Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Monday, December 30, 2024

MASHABIKI WAFURIKA KUSHUHUDIA DERBY KALI YA NDONDO CUP.




Black Peole wakichomoa bao hilo na kumuacha kipa wa Viba Gumbo Mfaume akidaka hewa.

 
Bauns Big Suma kutoka Gym ya Bad Boya Mjini Mpya akiwa makini kulinda usalama kwenye Dabi hiyo
.


Kiungo fundi wa Black Viba akiwatoka mabeki wa Back people na kufumua shuti kali lililopaa juu ya gori


Kweli kutoka kisoka ni bahati jamaa huyu Kiungo fundi wa Mpira Star Mwande ambaye kwenye Dabi hiyo aliitumikia Black People kama kawaida yake juzi alikichafua sana kwenye gemu hiyo



 

 

    Na Dustan Shekidele,Morogoro,

Mashabiki wa Soka Mkoa wa Morogoro juzi walifurika Uwanja wa  CCM Saba saba ‘Shamba la Babu’kushuhudia Derby kali ya Ndondo Cup kati ya timu mahasimu Mkoa hapa, Black People’Taifa la Watu weuzi kutoka Kata ya Mji Mpya na Black Viba ‘Watakatifu Weusi’ kutoka Kata ya Mbuyuni.

Katika Dabi hiyo ya Nusu fainali ya kwanza ya michuano hiyo ya Ndondo, hadi dakika 45 za kwanza zinatamatika,wababe hao walitoka sale ya bao 1-1, Viba wakitangulia kupata bao dakika 36 na People kuchomoa bao hilo dakika ya 44 na kuzima ‘kigoma’ cha mashabiki wa Viba kilichokuwakikitamba uwanjani hapo.

Dakika 45 za pili zilianza kwa timu hizo zilizosheheni vyota wengi wa mkoa Morogoro wanajiandaa kutoka kwenda timu kubwa kushambulianza k wa zamu huku kila timu ikihitaji kuibuka mshindi na kutinga fainali.

Kwa mshangao wawengi dakika 57 gemu hiyo ilivunjika baada ya vulugu kubwa kutokea uwanjani, polisi waingilia kati.

 Kama kawaiwa Mpiga picha wa Mtandao huu alikusanya picha zote za vulugu hizo, hivyo endelea kuwa jirani na Mtandao huu  kuona picha hizo na kujua chanzo cha vulugu hizo.

Saturday, December 28, 2024

MWANA BIRTHDAY AGAWA NET KWA WATOTO YATIMA, WAELEZA CHANGAMOTO WANAZOPITIA I


  Mwana Birthday Shekidele akitoka nyumbani kuelekea kituo cha watoto yatima cha Mihayo.

                       ........Akiwasili kwenye kituo hicho
Mwana Birthday Shekidele akiendelea kugawa zawadi kwa watoro hao yatima.

.......Akigawa  chabarua chenye dawa ya kua Mmbu

Mwana Birthday Shekidele akimkabidhi zawadi ya nguo mtoto Kamila wa kituo hicho cha kulelea watoro yatima cha Mehayo
....Akizungumza na ndugu zake hao wanaoishi kwenye kituo hicho

 Mkoba wa kike aliokabidhiwa Matroni wa kituo hicho

.
Na Mwandishi Wetu Morogoro.
Mwandishi wa Mtandao huu. Dustan Shekidele. Desemba 25 aliadhimisha kukumbizi yake ya kuzaliwa’Happy Birthday kwa kukata na kula keki na watoto yatima wa Kituo cha Mehayo kilichopo Kata ya Mazimbu Mkoani hapa. 
 
Mara baada ya zoezi hilo lililoongozwa na Matroni wa kituo hicho Bi, Esther Daniel kutamatika, Shekidele alifungusha fuko la zawadi na kuwakazi watoto hao. 
 
Miongoni mwa zawadi hizo ni Nguo na vyandarua’Neti’ pamoja na mkoba wa kisasa aliopewa Matroni huyo kama motisha ya kazi kubwa anayoifanya ya kuwahudumia ndugu zetu hao wenye changamoto mbali mbali. 
 
                  MAZINGATIO YA ZAWADI.
 
Wasomani wa Mtandao huu watakumbuka Kwenye Birthaday ya Shekidele iliyofanyika Desemba 25-2023 kituoni hapo, mara baada ya Mwana Birthday huyo kukata keki na kulishana na watoto hao.
Aliuvua uwana Birthday na kuuvaa Uandishi wa habari ambapo alimuliza Matroni Esther changamo zilizopo kituo hapo ili mtu atakaye guswa aweze kusaidia.
 
Matron alisema.”Kwa niaba ya Mkurugeni wa kituo Mama Linda Sprian Gido tunakushukuru kwa zawadi unazozileta kila siku ya Birthday yako.
 
Kila Mwaka umefika hapa kituoni na kukata keki na hao watoto ambao wengi wao hawana wazazi hivyo ishu ya kukata na kula keki kwao ilikuwa kama ndoto”alisema Matroni huyo na kuongeza.
Kuhusu changamoto ziko nyingi baadhi ni ukosefu wa Sukari kama unavyojua hapa kituoni kuna watu zaidi ya 50 kwa namba hiyo unapima mwenyewe matumizi ya sukari kwa siku ni kiasi gani tukikosa sukari tunawachemshia uji asubuni. 
 
Changamoto ngingine ni chakula na Madawa, hapa kituoni tuna uhaba wa Net watoto wanalala bila chandarua kwa hali hiyo wanapata maradhi mara kwa mara, hivyo mtu atakayeguswa atusaidie Net kupunguza haya maradhi ya mara kwa mara nayokula pesa nyingi kama unavyojua Mtoto anavyoumwa hospital hawajua kama ni Yatima au Mlemavu wanataka pesa”alisema Matroni huyo.
Alipoulizwa kufuatia hali hiyo anamaombi gani kwa serikali? 
 
Alijibu.
 
Maombi yangu wasaidie vitu vya watoto yatima Bima ya Afya naamini hiyo inawapunguzia mzigo wamiliki wa vituo hivyo”
Kwa kuzingatia maombi hayo kwenye Birthday ya Mwaka huu Shekidele alibeba Net na kuwakabidhi watoto hao. 
 
Kuhusu ombi la Bima ya Afya kama serikali itasikia maombi hayo Shekidele amesema atajitolea kuisaidia serikali kwa kuwapiga passpot Size watoto wa Vitu vyote vya jimbo la Morogoro Mjini bure hata wakiwa zaidi ya 500.
 
Akithibitsiha hilo Shekidele alisema”Hasara Roho pesa makaratasi, mimi ni Mpiga picha kazi ya kuwapiga Passpoti Size watoto hao iko ndani ya uwezo wangu.
 
Kwenye maisha yangu nilichangua kazi ya Mwanasheria[Wakili] kwa lengo la kuwatetea wanyonge, baada ya kushindwa kufikia tamanio langu hilo kwa sababu za kiuchumi, nikageuika kwenye Uwandishi wa habari kwa lengo lile lile la kuwateta na kuwasemea wanyonge na watu wenye uhitaji.
 
Nikitumia karamu yangu kupaza sauti kwa wasio na sauti .”alisema Shekidele na kuongeza.
 
“Kwenye Birthday ya Mwaka huu nimewaahdi wale watoto kwamba Mwenyezi Mungu akinipa zawadi ya Uhai na kuniongeza Mwaka Mwingine basi Birthday ya Mwakani Desemba 25-2025 nitamkodi mpishi Maarufu wa Pilau Mkoa wa Morogoro apige Pilau kituoni hapo.
 
Wakiona kimya wajue waliompenda Mungu amempenda zaidi” Shekidele aliwambia watoto hao kama anavyoonekana pichani.

Wednesday, December 25, 2024

HAPPY BIRTHDAY MWANA WA MUNGU YESU KRISTO, HAPPY BIRTHDAY MWANA WA SHEKIDELE.




   Na Mwandishi wetu Morogoro.

DESEMBE 25  ni siku kuu ya Krismasi, siku ya kuadhimisha kumbukizi ya kuzaliwa Yesu Kristo yapata miaka 2000 iliyopita.

Taarifa za kuzaliwa kwake tena kwenye zizi la Ng’ombe Mjini Bethlehemu ziliposambaa kwamba Mfalme wa Wayahudi kazaliwa, Mfalme Herode kusikia hivyo, katoa agizo la kusakwa na kuuwawa watoto wote wa kiume wenye umri  chini ya miaka 2. Imeandikwa Mathayo 2 mstari 16.

Mungu ni Mwema licha ya msako huo Yesu aliponyeka na kuendeleza ufalme wake na kumuacha Mfalme Herode akiduwaa kwa amri yake hiyo ya kuuwa watoto  wasio na hatia kugonga Mwamba.  

Yesu aliendelea kuwindwa hatimaye  alipofika umri wa miaka 33 alikamatwa akapigwa mijeledi, akavishwa taji la miba kisha akitundikwa  Msalabani akapigiliwa misumari alipokaribia kukata roho Yesu alisema maneno haya ya kiyahudi ‘Heroi Heoi lama wa mabirai’ Maana yake Mungu wangu Mungu wangu Mbona umeniacha?.

 Baada ya kusema maneno hayo Yesu akainamisha shingo msalabani na kukata roho. Ukuu wa Mungu umetimia hakumuacha Mwanae, Yesu baada ya kuzikwa siku ya tatu alifufuka na kuwaacha watu midomo wazi wakishuhudia jiwe kubwa liliweka kwenye kaburi lake likiondolewa na Mwamba Yesu kafufuka.sote tusema Haleluya Mwana wa Mungu yu hai.

Leo Desemba 25-2024 tunaadhimisha Siku kuu ya Krismasi tukikumbuka kifo cha Mpendwa wetu Yesu Kristo aliyetoa sadaka maisha yake ili mimi na wewe tupone.

Siku kama ya Leo mikaa kadhaa iliyopita Familia ya Peter Zakaria Shekidele na mkewe Tumaini Samwel Juma walijaliwa kupata Mtoto wa Kiume waliyembatiza  jina la Dustan Peter Shekidele akiwa ni mtoto wao wa 5 kwenye familia hiyo iliyofunga kizazi na watoto 7.

 Hii Leo Desemba 25  Dustan anaunga na wakristo wote kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa na Mokozi Yesu Kristo.  

Akizungumza na Mtandao huu Dustan alisema. “Awari ya yote najisikia fahari kubwa kuzaliwa siku moja na Mwokozi Yesu, kwa mantini hiyo sote tuliozaliwa siku moja na  Yesu[Nabii lssa] tunapaswa kuishi maisha  ya kitakatifu kama alivyoishi Yesu ili tunavyoadhimisha siku hii  matendo yetu yakisi mema mengi aliyofanya Mwana Birthday mwenztu Yesu”alisema na kuongeza.

Kufuatia hali hiyo kama kawaida Leo jioni nitaadhimisha siku yangu ya kuzaliwa kwa kutembelea kituo cha watoto Yatima cha Mihaya kilichopo kata ya Mazingu Mkoani hapa.

Nikiwa huko nitakata keki na ndugu zangu hao kisha nitawapa zawazi kadhaa nilizojaliwa na Mwenyezi Mungu, baada ya kufanya hivyo Sherehe yangu itaishia hapo.

Inashangaza Mungu kakupa zawazi ya kukuongezea Mwaka, baada ya kumshukuru kwa kutenda mema ili mwakani akuongeze  mwaka Mwingine, unashuhudia mtu anakodi ukumbu na kuwanywesha watu bia baadae watu hao wake kwa waume wakishalewa baadhi yao wanasalitia ndoa zao na wasio na ndoa wanaansisha mahusiano mapya kupitia siku yako hiyo ya kuzaliwa, kwangu mimi hilo sio sawa mwenye masiki na asikie nasiye na msikio[….]”alimalizia kusema Shekidele.


 

Monday, December 23, 2024

DESEMBE 22 MY WANGU UMETIMIZA MIAKA 5 TOKA UIAGE DUNIA.

 


Neema Muilokozi akiweka shada la maua kwenye kaburi la Mama yake
Davidi Juma akiweka msalama kwenye kjburi la mama yake

....Msaafara ukiongozw ana Matarumbeta ulkielekea makaburini nyumbani kwa marehemu
Mwili wa bibi kete ukitokandani ya kanisa la KKKT Usharika wa Mlalo
                  Msafara umeasili nyumbani kwa marehemu
......Msafara umewasili Mkongoroni Mlalo Wilaya ya Lushoto Tanga
Mwandishi wa Mtandao huu aliyekti siti za mbele akicvhukua matukio yote ya barabarani, hapa msafara ukivuka daraja la Wami.
.......Msafara huo ukikatiza mitaa mbali mbali ya jiji la Dar
Mwili ukiigizwa kwenye gari tayari kwa safari la Tanga
Neema Mulokozi aliyekuwa akimuga mama  yake

Birthday yake ya mwisho iliyofanyika Sempemba 27 iliruka gazeti la Uwazi

Bibi Kete akimpa wosia Mjukuu wake Dustan Shekidele kwa Lugha ya Kisambaa



Bibi Kete akimrishs keki Mjukuu wake Dustan Shekidele

 

       Na Dustan Shekidele,Morogoro.

MKE wangu kipenzi, My Number One. Honey.Kabari yangu, Msiri wangu hayo yote ni majina mazuri niliyokuita Mpendwa bibi yangu Kete Abdallah ambaye jana  umetimiza miaka 5 toka ulipoiaga hii dunia, Desemba 22- 2019 ukiwa na umri wa miaka 103.

Watoto wako wapendwa Tumaini Samwel Juma Mrs.  Peter Zakaria Shekidele.ambaye ndiye Mama yangu Mzazi, David Samwel Juma na Neema Samwel Juma Mrs. Mulokozi wanakukumbuka daima.

Wajukuu, Vitukuu na Vilembwe zaidi 100 tunakukumbuka  Mpendwa bibi yetu tuna kumbuka ulipotimiza miaka 100 Wajukuu, Vijukuu na Vilembwe kwa pamoja tulikubaliana kila Mwaka tukufanyie sherehe Kubwa ya kumbukizi  ya siku yako ya kuzaliwa’Happy Birthday’.

Tunashukuru tulilimiza hilo kwa kukufanyia sherehe nyumbani kwako Moshi Baa Mombasa Gongola Mboto Jijini Dar es salaam na Birthday yako ya mwisho tuliifanya Septemba 27-2019 ulipotimiza miaka 103.

Mwaka huo huo Desemba 22 akiwa usingizini majira ya asabuhi alifariki dunia nyumbani kwake Moshi Baa Dar na maiti  kuhifadhiwa hospital ya Amana.

Kufuatia kifo hicho Mtoto  wa Kiume David Juma’Anko’ anayeishi Marekani aliomba mama yake asizikwe  mpaka afike, hivyo mwili huo iliendelea kusalia Mochwari hadi Desemba 25 alipowasili nchini.

 siku hiyo ya X Mas mwili  ulitolewa Mochwari na kuwekwa  ukumbi wa Hospital ya Amana ikafanyika lbada  kisha watu wa Dar walitoa heshima za Mwisho.

Baadae Mwili uliingizwa kwenye gari na safari ya kuelekea  Kijijini kwake Mlalo Lushoto Tanga kumpunzisha kwenye nyumba yake ya Milele ilianza kwa msafara wa magari zaidi ya 5.

Desemba 26 lbada ya kumuombea marehemu ilifanyika kanisa la KKKT Usharika wa Mlalo na baadae msafara ulioongozwa na Matalumbeta ulianza kuelekea kwenye kaburi  lilipo nje ya nyumba ya Marehemu tukampunzisha Mpendwa wetu kwenye nyumba yake hiyo ya Milele.

    MJUKUU KUSIMAMISHWA KAZI.

Kufuatia KIfo hicho Mjukuu wa Bibi huyo  alisimamishwa kazi kwa kile kichoelezwa na Uongozi wa kampuni ya yake ‘utoro kazini’.

Awari baada ya Mjukuu huyo kutoa taarifa za kifo hicho kwenye uongozi wa kampuni walimpa ruhusa ya wiki moja  sambamba na kutuma Mwakilishi kuiwakilisha kampuni kwenye msiba huo.

Kutoka na mazingira ya msiba huo wiki moja aliyopewa mfanyakazi huyo haikutosha hivyo ilimradhimu kukaa wiki mbili kumaliza msiba huo kufuatia kuchelewa kuzikwa kwa marehemu na ukubwa wa mziba wenyewe upande wa kifamilia.

 Hivyo huyo aliyefanya kazi kwenye kampuni hiyo kwa miaka 17 baada ya kurejea kazini alikutana na barua ya kusimamiswa kazi.

AlipojalibuLicha  kujitetea l utetezi wake haukusaidia chochote, hadi sasa miaka 5 imepita bado amesimamishwa kazina bila kulipwa chochote,

 lfahamike hadi sasa mtumishi huyo hajapewa barua ya kumfukuza kazi huku akiwa na baadhi ya vifaa vya kampuni hiyo.

Kwa mujibu wa uongozi  wa kampuni hiyo inayojihusisha  na mambo ya habari ulisema kwamba wanatoa ruhusa ndefu kwa mfanyakazi aliyefiwa na Baba,Mama, Mke\Mume au Mtoto la si kwa kila ndugu.

Hivyo kila Desemba 22 Mjukuu huyo jina kapuni ana kumbuka  machungu mawili ya kuondokewa na mpendwa bibi yake sambamba na kutimuliwa kazi kwa  kifo cha bibi yake inauma sana aishee.

Akizungumza na Mtandao huu Mjuu huyo alisema “kifo cha bibi yangu kinadhamani kubwa kuliko kazi” alisema kwa uchungu mkubwa.

 Alipoulizwa kama amekwenda kulalamika kwenye taasisi yoyote ya kiserikali Mjuu huyo alijibu.

 “Sijalalamika popote hapa chini ya jua  nimemshitakia MUNGU,ninachoweza kusema kila siku ya kumbukizi ya kifo cha bibi yangu Desemba 22 nitalalamika kwenye maeneo kama haya nikiadhimisha kumbukizi ya kifo cha mpendwa bibi yangu kilichoambatana na kutimuliwa kazi” alisema na kuongeza .

“Ningekuwa kwenye kipindi Redioni ningeomba nipigiwe  wimbo wa Muumini Mwijuma ‘Kocha wa dunia wa ’ Kifo cha baba yangu’ambaye naye yalimkuta kama haya yangu na kuamua kutumia kipaji chake cha uimbaji kulalamika dhdi ya Muajili wake”.alimalizia kusema Mjuu huyo wa kiume.

 

 

UJUMBE WA NANE LA MUNGU USALAMA WA WATU WAMUNGU.

Mwandishi wa Mtandao huu akiwa kwenye msitu Mnene Matombo Wilaya ya Morogoro Vijiji ........Mwandishi huyo akiwa Juu ya Milima ya Mgeta wila...