Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Saturday, August 31, 2024

MAUZA UZA YA AJALI.


Chuma imeingia kwenye Mtaro ndani ya kituo cha Mafuta Msamvu
....Wasamalia wema wakihangaika kuitoa kwenye Ngema
 


Na Dunstan Shekidele, Morogoro.

Gari ndogo yenye namba za Usajairi T 902 EDZ imeacha njia na kuingia kwenye mtaro ndani ya kituo cha mafuta[Sheli]iliyoo jirani na Stend ya Mabasi  Msamvu kando kando ya barabara kuu ya Morogoro- Dar es salaam.

Tukio hilo lililoshuhudiwa ‘Live’ bila chenga na Mwandishi wa Mtandao huu limetokea jana mchana ndani ya kituo hicho.

Wakizungumza na Mtandao huu mashuhuda wa tukio hilo walisema” Haya ni mauza uza gari hili jipya limetoka kwenye barabara  kuu ya Moro-Dar yenye msongamano Mkubwa wa magari, chaajabu huko halikutumbukia kwenye Mtaro. lilipoingia eneo hili la Sheli ambalo halina msongamano wowote wa magari limetumbukia kwenye hii ngema”alisema shuhuda huyo na kuongeza

“Tunashukulu  hakuna mtu aliyejeruhiwa ingawa gari limehalibikika kidogo muda huu dereva wa gari hili amekodi hilo Lori kama unavyoshuhudia tunahangaika kulivuta ili litokea kwenye hii ngema”alimalizia kusema shuhuda huyo aliyejitambulisha kwa jina la Juma Mbago. Naye Joseh Damas aliohojiwa alisema” Haya sio mauza uza wala nini kama alivyosema huyu mwenzangu ninachoona mimi huyu dereva alivyokuwa batabra kuu alikuw amakini alipoingia kwenye eneo hili la sheli kapunguza umakini huenda alikuwa akichezea simu kajikuta kaingia mataroni,  kwenye ukweli lazima tuseme ukweli”alisema shuhuda huyo kwa hisia kali

Wednesday, August 28, 2024

KIJIWE NONGWA. UKIONA KAFUTA BANGO UJUMBE UMEFIKA













 


Na Mpekunyuzi wa Mitandao Dunstan Shekidele.
 
Kama kawaida mtumishi wako, kila wiki naweka Bando linalonitembeza kwenye Mitandao ya Kijamii kukusanya jumbe mbali mbali.
Miongoni mwa jumbe hizo ni za Kuelimisha, Kukosoa na Maneno ya hekima yanayotukumbusha kuwa jirani na Mwenyezi MUNGU.
Tukutane Wiki Ijayo kwa mabango Mengine yenye Jumbe Moto Moto.

Tuesday, August 27, 2024

PIchani hii inayoonyesha Mji wa Morogoro niliipiga nikiwa juu ya Kilele cha Milima ya Uluguru.
Mwandishi wa Mtandao huu akionyeshwa moja ya mashamba yaliyopo juu ya Mlima huo na Mmiliki wa shamba hilo [hayupo pichani].
.......Nikitua Juu ya Kilele cha Milima ya Uluguru na Boda boda yangu ambayo iliniwezesha kufika kwenye kilele hicho

 Baada ya kushuka niliamu kupiga picha Mlima huom kumbuka nilikuwa juu kabisa ya Kilele cha Mlima huo wa Uluguru

UTALII WA NDANI.

Kuna nyakati Watanzania tunapaswa kutalii kwenye vivuti vyetu, pichani Mwandishi wa Mtandao huu aliamua kupanda juu ya kilele cha Milima ya Uluguru kwa kutumia boda boda yake.

Juu ya Milima hivyo kuna vivutia vingi miongoni mwao ni Ndege na Vyura ambao dunia nzima wanapatikana kwenye mlima huo pekee.

Kivutia kingine ni eneo la ‘Morning Site’ eneo hilo siku zote linaonekana ni asubuni likitandwa na mawingu na kwamba hata jua liwake vipi halifika eneo hilo January Mpaka Desemba.

 Kwa maajabu ya Mwenyezi Mungu Muumba wa Mbingu na nchi muonekana wa eneo hilo ni kama  limeezekwa kitu cha Kuzuia Mwanga juu yake lakini ukiangalia juu hakuna kitu chochote.

Najiandaa kupanda tena juu ya Mlima huo kwa lengo la kupiga picha vivutia hivyo na kuvitanga kwa lengo la kuwavutia watalii na kuingiza mapato Mkoa wetu wa Morogoro.

Juu ya Milima hiyo nimeshuhudia watu wakilima mazao mbali mbali kando kando ya Mito iliyozaliwa na miti ya Milima hiyo.

Wakati nashuka juu ya Milima hiyo nilisimamisha pikipiki na Kupiga picha Mji wa Morogoro, picha hiyo unaweza kuzani imepigwa na kamera ya Juu ’Drone’ kumbe nimeipiga na kamera yangu ya kawaida nikiwa juu ya Milima hiyo.

Hivyo endelea kuwa jirani na Mtandao huu kushuhudia vivutia hivyo kama nitafanikiwa kupata picha za Ndege na Vyura hao pamoja na eneo la Morning Site

Nikiwa huko huko juu nyakati za jioni nilishuhida Mwezi ukichomoka nyuma ya Milima hiyo jambo ambalo pia lilinishangaza.

[Picha zote na Dunstan Shekidele Morogoro.]

 

 

Drone Camera.

Monday, August 26, 2024

PICHA KALI YA KUFUNGUA WIKI


 

KUMBUKIZI.

Wazee wa Mji Kasoro Bahari[Morogoro] Tajiri Aziz Abood ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini,alinaswa na Kamera za Mtandao huu akiteta jambo na aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini ’I.G.P’ Mstaafu Alhaj Omar Idd Mahita [aliyeketi].

  Picha na Dunstan Shekidele,Morogoro

Thursday, August 22, 2024

KIJIWE NONGWA. UKIONA KAFUTA BANGO UJUMBE UMEFIKA









 


Na Mpekunyuzi wa Mitandao Dunstan Shekidele.
 
Kama kawaida mtumishi wako, kila wiki naweka Bando linalonitembeza kwenye Mitandao ya Kijamii kukusanya jumbe mbali mbali.
Miongoni mwa jumbe hizo ni za Kuelimisha, Kukosoa na Maneno ya hekima yanayotukumbusha kuwa jirani na Mwenyezi MUNGU.
Tukutane Wiki Ijayo kwa mabango Mengine yenye Jumbe Moto Moto.

Wednesday, August 21, 2024

KUMBUKIZI MSANII DIAMOND PLATNUMZ ENZI HIZO.





 


Mwandishi wa habari Dunstan Shekidele ’Mkude Simba’ anaweza kuwa sehemu ya Mafanikio ya Msanii nyota Afrika wa Muziki wa Kizazi Kipya ‘Mwamba’ Nassib Abdul Maarufu Diamond Platnumz Baba Tiffa.

Kwa sehemu kubwa Mwanahabari huyo aliandika habari nyingi za Diamond kwenye Magazeti Pendwa ya Global Publishers tunazohisi zilimuongezea umaarufu.

Pichani Shekidele akimhoji Diamond kwenye Tamasha la Vodacom lililofanyika takribani miaka 10 iliyopita kwenye uwanja wa Jamhuri Morogoro na kuhudhuriwa na Umati mkubwa wawatu kwa kiingilio cha Free Mandela ‘Bure’

Picha hizo kali za Diamond zilizopigwa na Shekidele zilitumika kwenye  Magazeti ya Global na Mitandao ya Kijamii ya kampuni hiyo.

Kwa sasa Diamond Mzaliwa wa Kigoma ni Miongoni mwa wasanii matajiri barani Afrika.

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...