Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Wednesday, August 21, 2024

KUMBUKIZI MSANII DIAMOND PLATNUMZ ENZI HIZO.





 


Mwandishi wa habari Dunstan Shekidele ’Mkude Simba’ anaweza kuwa sehemu ya Mafanikio ya Msanii nyota Afrika wa Muziki wa Kizazi Kipya ‘Mwamba’ Nassib Abdul Maarufu Diamond Platnumz Baba Tiffa.

Kwa sehemu kubwa Mwanahabari huyo aliandika habari nyingi za Diamond kwenye Magazeti Pendwa ya Global Publishers tunazohisi zilimuongezea umaarufu.

Pichani Shekidele akimhoji Diamond kwenye Tamasha la Vodacom lililofanyika takribani miaka 10 iliyopita kwenye uwanja wa Jamhuri Morogoro na kuhudhuriwa na Umati mkubwa wawatu kwa kiingilio cha Free Mandela ‘Bure’

Picha hizo kali za Diamond zilizopigwa na Shekidele zilitumika kwenye  Magazeti ya Global na Mitandao ya Kijamii ya kampuni hiyo.

Kwa sasa Diamond Mzaliwa wa Kigoma ni Miongoni mwa wasanii matajiri barani Afrika.

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...