Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Monday, November 24, 2025

FOUNTAIN GATE YATWAA UBINGWA WA CRDB FEDERATION CUP.

                                Papatu papatu ya fainali hiyo







wachezaji,Viongozi na mashabiki wa Fountain Gate wakiwa katikati ya uwanja wakimshukuru Mungu kwa kufanikiwa kutwaa ubingwa wa CRDB Federatin Cup
                                     Kipa wa mabingwa hao
Mgeni rasmi wa fainali hiyo Selestini Mbilinyi akimkabidhi zawadi ya jezi Nahodha wa Fountain Gate Denis Mwantenga.

                       Na Dunstan Shekidele, Morogoro.

TIMU ya Fountain Gate wiki iliyopita imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Michuano ya kombe la Shirikisho’Wilaya ya Morogoro Maarufu CRDB Federation Cup.

 

Vijana hao wa Fountain Gate kutoka kituo cha kukuza na kurea Vipaji chenye maskani yake Kihonda Maghorofani Manispaa ya Morogoro kinachomilikiwa na Mfanyabiashara Maarufu nchini Japhat Makao mwenyeji wa Morogoro mwenye maskani yake Jijini Dodoma,imenyakua ubingwa huo baada ya kuinyuka Moro Rangers kutoka Kilakala kwa pelnati 5-4 miamba hiyo imefikia hatua hiyo ya pelnati baada ya kutoka sare ya bao 1-1 kwenye mchezo huo wa fainali uliopigwa uwanja wa Saba saba Manispaa ya Morogoro Alhamisi iliyopita.

 

Baada ya kunyakua ubingwa huo na kukabidhiwa zawadi ya jezi na mwenyekiti wa chama cha Soka Wilaya ya Morogoro Selestin Mbilinyi, Vijana hao wa Fountain Gate wamesafiri kuelekea Wilaya ya Mvomero ambapo Leo Jioni watacheza mchezo wa fainali na Volucano Fc ambao ni mabingwa wa kombe hilo Wilaya ya Mvomero.

 

Mshindi wa mchezo huo atauwakilisha Mkoa wa Morogoro kwenye michuano hiyo inayoshika nafasi ya pili kwa ukubwa nchini Tanzania.

 

lfahamike Japhat Makao anamiliki shule kadhaa mkoani Morogoro zinazojulikana kwa jina la Fountain Gate School.

              


 

 .

 

Thursday, November 20, 2025

CRDB FEDERATION CUP, WILAYA YA MOROGORO IMEFIKA PATAMU.

                                                 Kikosi cha Chamwino Rangers
                               Kikosi cha Zuia Fc
Kocha Mkuu wa Chamwino Juma Mgonja akiwapa maelekezo vijana wake kabla ya gemu kuanza




Mshambuliaji wa Zuia akiokota mpira wavuni baada ya kufunga bao la Kwanza
..... Baada ya kufunga alikwenda kwenye Bench kushangalia na wenzake
             Mshambuliaji wa Zuia akifunga bao a kwanza


                Kipa wa Chamwino akipangua mpiia wa Kona.



 

   

            Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

 MICHUANO namba mbili kwa ukubwa Tanzania,Ligi ya Shirikisho’FA’ Maarufu ‘CRDB FEDERATIN CUP’inayoanzia chini kabisa hatua ya Wilaya,imefika patamu Wilaya ya Morogoro.

Timu mbili za Fountain Gate yenye maskani yake kata ya Kihonda Maghorofani na Moro Ranger yenye Maskani yake Kata ya Kilakala, zimefanikiwa kutinga hatua ya fainaii itakayopigwa Leo Alhamisi katika uwanja wa Saba Saba Manispaa ya Morogoro.

Bigwa wa Michuano ataiwakilisha wilaya ya Morogor kwenye hatua ya Mwisho ya kucheza na mabingwa wa wilaya nyingine za kumsaka Bingwa atakayeuwakilisha Mkoa wa Morogoro kucheza hatua ya Mtoano na mabingwa wa mikoa mengine.

Mtandao huu utakuwa uwanjani hapo kukusanya matukio yote hivyo endelea kuwa jirani na Mtandao huu muda wote.

 

Pichani ni matukio mbali mbali ya mchezo wa hatua ya makundi ya Ligi hiyo kati ya Chamwino Ranger[Jezi nyeusi] kutoka Kata ya Chamwino dhidi ya Zuia Fc Kutoka kata ya Lukobe.

 

Katika mchezo huo Zuia alisonga mbele baada ya kuinyuka Chamwino bao 2-0.

Thursday, November 13, 2025

MWAKA MPYA MAMBO MAPYA MOSHI MWEUPE UNAANZA KUONEKANA UJEZI WA DARAJA LA RELWE.




 

              Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

KAMA nilivyoahidi juzi kwamba panapo majaliwa ya Mwenyezi Mungu jumatatu ya wiki hii ningetembelea tena kwenye ujenzi wa daraja la Relwe lililopo mto Morogoro Mtaa wa Makaburi ‘A’ Kata ya Mji Mpya Mkoani hapa,kukagua maendeleo ya ujenzi wa daraja hilo ambalo ni maarufu kwa jina la daraja la Ng’ombe.

 

Mwenyezi Mungu ametii maombi yetu amempa afya njema na kibari Mwandishi wa habari hizi cha kutimiza ahadi hiyo niliyoitoa mwishoni mwa wiki iliyopita kupitia mtandao huu pendwa wa Shekidele.

 

Mwandishi huyo alipofika ‘Site’ alishuhudia Mkandarasi huyo Mzawa anayefanya kazi hiyo kwa kasi ya ajabu ameshamwaga zege eneo la juu ya daraja.

 

Mpiga picha wa Mtandao huu alipanda juu ya daraja hilo na kushuhudia mafundi wakiwa katika hatu za mwisho za kufunga mabosi ya nguzo za pembezi tayari kwa kumwaga zege ambapo hiyo ndio hatua ya mwisho ya ujenzi wa daraja hilo.

 

Kama kawaida daraja hilo litakapo kamailika Mtandao huu utarusha hewani hivyo endelea kuwa jirani na mtandao huu muda wote

    

Monday, November 10, 2025

DARAJA LA RELWE MWENDO MDUNDO.



 


        Na Dustan Shekidele Morogoro.

 Awari ya wote natangulisha samahani kwa kutokuwa hewani takribani wiki Moja hii ni kwa sababu zilizo nje ya uwezo wangu.

 

Baada ya hali kuwa swali Mtandao huu umerejea hewani kuendelea kurusha habari Moto moto za chini ya kapeti, hivyo nakusihi endelea kuwa jirani na Mtandao pendwa wa Shekidele Muda wote ambapo kwa leo tunaanza na habari ya ujenzi wa daraja la Mji Mpya Morogoro.

 

UJENZI wa daraja la Relwe Maarufu daraja la Ng’ombe lililopo Mto Morogoro Mtaa wa Makaburi ‘A’ Kata ya Mji Mpya Mkoani hapa  lipo hatua za mwisho  kukamilika.

 

Katikati ya wiki iliyopita Mtandao huu ulitembelea daraja hilo na kushuhudia mafundi wakiendelea kusuka Nondo ‘Silabu’ ya juu kuelekea hatua ya mwisho ya umwagaji zege eneo la juu la daraja hilo ambalo ni kiungo muhimu kwa kata za Mji Mpya, Kichangani.na Kilakala.

 

Panapo majaliwa ya Mwenyezi Mungu kesho Mtandao huu utakatiza tena kukagua maendeleo ya daraja hilo hivyo nakusihi endelea kuwa jirani na Mtandao huu muda wote.

 

 

VITUKO VYA MWEZI JANUARI

  Mwezi uliopita tumeshehelekea Siku Kuu mbili X Mas na Mwaka Mpya.   Mwezi huu dume January tunashehelekea kulipa Ada za Shule na kod...