Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Friday, April 11, 2025

DAWA YA KUZUIA VIFARANGA VYA KUKU KULIWA NA MWEWE HII HAPA.



 


       Na Dustan Shekidele,Morogoro.

UTAFTI wa kienyeji uliofanywa na baadhi ya wananchi wa Mkoa wa Morogoro umebaini kwamba  rangi ya ukindu ni kinga sahihi ya vifaranga vya kuku kukamatwa na Ndege Mwenye Maafufu ‘Kipanga’.

Kufuatia hali hiyo wiki hii Mwandishi wa habari hizi aliingia mtaa kuichimba habari hiyo ambapo juzi alikatiza Mtaa wa Mafisa Mwanzo Mwisho Kata ya Mwembesongo na kushuhudia Vifaranga vya kuku vikiwa na rangi hiyo ya ukindu.

Taarifa zinadai baada ya kuzaliwa vifaranga hivyo vilitumbukizwa kwenye kopo lenye rangi ya Ukindu kwa lengo la kuvilinda visikamatwe na Mwewe.

Akizungumza na Mtandao huu mmoja wawananchi wa Mkoa wa Morogoro Asha Juma alisema” Kwa umavyojua kwa sasa biashara ya kuku wa kienyeji imekuwa nzuri sana, bei ya chini Jogoo ni elfu 30, na teteza kwa maana ya kuku jike ni elfu 20.

Sasa tuna vita kali na Mwewe kuku anaweza kufyatua vifaranga 11 utakuta viwili tu ndio vinakua vingine vyote vinaliwa na Mwewe, hivyo tumebuni mbinu hii ya kuvipaka ukindu ambao unamzuia Mwewe kukamata vifaranga”alisema Bi Mkubwa huyo na kuendelea kudadavua.

“ Ukienda Vijijini ambako kuna Mwewe wengi mfano Mikese, Kiloka, Mkambarani. Ubena, Bwawani. Gwata unaona wafungaji wengi wa kuku wanatumia mbinu hiyo ya ukindu.”alimalizia kusema Mama huyo. Alipoulizwa kitu gani kinachomfanya Ndege huyo aina ya Mwewe, kuogopa kuvikamata vifaranga hivyo vya Ndege aina ya Kuku.?

Alijibu “Kwa Mujibu wa utafiti wetu wa kienyeji Mwewe haipendi harufu ya rangi ya ukindu”

                  UKINDU NI NINI.

Ukindu ni rangi ya mkeka ambayo pia kwa baadhi ya wafanyabiashara wa mbao wasio waaminifu huitumia kupaka kwenye mbao na kuwadanganya wateja wao kama ni dawa ya mchwa na wadudu wanaopekecha mbao.

Ushauri na Mwandishi wa habari hizi kwa wanunuzi wa mbao kwa lengo la kupaua nyumba zao, kama unamshaka na anayekuuzia mbao hizo ni hari ununue dawa hiyo ya mchwa Og wewe mwenyewe inauzwa bei mbaya kikopo kidogo elfu 20 na kopo kubwa elfu 40.

Matumizi ya dawa hiyo ili iwe kali zaidi kopo dogo unachanganya na maji lita 20 unaloweka mbao hizo kwenye maji hayo yenye sumu kwa dakika 20 mbao hizo zitakunywa maji hayo yenye sumu hiyo kiboko ya mchwa na wadudu wanaokula mbao.

Tuesday, April 8, 2025

LIGI YA MABIGWA BARA LA ULAYA.ARSENAL AMFANYIA KITU MBAYA BINGWA MTETEZI


 


            Na Dustan Shekidele.

WASHIKA Bunduki wa Jiji la Maraha la London nchini England Arsenal  usiku wa leo imeishangaza dunia baada ya kuwakanda Mabingwa wa kihistoria wa Ligi ya Mabingwa Ulaya’UEFA Champion League’ Real Madrid ya Hispania  kwa kuinyuka bao 3-0.

Mabao yote yamefungwa kipindi cha pili na Mwamba Rice aliyefunga mabao 2 kwa mikwaju ya faulo nje ya 18.

Bao la kwanza akifunga dakika 58 na la pili akifunga kwa style hiyo hiyo dakika 70, huku bao la 3 likifungwa na Merino  dakika ya 75

Gemu hiyo ya mkondo wa kwanza imepigwa majira ya saa 4 usiku na kutamatika Muda huu saa 6 usiku kwenye Uwanja wa Emirates unaomilikiwa na  Arsenal,  mechi ya maludiano inatarajiwa  kupigwa wiki ijayo Jijini Madrid Hispania kwenye dimba la Santiago Bernabeo.

  Real ambao ni mabinga watetezi wa kombe hilo ili wafanikiwa kuvuka Nusu fainali na kutetea ubingwa wao wanapaswa kuifunga Arsenal bao 4-0.

Kinyume na hapo watakuwa wamevuliwa ubingwa na chama hilo la Wana Arsenal ambao kwa sasa ni moto wa kuotea mbali hapa duniani,tusubiri tuona matokeo ya gemu ya Mkondo wa pili.

Pichani Mwandishi wa habari hizi ambaye ni shabiki lia lia wa Arsenal akiwa amejifunika shuka la timu hiyo.

Monday, April 7, 2025

KARUME DAY, MH DIWANI ATOA SADAKA KWA NDEGE NJIWA.

                                    Ramadhan Rajabu
                                                     Nassoro Hamoud' Mpemba'

                                Mhe Hassan Malingo

 


       Na Dustan Shekidele Morogoro.

AMANI ya Mwenyezi Mungu iwe nanyi wadau wote wa Mtandao Pendwa wa Shekidele, ama baada ya salamu, naomba radhi kwa kutokuwa hewani kwa takribani siku 10.

Hii ni baada ya kuwa likizo iliyonifanya niende sehemu kupunzisha akili, nimerejea Leo kuendeleza kazi ya kuwapa habari Moto Moto za chini ya Kapete hivyo usicheze mbali na Mtandao huu kuna habari kali.

Nimeanza Kazi Leo Jumatatu ya April 7 siku ambayo Taifa la Tanzania Linaadhimisha kumbuziki ya Kifo cha Mpendwa wetu hayati Abeid Aman Karume Rais wa kwanza wa Zanzibar.

Hayati Karume aliuwawa na watu wasiojulikana Apeil 7 -1972 hivyo Leo April 7- 2025 ametimiza miaka 53 ya kifo chake.

Kama kawaida Mwandishi wa Mtandao huu ambaye siku zote anatumia ubunifu mkubwa kusaka habari za tofauti, Leo baada ya kuanza kazi aliamua kwenda Mtaa wa Karume uiopo kata ya Mji Mkuu Mkoani hapa kwa lengo la kuzungumza na wananchi wa Mtaa huo uliobeba jina la Karume.

Nilipofika kwenye mtaa huo moja kwa moja nilitinga kwenye Mgahawa wa Mpemba ambao ni maarufu mkoani hapa kwa kuuza Al- Kasusu. Karanga, Maandazi Kacholi Asari na Juice ya Bungo.

Mtandao huu ulipofika kwenye Mgahawa huo ambao  upojirani na Msikiti wa Karume alimshuhudia diwani wa Kata hiyo Mhe Hassan Malingo[aliyechuchumaa] akitoa zawadi ya Karanga mbichi kwa kundi kubwa la Njiwa waliokuwa wakimpanda mikononi mabegani na kichwani wakigombea zawadi hiyo ya chakula.

Mhe huyo lifanya hivyo kwa kushirikiana na Mmiliki wa Mgahawa huo  Mpemba Nassoro Humoud.

Akihojiwa na Mtandao huu Mhe Malingo alisema”Leo ni karume Day kwenye kata yangu ya Mji Mkuu inamitaa miwili yenye majina ya hayati karume,kuna Mtaa wa Aman ule pale juu na hapa tulipo ni Mtaa wa Karume.

Hivyo muda huu nimetoka kuswali nimepita hapa kunywa Kasusu nimeona ninunue karanga nitoe sadaka kwa hawa Njiwa shekidele na wewe karibu unywe kasusu”alisema Mhe Maingo

lfahamike Mhe Malingo kabla ya kuuvaa udiwani wa kata hiyo iliyopo katikati ya Mji alikuwa Katibu Mkuu wa timu ya Moro United  “Chelsea ya Bongo”iliyomiikiwa na tajiri wa mafuta mwana Morogoro Mwarabu Merey Balhabou.

Wachunguzi wa Mambo wanadai kata hiyo  ndio kati tajiri kati ya kata 29 za Jimbo la Morogoro,ikifuatiwa na kata ya Mafisa yenye viwanda vingi na Stend ya Mabasi ya Msamvu.

 Kwa upande wake Mmiliki wa Mgahawa huo Hamoud alisema Njiwa hao sio wake ni wamajirani zake, wamezowe kufika eneo hilo kila siku kwa sababu huwapa chakula kama sehemu ya sadaka yake kwa viumbe hao.

                 HISTORIA FUPI YA NJIWA

Miaka ya nyumba Mungu alichukizwa na  vitendo viovu vilivyofanywa na binadamu hapa ulimwenguni kabla ya kuuangamiza ulimwengu kwa maji alimwambia Nuhu atengebeze safina na wale watakatifu waliingia kwenye hiyo safina.

Baada ya safina hilo kutengemaa na watu wake safi kuingia ndani ,Mungu alionyesha uunguwake kwa watenda dhambi alishusha Upepo mkali nayo maji ya Gharika ya maji ilishuka kutoka milimani,kwa siku Arobaini Mfurulizo Nuhu na wenzie walielea kwenye safina ‘Mwanzo 7-11-13’

Baada ya siku kadhaa kupita watu hao walimtuma ndege Kunguru kwa sababu anauwezo wa kuruka  akaangalie kama maji yamekauka ili watoke kwenye safina.

Kunguru alipofika na kukuta maji yamekauna huku eneo hilo likitapakaa mizoga ya wanyama na watu Mwamba huyo aliamua kula mizogo hiyo na kusahau kurejea majibu kwa aliyemtuma.

Watu hao baada ya kuona kunguru harudi wakaamua kumtua Njiwa ambaye alikuwa Mwaminifu alikuta maji yamekauka, hivyo hakuwa na tama ya kula mizoga alichofanya alitua chini na kuchukua jani kavu mdomoni fasta akareja kwa aliyemtuma na mueleza kwamba huko mambo ni swali maji yamekauka kiasi cha kutua chini na kubena kijiti.

Kwa histori hiyo ndio maana mpaka Leo Njiwa anapotaka kutaga anajenga kiota chake kwa kuokota vijiti vikavu, huku Kunguru akiendelea kuwa kero mtaani kwa kukwapua mizoga, ukiacha wazi sinia lako la samaki utakuta leupe.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

DAWA YA KUZUIA VIFARANGA VYA KUKU KULIWA NA MWEWE HII HAPA.

         Na Dustan Shekidele,Morogoro. UTAFTI wa kienyeji uliofanywa na baadhi ya wananchi wa Mkoa wa Morogoro umebaini kwamba   rangi...