Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Sunday, August 31, 2025

UJUMBE WA NENO LA MUNGU JUMAPILI YA LEO AGOSTI 31 UNAHUSU CHAKULA NA KINYWAJI.

Pichani mtumishi wa Munngu Dustan Shekidele akiwa na wanae Tumaini[kushoto] na Neema  kwa pamoja wanamshukuru Mungu  kwa kuwapa chakula na afya nyema inayowapa fursa ya kula na kunywa chochote.

 

   

          Na Dustan Shekidele Morogoro.

NAWASALIMU kwa jina kuu la Yesu Kristo,ama baada ya salamu tuingie kwenye somo letu la Leo ambalo linahusu Chakula na kinywaji.

 

Hakuna asiyefahamu kwamba Chakula na kinywaji ni uhai wa kiumbe chochote kilichopo hapa Duniani kisipokula au kunywa lazima kifariki dunia.

 

Naamini Muda huu ninapoandika ujumbe huu kuna watu waina mbili , wenye njaa hawana chakula kwa sababu mbali mbali ikiwemo ufukura  huku kuna baadhi  ya watu wenye uwezo wanakula chakula kingi mpaka wana saza na kukitupa jalala ili hari kuna jirani yake amelala  njaa kwa kukosa chakua.

 

 Hii ya kutupa chakula ni chukizo kubwa mbele ya  Mungu aliyekujalia kupata hicho chakula nawakumbusha na kuikumbusha pia nafsi yangu kwamba tusiwe wabinafsi wa kujilimbikizia mali sisi na familia zetu. Ifahamike kuwa tajiri au kuwa na mali nyingi sio dhambi. Ila dhambi ni namna ya kutumia huo utajiri wako.

 

Kundi la pili kuna baadhi ya watu wengi wao wakiwa ni matajiri wanachakula kingi lakini wanashindwa kula  kwa sababu mbali mbali ikiwemo magonjwa.

Kwenye jamii yetu utasikia mtu anasema kutokana na magonjwa aliyonayo anayoishi ili aendelee kuishi Madaktari wamemzuia kula Nyama, Wali wenye mafuta,  chai yenye sukari chakula chernye chumvi, asinywe Soda na Juice nakadharika na kadharika.

 

Kwa wewe ambaye siku zote unachakula ndani na huna ugonjwa wowote unaosababisha kuchagua chakula  Mwambie Mungu asante huku ukitenga muda wako  kwenda  nyumba ya lbada kumuabudu kwa wema huo anaoendelea kukutendea.

Utashangaa kuna mtu kapewa vyote Chakula na afya nyema lakini jumapili kama leo kanisani kwake kuna meza ya  Bwana sakrameti Takatifu [kula na kunywa damu ya Yesu] Kwa sababu anazozijua yeye mtu huyo anakimbia kula na kunywa Sakramenti hiyo.

 

         MADHARA YA CHAKULA NA KINYWAJ.

Sio kila chakula unacho ni sahihi kwako vingine ni mitego kwako, mfano Mwanafunzi ‘Dent’ anakaribishwa chips kuku na mwanaume, Mwisho wa siku ofa hiyo itamgharimu pakubwa anaweza  kupata Mimba au gonjwa hatari la UKIMWI na kukatisha ndoto zake za kimaisha kwa tamaa ya Chips Yai ambayo dharama yake haizidi elfu 5.

 

Mke wa mtu anapewa Ofa ya Bia na Njama Choma anasaliti ndoa yake anaibanyua Amri ya 6[Usizini]  mwisho ya siku anazoa Gonjwa la Ukimwi huko nje anampelekea Mumewe ndani badae wote wawili wanakufa na kuwaacha watoto zao yatima kwa tamaa ya Pombe na Nyama Choma ambayo gharama yake haizidi elfu 20.

        KIIMANI KWA WAMCHAO MUNGU.

Sio kila kalamu unayoalikwa  inautukufu wa Mungu, nyingine ni Madhebau za kipepo[Kishetani] Mfano unaalikwa kwenye kalamu kumbe shughuri hiyo ni ya kumsimika Mganga wa kienyeji.

 

Au unaalikwa kwenye Mkutano kumbe mkutano huo kiongozi anayetaka uongozi anaandaa chakula kwa lengo la kuwakusanya wajumbe  wamchague kwenye nafasi anayogombea.

Mwenye masikio na asikie asiye na masikio…..]

Kwa leo naishi hapa tukutane kwenye mada nyingine Jumapili ijayo panapo majaliwa ya Mwennyezi Mungu.

 


 

Tuesday, August 26, 2025

BWANA HARUSI AMKOSHA ASKOFU BAADA YA KUITAJA YANGA KANISANI.

Baba Askfu Msimbe akiingia kanisan huku akiwasimia waumini wake

             Bwana harusi Saema akizungumza na Mtanda huu

                  ....Mzee Massawe na kadi zake za Yanga

 


   Na Dustan Shekidele. Morogoro.

HIVI wewe huogopi? Yanga inatajwa mpaka kanisani.

Bwaha harusi  ameitaja Yanga akiwa juu ya Madhebau ya kanisa Katoliki Parokia ya Bikira Mama wa Kanisa Kigurunyembe Mkoani hapa.

 Mwanandoa huyo Seraphin Josephat Salema[Pichani mwenye suti kali]amewataja mabingwa hao wa kihistoria [Yanga] wakati akitoa neno la shukrani kwa kanisa na  Askofu Razarus Vitalis Msimbe.

Kwa nini Bwaha harusi  ameitaja yanga? Ijumaa iliyopita kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro kwa ufadhiri wa Askofu Msimbe walifungisha ndoa 101  kwa wakati mmoja maarufu[Ndoa za mafungu].

 

Kwa mujibu wa taarifa ambazo zimethibitishwa na Askofu Msimbe zinadai Big Boss huyo wa kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro ametoa Milioa 10 kutoka mfukoni kwake kugharamia ndoa hizo.

 

Kwa Upendo huo  mmoja wa maharusi Selema aliamua kupanda madhebahuni na kumshukuru Askofu huyo kwa jambo hilo kubwa alilowafanyia.

 

“Kwa niaba ya maharusi wote tunakushukuru sana baba Askofu kwa jambo hili kubwa ulillotufanyia kwenye historia  ya maisha yetu mwenyezi Mungu akubariki sana, umeupiga mwingi kama Yanga.

 

Hivyo nawaomba maharusi wote na wasimamizi wetu tupite mbele tumpemkono wa shukrani Askofu wetu”alisema Bwanahauri huyo na kupokea zawadi ya makofi na vigeregere.

 

Baadae Mtandao huu ulimshuhudia Askofu Msimbe akitabasamu muda wote huku akisogea kwenye benchi la Selema na kupiga naye picha kama wanavyoonekana pichani.

 

Mwingine aliyefurahishwa na kauli hiyo ni Mwanachama maarufu wa Yanga mkoani Morogoro Mzee Leold Massawe kutoka tawi kuu la Yanga la mkoani hapa.

 

Mzee Massawe ambaye ni Mwanajeshi Mstaafu mara nyingi Yanga inapofika Mkoani Morogoro  mtadaoo huu humshuhuidia akiongoza kitengo la Ulinzi na usalama wa timu yao.

 

‘Mjeda’ huyo ambaye ni Muumini mzuri wa kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro kwenye lbada hiyo alikuwa ni miongoni mwa mshuhuda wa Ndoa hizo.

 

Wakati akihojiwa na Mtandao huu Mzee Massawe [Yanga Lia lia] alichana Waleti yake na kuchomoa kadi  mbili za Yanga ile ya uwanachama na ile ya Bank akimuonyesha Mwandishi wa habari hizi.

            MSIKIE ASKOFU .

Siku hiyo hiyo ya ijumaa majira ya usiku Mtandao huu ulimtwangia simu Askofu Msimbe na mahojiano yetu yalikuwa hivi.

Mtandao. Tumsifu Yesu Kristo baba Askofu.

Askofu. Milele Amina karibu.

Mtandao. Wakati mmoja wa maharusi akitoa neno la shukrani kwa wema uliowafanyia alipoitaja Yanga ulishindwa kujizuia akuangua kicheko,kwa kitendo hicho baadhi ya waumini wako waliibuka minong’ono wakisema wewe ni shabiki wa Yanga je ni kweli wewe ni Yanga au Simba Wazee wa Ubaya Ubwela?

Askofu. Kabla ya kujibu kaangua kicheko kisha akasema.

Niwe mkweli naipenda sana Yanga ikifungwa naumia sana na ikifanya vizuri nafurahi sana hivyo huyu Bwanaharusi kwenye neno lake la shukrani kwangu na kwa kanisani mwisho aliitaja Yanga jambo hilo pia limenifurahisha kwa sababu ametaja timu yangu ya Moyoni.

Mtandao. Sawa asante nikutakia usiku Mwema.

Askofu. Nakwako pia.

Tuesday, August 19, 2025

NDOA YA VIKONGWE YAFANA, ASKOFU AWEKA NENO

Baba Askofu Msimbe akiingia kanisani huku akiwapungia waumini wake
......Maharusi wakivishana pete baada ya kura kiapo cha Ndoa

.....Maharusi  hao 101 pamja na wasimamizi wao 101   ndugu na jamaa zao wakiwa nje ya kanisa wakijiandaa kula chakula kiihcho andaliwa na baba Askfu
Muonekana mzuri wa kanisa katoliki Parokia ya Kigunyenyembe

                     Askofu Msimbe akiombea chakua

.

           Na Dustan Shekidele Morogoro.

IJUMAA iliyopita kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro kupitia kiongozi mkuu wa Jimbo hilo Askofu Lazarus Vitalis Msimbe, wameandaa ndoa za mafungu.

 

Katika ibada hiyo ya ndoa iliyofanyika Parokia ya ‘Bikira Maria Mama wa Kanisa’ Kigurunyembe kata ya Kilakala Mkoani hapa.wanandoa 101 walijitokeza kubariki ndoa zao‘kupasha Moto Kiporo’ huku kivutio kikubwa kikiwa kwa mahurusi ‘Vikongwe’  Silali Banyakirusa mwenye umri wa miaka 75 na mchumba’ke Bibi harusi Kalolina Mshauri mwenye umri wa miaka 77’

Baada ya kura kiapo cha ndoa na kuunganishwa kuwa mwili mmoja Mtandao huu uliwafuata maharusi hao na kufanya nao mahojiano maalum  wa kwanza fungunguka aikuwa bwana hasusi

Mtandao. Mzee wangu shikamoo na hongera kwa kufunga Ndoa.

Bwana Harusi. Marahaba na asante kwa pongezi.

 

Mtandao. kwa mtazamo wangu kwa maharusi wote 101 wewe na mkeo ndio mnaonekana kuwa na umri mkubwa je una miaka mingapi na mmeishi kwenye uchumba kwa muda gani?

 

Bwana harusi. Mimi ninamiaka 75 na uchumba wetu unamiezi 2 tu, jumapili kama mbili hvi zilizopita tumesikia tangazo kanisa kwamba Askofu wetu ameandaa ndoa kwa waumini wake hivyo  tumejiandikisha na hatimaye Leo tumefunga ndoa binafsi namshukuru sana baba Askofu kwa jambo hili

Mtandao. Kweli nimeamini kila jambo la Kheri lina kuwa na baraka za Mungu.mkiwa ndani ya penzi Jipya lenye umri wa miezi 2 ikatokea nafasi hii hadhimu ya kufunga ndoa.

 Umesema uchumba wenu ni mchanga je awari ulikuwa na mahusiano mengine nakama uikuwa nayo umejaliwa kupata watoto na wajukuu wangapi?

Bwana hasuri. Nikweli huko nyuma nikuwa na mahusiano mengine nimejaliwa kupata watoto  4 na wajukuu 9

Mtandao. Asante kwa ushirikiano nawaombea kwa Mungu abariki ndoa yengu iwe ya amani na furaha huku mkibebeana misalaba kwenye madhaifu yenu kwani hakuna binadamu mkamilifu isipkuwa Mungu pekee.

 

Bwana haurusi. Asante sana kwa maneno ya hekima.nawe Mungu akubariki kwenye kazi zako.

 

Kwa upande wake Bibi harusi amesema yeye na Mumewe huyo wanaishi Kichangani baada ya kukutana wameamua kufunga ndoa ns utu uzima wao.

 

“ Unajua lbada njema huanzia nyumbani sasa kama mnaishi kinyumba miaka nenda miaka ludi nyumbani yenye haiwezi kuwa na baraka ndio maana na utu uzima wetu huu mimi na mwenzangu baada na kupata fursa hii tumeamua kuichangamika”amesema Bi. Kalolini.

 

Kama ilivyo kwa mumewe Bi Kalolini awari alikuwa na mahusiano mengine na alipoulizwa ana watoto na wajukuu wangapi alijibu.

 

“kwa umri wangu huu wa miaka 77 nimejaliwa kupata watoto 7 na wajukuu 14”

 

                 AMSIKIE ASKOFU SASA.

Kutokana ubize na uchovu wa kufungisha kwa mpigo ndoa hizo 101 busara zilimungoza Mwandishi wa habari hizi kumpa muda wa kupunzika Askofu Msimbe na kwamba siku iliyofuata majira ya usiku Mtandao huu ulimtwangia simu Askofu huyo na kufanya naye mahojiano kama ifuatavyo.

 

Mwandishi. Baba Askofu Tumsifu Yesu Kristo

Askofu. Milele Amina

 

Mwandishi.Pole kwa kazi ngumu ya jana ya kufungisha ndoa 101 lakini nikupongeze kwa uchungaji mzuri wa ndoo yako uliofanikisha kuwarejesha  zizini mwa bwana kutoka kwenye dhambi ya kuishi bila ndoa.

 

Askofu Asante sana kwa maneno  ya faraja.

 

Mwandishi. Taarifa nilizo nayo ni kwamba shughuri nzima umeandaa wewe ikiwemo chakula cha watu zaidi ya elfu moja tuliokuwa pale kanisani tumekula na kunywa je ni pesa za kanisa au zimetoka mfukoni kwako ?

 

Swali la pili niliwaona maharusi kutoa Maeneo ya mbali kama vile Mzumbe, Lukobe Mkundi Tungi,Misongeni na Kingolwira je umetumia njia gani kuwapa taarifa?

 

Askofu. Kwanza ufahamua  tukio lile ni la Jimbo lote la Morogoro ambalo mimi naliongoza ndio maana umeona wanandoa tukoka maeneo yote ya Jimbo.

 

Kuhusu taarifa nilimpa kazi hiyo Msaidizi wangu Padri Sewando ambaye aliwaagiza makatekista wote jimboni kuwatangazia waumini wetu uwepo wa jambo hilo.

 

Kimsingi tukio lile lilipaswa lifanyike kanisa kuu la Mt. Patrick kama unavyojua kanisa hilo kwa sasa lipo kwenye ukarabati Mkubwa ndio maana tukaamua kufanya pale Parokia ya Kigurunyembe.

 

Kuhusu kuandaa shunguli ile ni mimi niiyendaa  nimetumia million 10 kuanzia chakula na gharama nyingine.

 

Mwandishi.Mungu akubariki sana kwa Moyo wako huo. pale kanisani palikuwa na minong’ono wakiuliza kama utaanda tena tukio kama hili je jibu lako ni lipi  kwa hao waumini wako?

 

Askofu. Swali zuri Mungu akipenda mwenzi wa 12 tutaandaa tena tukio kama lile hivyo waumini wetu wajiandae.

 

Mwandishi Sawa mtumishi wa Mungu barikiwa sana na asante kwa ‘time’ yako.

 

Askofu Asante na wewe pia usiku mwema.

 

Katikati ya Ibada hiyo mmoja wa maharusi aiyepewa nafasi ya kutoa neno la shukrani. kaitaja timu ya Yanga  Askofu katia neno.habari hiyo na picha itaruka hewani hivi punde hivyo endelea kuwa jirani na Mtandao huu muda wote.

 

 

 

Sunday, August 17, 2025

BIG MARCH MANCHESTER UNITED DHIDI YA ARSENAL.





 


TIMU Kabambe ya Arsenal ‘Chama a Wana’ Usiku huu wameiadhibu ‘Kibonde chao’  Manchester United kwa kuichapa bao 1-0 Bao hilo pekee imefungwa mapema dakika 13 na fundi wa mpira  R. Calafion

 

Bao hilo lilitosha kukata ngebe za mashabiki wa Man U walijazana kwenye uwanja wao wa Tofari za kuchoma Old Trafford.

 

Kwa sasa sisi mashabiki wa Arsenal ni Mwendo wa kupiga ‘Pushapu’pichani shabiki lia lia wa Arsenal Washikabunduki wa London anayejulikana kwa jina la Dustan Shekidele akiwa kwenye matukio mbali mbali na jezi za Arsenal.

 

VITUKO VYA MWEZI JANUARI

  Mwezi uliopita tumeshehelekea Siku Kuu mbili X Mas na Mwaka Mpya.   Mwezi huu dume January tunashehelekea kulipa Ada za Shule na kod...