msalaba akiwaongoza waombezaji kutoka ndani ya kanisa baada ya ibada kutamatika juzi
Wazee wa kanisa wakiingiza mwii wa mwenzao kwenye gari tayari kwa safari ya kwenda kumpunzisha kwenye nyumba yake ya milele
Watoto wakiwa na shada a maua
.... Nje ya kanisa ni vilio tu
....Mtoto wa mwisho wa marehemu toka tukiwa kwenye mkesha nyumbani kwa SUA usiku kucha alimlilia mpendwa baba yake, pichani akibembelezwa na dada yake
Hayati Dkt Mbilu enzi za uhai wake
Mke wa Mrehemu Mhe Futakamba aitka kanisani
Matalumbenda kutoka KKKT Usharika wa Kolla wakiimba baada ya kutoka kanisani
Na Dunstan Shekidele.
WAHESHIMIWA Majaji wawii wa Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro na Mahakama ya Rufaa wameshiriki lbada ya kumuombea na kumuaga Kigogo wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine’SUA’ Dkt Zenu John Mbilu[53]iliyofanyika juzi kanisa la KKKT Usharika wa Mji Mpya mkoani hapa.
Hayati Mbilu aliyekuwa Mteknojia Mkuu wa Mahabara [SUA], Kiongozi wa kanisa KKKT Usharika wa Mji Mpya na Mdau Mkubwa wa Soka Mkoani Morogoro alifariki March 30 akiwa njiani kuelekea Muhimbili baada ya kupewa Rufaa kutoka Hospital ya Rufaa Morogoro,
Akizungumza kwenye Ibada hiyo kaka wa Marehemu alisema.
Mdogo wake alianza kuugua March 27 wakampeleka hospital ya SUA na kwamba March 29 hali yake iliendelea kuwa mbaya hivyo akapewa Rufaa ya kwenda hospital ya Mkoa.
Amesema huko pia hali iliendelea kuwa mbaya akapewa Rufaa nyingine kwenda hospital ya Taifa Muhimbili, wakiwa njiani Mpendwa wetu Dkt Mbilu alifariki dunia.
Hayati Mbilu aliyekuwa akiishi Mtaa wa Kididimu SUA ameacha Watoto 3 Mjane Bi, Regina Futakamba ambaye ni Mheshimiwa Makimu Mwandamizi Mkoania Morogoro.
HAYATI MBILU LICHA YA ELIMU YAKE HAKUWA MJIVUNI ALIJICHANGANYA KWENYE JAMII ZOTE.
Mwandishi wa habari hizi anayemjua vizuri Dkt Mbilu ana uthibitisho wa hilo kwa haya anayobainisha ambayo yameungwa mkono na Viongozi wa dini akiwemo Mchungaji Sifuni Dunia aliyehubiri kwenye lbada hiyo iliyoongozwa na Wachungaji wawii Mchungaji Kiongozi wa Ushariki huo Dkt Rhoda Chamshama aliyehamia usharika huo takrinai Miezi 2 akitokea Usharika wa KKKT Kolla akichukua nafasi ya Mchungaji Dunia.
kwenye Mahubiri hayo Mchungaji Dunia alisema,
”lshi duniani ukiwa na huruma na shida za wengine ukijua kwamba siku moja utakufa, mimi kama mchunganga nashuhudia haya ndio maisha aliyoishi Dkt Mbilu”alisema Mchungaji huyo na kuongeza
“Dkt Mbilu alikuwa Mzee wa kanisa kwa zaidi ya Miaka 10 na kwamba kwenye ibada ya 3 asipoonekana utajua tu.
Jitafakari wewe ukifa watu watashuhudia nini kwenye maisha yako?
Kwa upande wake Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kilimo Cha Sokoine[SUA] Profesa Amadus Muhairwa akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Chuo hicho Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba amesema wamepoteza mtumishi mahiri na kwamba kwenye msiba huo Uongozi wa Chuo umetoa kitu kidogo ambacho hakukitaja kwa sabubu anadai akilingani na thamani ya uhai wa mtumishi wao,
Dkt Mbillu alikuwa mdau Mkubwa wa Soka Mkoania Morogoro ikumbukwe wakati timu ya Burkina Faso ikishirki ligi daraja la kwanza ilikubwa na Ukata Mkubwa na Dkt Mbilu alijitosa kuwasaidia.
Kwa wema huo kwenye uchaguzi Mkuu wa timu hiyo wanachama walimfuata na kumuomba agombee nafasi ya uwenyekiti, Dkt Mbilu alikubali ombi hilo na kuchanguliwa kwa kura nyingi,
Baadae Burkinafaso ‘Wana Kisiki cha Mpigo’ walishuka daraja wakati Dkt Mbilu akiwa nchini Ghana kikazi.
Mawenzi Market iliyokuwa ikishiriki pia daraja a kwanza walivutiwa na uongozi wa Dkt Mbilu hivyo nao walimumba kujiunga na timu yao Dkt Mbilu alikubari kujiunga na Mawenzi ambayo wakati huo kipa wao namba Moja alikuwa Yona Amosi ambaye kwa sasa ni Kipa namba Moja wa Pamba Jiji ya Mwanza na timu ya Taifa ya Tanzania.
Baadae Mawenzi ikauzwa kwa Mwanasiasa kutoka Mkoani Singida, nyota ya Dkt Mbilu ilizidi kung’ara wadau wa soka walimuomba kuingia kwenye uchanguzi wa chama cha Soka Wilaya ya Morogoro huko nako alichaguziwa kwa kushindo.
Hata hivyo Kufuatia kutingwa na majukumu ya kikazi yaliyopelekea kusafiri mara kwa mara ndani nje ya nchi Dkt Mbilu aliamua kujitoa kwenye uongozi.
kufuatia mchango wake kwenye soka takribani siku mbili Mtandao huu umeshuhudia Grop la Whatssap la chama cha soka Wilaya wakiomboleza kifo cha Dkt Mbilu huku kiongozi wa Grop hilo akitoa ratiba za mazishi mara kwa mara.
Hayati Mbilu Mgosi Kutoka Tanga ambaye pia alikuwa mdau mkubwa wa Mtandao pendwa wa Shekidele amezikwa April 1 kwenye Mji wake uliopo Kasanga nje kidogo ya Mji wa Morogoro jirani na Bwawa la Mindu.
" Bwana ametoa na Bwana ametwaa jina lake ihimidiwe"
Tangulia kamanda tutaonana baadae


































