.........Akikabidhi zawadi ya Neti kwa watoto hao
Mwana Birthday huyo akitoka nyumbani na usafirir wake wa baiskeli akielekea kwa waendwa wake kukata hao keki kwenye kumbukizi ya siku yake ya kuzaliwa
Na Dunstan Shekidele.Morogoro.
WATOTO Yatima na wale wenye ulemavu wa utindio wa Ubongo wanalelewa katika kituo Cha Mehayo kilichopo Mazimbu Manispaa ya Morogoro jana wamefurahia zawa za Siku kuu ya Chris Masi walizokabidhiwa na Msamalia Mwema.
Msamalia Mwema huyo Dunstan Shekidele ambaye jana Disemba 25 ilikuwa ni kumbukizi yake ya mfanano wa siku yake ya kuzaliwa 'Happy Birthday's aliamua kwenda kusheherekea siku yake hivyo na Watoto hao wenye uhitaji wa faraja na vitu mbali mbali.
Hata hivyo Mwana Birthday huyo alipofika kituo hapo alikuwakuta Watoto wachacha tofauti na miaka yote anaposheherekea Birthday yake na Watoto hao.
Hivyo kabla ya kukabidhi zawadi hizo Shekidele alimuliza Matron wa Watoto hao Bi Esther Daniel kwamba Watoto wengine wako wapi?
Alisema wamechukuliwa na mmoja ya chuo kikuu Cha Mkoani Morogoro mtandaoo unahifadhi jina la chuo hicho kwa sababu huenda wenyewe hawakupenda jambo hilo litangazwe.
"Chuo kikuu (anakitaja jina) asubuhi wametuma basi limewachukua Watoto zaidi ya 20 wamekwenda kula.nao siku kuu kwenye chuo chao.wamebaki hawa wachache na Mungu alivyo MKUBWA na wewe kama kawaida yako kila Mwaka siku kama ya Leo unakuja hapa kituoni kushiriki.Birthday yako na Watoto hawa huu.ni upendo Mkubwa sana'alisema Matron huyo.
Baada ya zoezi hilo kukamilika Shekidele alikwenda kwenye Bonet la Baiskeli yake akitoa mizigo na kuwakabidhi Watoto hao.
Zawadi hizo ni Nguo.Viatu.Juice na vyandarua'Net'
KWA NINI NET?
Kwenye Birthday ya Mwaka jana Matron Esther akitoa neno la shukrani kwa Shekidele alisema maneno yaliyomchoma.mwana Birthday huyo na maneno hayo.ni haya.
"Tunakushukuru sana kaka Shekidele kwa kuwakumbuka hawa Watoto na kuwaletea zawadi hizi ungeweza kufanya sherehe yako ya Birthday kwenye baa yoyote lakini umeona uje kusheherekea na hawa Watoto wanaohitaji faraja kama hii barikiwa









No comments:
Post a Comment