Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Wednesday, April 30, 2025

YARIYOJIRI KUMBI ZA STAREHE MWISHONI MWA WIKI, MAISHA MAPYA YANGUSHA MOJA MOJA UKUMBINI.






 


Na Mlala Nje Dustan Shekidele,Morogoro.

 BAND ya Maisha Mapya’Vijana wadogo waliokomaa Vichwa kwa Ugumu wa Maisha’ Wiki End iliyopita wameuwasha Moto kwenye ukumbi Mmoja uliopo Msamvu Iringa Road kwa kuangusha moja moja mpaka Majogoo yalipowika mara tatu.

Baada ya kuwapagawisha mashabiki ‘Big Boss’Mmiliki wa Band hiyo Joshua Malekela Maafuru Joshkela Msingisi Mwamba kutoka Kijiji cha Msingi Wilaya ya Gairo Mkoani Morogoro, aliacha kuimba akanyoosha mkono juu kuashiria vijana wake wamtwangie Sebene kavu.

Hapo sasa Joshua  kutupa Mic Chini akaanza  kunengua akijigaragaza chini huku akiteleza kwenye jukwaa kama kambara kwenye tope.

Kwa umahiri huo baadhi ya Mashabi walivutiwa na shoo hiyo wakaamua kunyanyuka kwenye viti na kumtunza pesa.

Wiki End ijayo Mlala Nje atahudhuria shoo ya Band ya Waluguru Original.kusaka matukio.

Mpendwa Msomaji wa Mtandao pendewa wa Shekidele kile kipengele chetu cha stori kali ya Mtaa kitaendelea hivi karibu ambapo Mtandao huo umenasa habari kali ya Kitaa.

 Kwa sasa Mwandishi wa Mtandao huu anakamilisha Stori hiyo kwa kumsaka Askofu wa Kanisa kutoa ufafanuzi wa habari hiyo hivyo endelea kuwa jirani na Mtandao huu muda wote kufuatilia habari hiyo kubwa kwenye Jamii yetu.

 

Sunday, April 27, 2025

VAR YA MTANDAO WA SHEKIDELE IMEBAINI TUKIO HILI.

                   Nassirin Kombo beki wa Tabora United










 

.

   Na Dustan Shekidele,Morogoro.

KWENYE Berby ya juzi ya Michuano ya Ndondo Cup,kati ya Mangolo Fc na Washashi Fc iliyopigwa uwanja wa Saba saba Mkoani hapa na timu hizo kutoka eneo Moja la Mwembesongo  zilitoka Suluu ya 0-0.

Dakika 67 beki wa Mangolo Fc Nassiri Kombo Maarufu ‘Nasri Sccoba’ambaye ni mchezaji wa timu ya Tabora United akijiunga na timu hiyo msimuu huu akitokea Mtibwa Sugar ya Manungu  Kata ya Mtibwa Tarafa ya Turiani Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro.

Akijiamini huku akiwa mtu wa Mwisho aliuchezea mpira nje ya 18 na kujikuta akinyang’anywa na Winga wa Washashi Shani Adrew aliyemzunguka na  kuingia ndani ya 18.

 

 Wakati winga huyo mwenye mbio kama swala akijiandaa kufunga Nasri Sccoba alimkwatua kwa nyuma na kuanguka chini akiuacha mpira ukinyakwa kirahisi na Kipa.

Kwa Mujibu wa sheria 17 za Soka tukio hilo lilipaswa kuwa  Pelnaty lakini Mwamuzi wa mchezo huo alipeta akiashiria hakuna fau, tukio hilo lilisabisha Rais wa Washashi Fc kuingia uwanjani akitaka kumpiga refa.

Kabla ya kumkaribia refa huyo baadhi ya wachezaji wa Washashi walimdaka kiongozi wao huyo na kumtoa nje ya uwanja na mpira ukaendelea na kutamatika kwa Suluu.

Kwa sababu mchezo huo ni lazima mshindi apatikane timu hizo ziliingia kwenye kipengele cha kupigia mikwaju ya pelnati ambapo Mangolo Fc ‘Vijana wa Dida Masela’ walifanikiwa kutinga Nusu fainali baada ya kuwafunga Washashi kwa Pelnati 7-6.

Mpiga picha wa Mtandao aliyekuwa uwanjani hapo na kamera yake ya kisasa yenye Viwango vya VAR [Video Assistart Referee] alirekodi tukio hilo hatua kwa hatua kila picha moja ilipiga kwa sekundi 1 hivyo ndani ya sekunde 11 kamera hiyo yenye uwezo wa kwenda na kasi ya mpira ilipiga picha 11 kama zinavyoonekana pichani.

Pia kamera hiyo inauwezo wa kupiga picha umbari  wa mita 300 kwa wakazi wa Dar es salaamu umbali huo ni kama kutoka Ubungo Plaza Mpaka Manzese Darajani ‘Tip Top’.

 Kwa wakazi wa Morogoro umbali huo ni  kutoka Msamvu Shule eneo la Mtaa  Mpaka Msamvu Stend ya Mabasi, wahenga wana sema kujisifu sio dhambi ila dhambi ni kuziendekeza hizo sifa.

Hivyo kama una sherehe yako yoyote wasiliana na Mpiga picha wa Mtandao huu kwa namba 0754 28 90 73. Whatssap No 0715 289073 bei zake ni karibu na bure,ma anazingatia utu zaidi kuliko biashara.

 

   

Friday, April 25, 2025

ROBO FAINALI YA NDONDO CUP. DERBY YA MWEMBESONGO YATAMATIKA KWA MIKWAJU YA PELNATI.

Beki kisiki wa Mangolo Fc Sady Mapuya akimiliki mpira huku akinyemelewa na mshambuliaji wa Washashi Fc Shani Adrew ambaye alikuwa mwiba mkali kwa mabeki wa Mangolo.

Ifahamike  Mapuya alikuwa beki kisiki wa Lipuli ya Iringa wakati huo ukishiriki Ligi kuu, baada ya timu hiyo kushuka daraja Mapuya aliikimbia na kurejea nyumbani kwao Morogoro ambapo kwa sasa anaitumikia timu ya Moro Kids inayoshiriki Ligi daraja la Pili akiwa Nahodha wa kikosi hicho.




 


      Na Dustan Shekidele,Morogoro.  

ROBO Fainali ya kwanza ya Ligi za Mtaani Maarufu ‘Ndondo Cup’ iliyozikutanisha timu  mbili kutoka Mtaa mmoja, Mangolo Fc na Washashi Fc umepigwa jana Uwanja wa Saba saba kwa Mangolo kuibuka na ushindi wa Pelnati 7-6 baada ya dakika 90 miamba hiyo  kutoka suluu 0-0.

Timu hizo zilizosheheni wachezaji wengi nyota nchini zinatoka eneo mmoja zikitengwanisha na shule ya Msingi Mwembesho, Maskani ya Mangolo ipo eneo la uwanja wa michezo wa shule hiyo huku Maskani ya Washashi ikiwa geti kuu la kuingia kwenye shule hiyo.   .

 kwenye Mtanange’Derby’ hiyo iliyokuwa ‘tamu’ kwa muda wote wa dakika 90  Video Assistart Referee[VAR] ya Mtandao wa Shekidele iling’amua tukio moja tata lililosababishwa na na beki wa Mangolo Fc  ambaye pia ni mchezaji wa Tabora United inayoshiriki Ligi kuu.

Tukio hilo litaruka hewani hivi punde hivyo endelea kuwa jirani na Mtandao huu muda wote.

                 

Wednesday, April 23, 2025

YARIYOJIRI KUMBI ZA STAREHE SIKU KUU YA PASAKA. RUVU STARS BAND YAKINUKISHA MOROGORO.











 


Na Mlala Nje Dustan Shekidele,Morogoro.

KUSHEHEREKEA Siku kuu ya Pasaka Band ya Ruvu Stars’Wazee wa Kuku na Mayai yake’ kutoka Mkoa wa Pwani, Jumapili ya Pasaka wameuwasha Moto mkali kwenye ukumbi wa Florida uliopo Msamvu Mkoani hapa.

Kama kawaida kwenye siku kuu hiyo ya Pasaka ambayo Wakristo wote duniani walisheherekea kufufuka kwa Mokozi wao Yesu Kristo’Nabii Issa’ aliyeishinda mauti na kuushangaza ulimwengu  baada ya kuuwawa kikatili na watesi wake kisha akafufua ndani ya siku tatu toka alivyozikwa, Mlala Nje alizunguka kumbi za Starehe kusaka matukio.

 Kwenye shoo hiyo kivutio kikubwa kilikuwa kwa Wanenguaji wa Band hiyo ambao walikongo nyoyo za mashabiki waliojazana kwenye ukumbi huo uliopo jirani na Stend ya Mabasi ya Mikoani ya Msamvu.

Moja ya Vionjo vya madensa hao ni kurusha sarakani jukwaani eneo na kupanda juu ya nguzo za jukwaa na kunengua wakiwa huko huko kirereni mwa nguzo hizo za plastiki.

Akihojiwa na Mlala Nje Kiongozi wa band hiyo  Mponda Mahmoud Maarufu MK Masauti[Pichani mwenye Mic mdomoni na flana nyeupe] amesema wamefunga safari kutoka Ruvu  kuja Morogoro kutoa burudani ya viwango kwa mashabiki wa Mji kasoro bahari[Morogoro].

Baada ya kukamilika kwa shoo hiyo majira ya saa 9 usiku Vijana hao wa Ruvu waliingia kwenye Lori la Jeshi na kurejea Ruvu Mkoa wa Pwani kwa kuendeleza burudani kwenye viwanja vya maeneo hayo.

 

MAKALA PLANET NDONDO CUP. SIRI DAMU CHAFU KUTWAA UBINGWA MARA MBILI MFURULIZO HII HAPA.

  Baadhi ya mashabiki waliofulika kwenye mashishindano hayo.                           .....Kikosi cha Damu chafu Mkuu wa Wilaya Mhe Kilakal...