Na Mlala Nje Dustan Shekidele,Morogoro.
KUSHEHEREKEA Siku kuu ya Pasaka Band ya Ruvu Stars’Wazee wa Kuku na Mayai yake’ kutoka Mkoa wa Pwani, Jumapili ya Pasaka wameuwasha Moto mkali kwenye ukumbi wa Florida uliopo Msamvu Mkoani hapa.
Kama kawaida kwenye siku kuu hiyo ya Pasaka ambayo Wakristo wote duniani walisheherekea kufufuka kwa Mokozi wao Yesu Kristo’Nabii Issa’ aliyeishinda mauti na kuushangaza ulimwengu baada ya kuuwawa kikatili na watesi wake kisha akafufua ndani ya siku tatu toka alivyozikwa, Mlala Nje alizunguka kumbi za Starehe kusaka matukio.
Kwenye shoo hiyo kivutio kikubwa kilikuwa kwa Wanenguaji wa Band hiyo ambao walikongo nyoyo za mashabiki waliojazana kwenye ukumbi huo uliopo jirani na Stend ya Mabasi ya Mikoani ya Msamvu.
Moja ya Vionjo vya madensa hao ni kurusha sarakani jukwaani eneo na kupanda juu ya nguzo za jukwaa na kunengua wakiwa huko huko kirereni mwa nguzo hizo za plastiki.
Akihojiwa na Mlala Nje Kiongozi wa band hiyo Mponda Mahmoud Maarufu MK Masauti[Pichani mwenye Mic mdomoni na flana nyeupe] amesema wamefunga safari kutoka Ruvu kuja Morogoro kutoa burudani ya viwango kwa mashabiki wa Mji kasoro bahari[Morogoro].
Baada ya kukamilika kwa shoo hiyo majira ya saa 9 usiku Vijana hao wa Ruvu waliingia kwenye Lori la Jeshi na kurejea Ruvu Mkoa wa Pwani kwa kuendeleza burudani kwenye viwanja vya maeneo hayo.
No comments:
Post a Comment