Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Friday, December 29, 2023

MWANA BIRTHDAY ALIVYOSHEHEREKEA KUMBUKIZI YAKE NA WATOTO YATIMA

 

MWANA BIRTHDAY Dustan Shekidele alivyosheherekea siku yake ya kuzaliwa na watoto wenye ulemavu wa viungo na Vijana yatima. Angalia Clips Video hiyo kwenye kurasa za Facebook za Shekidele mkude simba na ile ya Dustan Shekidele

MATENDO YA HURUMA. MWANA BIRTHDAY ASHEHEREKEA KUMBUKIZI YAKE NA WATOTO YATIMA.


Shekidele akiwarisha keki baadhi ya watoto hao juzi.
Matron Esther akimrisha Keki Shekidele kwa niaba ya Uongozi wa kituo hicho.

Shekidele akiwakabidhi zawadi ya nguo wapendwa wetu hao Jana jioni.


 


             Na Mwandishi Wetu, Morogoro.

MWANANCHI wa kawaida  ‘Mtoto wa Mkulima’Dustan Shekidele Mkazi wa Mji Mpya Mkoani Morogoro juzi alisheherekea siku yake  ya kuzaliwa’Happy Birthday’ na  Watoto wenye ulemavu wa Viungo na Vijana Yatima wanaolelewa katika Kituo cha Mehayo kilichopo Kata ya Mazimbu Manispaa ya Morogoro.

Shekidele ambaye kitaaruma ni Mwandishi wa habari alizaliwa Desemba 25 miaka kadhaa iliyopita siku ambapo pia Mwana wa Mungu Mesia Yesu Kristo’Nabii lssa’  alizaliwa tarehe  hiyo hiyo takribani miaka elf 2 iliyopita huku kumbikizi yake hiyo kupewa jina la  ‘Merry Christmas’.

Katika kusheherekea siku hiyo ndugu, jamaa  na Marafiki walipanga kumuandalia sherehe kabambe ya kumpongeza Shekidele kwa kuongeza mwaka, huku wengine wakimtumia zawadi mbali mbali zikiwemo keki.

Shekidele alikataa ofa hiyo ya kwenda ukumbini kusheherekea siku yake hiyo kwa kuwanywesha watu Pombe na Vyakula vya kifahari ili hali  kuna watoto na vijana yatina wanaohitaji Msaada wetu.

 Kwa kuzingatia hilo kapiga chini ofa hizo za kwenda ukumbini na badala yake kaenda  kituo cha Mehayo kusheherekea siku yake hiyo na Watoto hao.

Mwana Birthday huyo alipofika kwenye kituo hicho alipokelewa kwa upendo mkubwa na watoto hao na moja kwa moja akapelekwa kwenye ukumbi wa kituo hicho na kusheherekea Birthday kwa utukufu wa MUNGU walikata keki na kula kwa pamoja.

Akizungumza na Mtandao huu mara baada ya kukamilika kwa sherehe hiyo Shekidele alisema.

 ”Siku zote siangalii maisha yangu binafsi nangalia maisha ya watu wengine hasa wale wenye uhitaji, kweli ninandugu na Marafiki wengi wenye uwezo ambao tungefanya sherehe kapambe.

Binafsi nimeona hilo halina utukufu mbele za Mungu ningewafurahisha wanadamu kwa kuwapa Pombe na chakula huku nikimchukiza Mungu aliyenipa zawadi ya kuongeza mwaka.

 Hivyo nimeamua kuja hapa Mehayo Centre kusheherekea Birthday yangu na ndugu zangu hao ambao pia wanahitaji faraja na misaada yetu”alisema Shekidele.

Kwa upande wake  Matron wa kituo hicho Esther alisema” Watoto hao wanahitaji faraja ya mara kwa mara kutokana na changamoto wanazopitia hivyo kitendo chako cha kuwakumbuka kwa kusheherekea nao siku yako ya kuzaliwa nifaraja kubwa sana kwao na Mungu atakubariki.

 Kwa muda mrefu hatujaona mtu akija hapa kufanya shehere yotote na watoto hao wewe ndio wa kwanza ubarikiwe sana”alisema.

Baada ya sherehe hiyo kutamatika Shekidele aliwashuhudia baadhi ya watoto hao wakivaa nguo zilizochanika jambo ambalo lilimgusa sana.

Hivyo siku iliyofuata yaani jana Desemba 28 alikusanya nguo nyingi nyumbani kwake na  kwenda  kuwakabidhi. 

Mara baada ya kukamilika kwa zoezi hilo Shekidele aliingia kazini na kuzungumza na Matroni huyo ambapo amefunguka mazito wanayokutana nayo  kwenye kituo hicho moja ya changamoto alizotaja ni baadhi ya watu kuelekeza mitaro ya maji Machafu kwenye kituo hicho jambo ambalo linaweza kuibua magonjwa ya mlipuko kwa watoto hao.

Clip Video za matukio hayo zitaruka hewani hivi punde hivyo endelea kuwa jirani na Mtandao huu muda wote.

                         


 

 

Wednesday, December 27, 2023

KWENYE BITHDAY ZETU TUWAKUMBUKE NA WATOTO YATIMA.




 


Leo Mwana Birthday Dunstan Shekidele amesheherekea kumbukizi ya siku yake ya Kuzaliwa’Happy Barthday’ kwa kula keki na watoto Yatima na wale wenye uhitaji wanao lelewa katika kituo cha Mehayo Kilichopo Kata ya Mazimbu Manispaa ya Morogoro. 
 
Mwandishi huyo aliyezaliwa Desemba 25 Miaka kadhaa iliyopita pamoja na Mesia Yesu Kristo juzi hakufanya sherehe yoyote na badala yake aliamua kufanya sherehe hiyo leo kwenye kituo hicho na kusheherekea siku yake hiyo na watoto hao.
 
Habari kamili na Picha Zaidi za tukio hizo zikiwemo Clip Video zitaruka hewani hivi Punde hivyo endelea kuwa jirani na Mtandao huu muda wote usike alichosema Matroni wakituAo hicho.

Monday, December 25, 2023

KUMBUKIZI YA BIRTHDAY.





TAIFA la watu wa Mungu, familia ya Mungu, duniani kote leo Desemba 25 wanashehereke kusiku ya kuzaliwa Mtoto wao Mesia Yesu Kristo[Nabii lssa] aliyetajwa kwenye vitabu vyote vya dini. 
 
Sherehe hiyoHappy Birthday hiyo imepewa jina la Mery Chrismas ambapo leo dunia yote inasimama kupisha siku hiyo Muhimu. 
 
Katika hali ya kushangaza Mama Mzazi wa Yesu Bikira Maria mara baada ya kuhisia anaujauzito wa Yesu alipasa sauti akisema toka nizaliwe simjui Mwanaume hii Mimba nimeipataje? Malaika wa bwana akamtokea akamwambia usihofu huyo ni Mwana wa Mungu na utazaa hivi karibu. 
 
Baada ya siku kadhaa mbele Desemba 25 Bikira Maria alijifungua Mtoto wa Kiume ndani ya zizi la Ng’ombe na akapewa jina la Yesi Kristo Mokozi wa Ulimwengu. 
 
Mara baada ya Yesu kufanya maajabu makubwa ya kimungu Wapinzania wake walimteka na kumfunga majeredi na mataji ya Miba wakamuua kisha wakampigilia misumari Msalabani.
 
Baadae walimshusha Msalabani na kwenda kumzika kwa mshangazo wawengi baada ya siku tatu yesu alifufuka, kaburi lake lilifunikwa na mawe makubwa lilifunuka kwa miujiza ya Mungu mwana huyo wa Mungu akapaa Mbinguni kwa baba yake. 
 
                        FAMILIA YA SHEKIDELE
 
Familia ya Shekidele kupitia kwa Bi. Tumain Samwel Juma Mshimbula’Mrs Shekidele’Desemba 25 miakaa kadhaa iliyopita Mama huyo alipata ujauzito na kukimbizwa hospital ya Bombo jijini Tanga siku hiyo hiyo ya Desemba 25 alijifungua Mtoto wa kiume aliyepewa jina la Ubatizo Dustan Shekidele.
 
Hivyo familia hiyo ya Shekidele leo Desemba 25 inaungana wa watu wote waliozaliwa siku ya leo akiwemo Mesi wetu Yesi Kristo. Naendelea 
 
Keki yangu leo nakwenda kuikata na kuila na watoto yatima kwenye moja ya vituo vya kulelea watoto hao huku pia nikiwabebea zawadi kadhaa. 
 
Nakushukuru MUNGU kwa kendelea kunipa zawadi ya Uahi sina chakukulipa Zaidi ya kuendeleakutenda mambo mema yanayokupendeza wewe na malaika wako 
 
                      “Happy Birthday to Me” 
 
                                   SHUKRANI. 
 
Nawashukuru wazazi wangu, kaka na dada zangu pamoja na wadogo zangu. 
 
Wangu Tumain na Neema, Waandishi na wapiga Picha wenzangu .Viongozi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuanzia ngazi ya Mtaa mpata taifa, Viongozi wa dini zote mbili,
majirani zangu pamoja na marafiki zangu kwenye mitandao ya Kijamii hakika leo mmenionyesha upendo wa thati lilichelewa kuwasha data ile naingia Facebook nakutana na jumbe zenu za kunitakia afya njema kwenye siku yangu hii muhimu, nasema kutoka chini  ya sakafu ya Moyo 
 
wangu Mungu awabariki wote walionipongeza sms zenu  sitazifuta kwenye eneo hilo zitabaki kama kumbukumbu kwenye maisha yangu.



 

Thursday, December 21, 2023

MTUMISHI WA MUNGU ATOA UFAFANUZI PETE YA UCHUMBA ALIYOFISHWA HAYATI NOERA.

Mwinjilisti Nyange akiongoza moja ya lbada kwenye usharika huo.
Hayati Noela enzi za Uhai wake na Picha hii ndio inasoma kwenye Profaili la Mtumishi Nyange.

                                   Mwinjilisti Nyange


   Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

MARA baada ya Mwana kwaya ‘Soro Rist’wa kwaya ya Sifuni, hayati Rehema Chao’ Maarufu Noela’ kufariki dunia kwa ajari akiwa njiani kuelekea Jijini Arusha Kufunga ndoa na Mchumba’ke Aman Moleni, maswali mengi yaliibua,Kwamba Pete hiyo ya Uchumba‘Engagement’amezikwa nayo au amevuliwa na kurejeshewa kwa Mchumba’ke huyo aliyemfisha siku chache kabla ya kufunga ndoa Jumamosi ya Desemba 2.

Kufuatia Maswali hayo Mwandishi wa Mtandao huu alitinga kanisa la Kiinjiri la Kiluteheri Tanzania’KKKT’ Usharika wa Mji Mpya na kuzungumza na Mtumishi wa Mungu Mwinjilisti Godfrey Nyange ambaye alikuwa  mtu wa karibu sana na hayati Noera.

Kwa kulitambua hilo Mara baada ya kutinga kanisani hapo  Juzi mchana,nje ya Mlango mkuu wa kuingia kanisani Mwandishi  aliwashuhudia Mchungaji Dunia anayechunga Kondoo wa Usharika wa Mji Mpya akipiga Story na Mchungaji Tengeneza anayeongoza waumini wa KKKT Usharika wa Kolla.

Mara baada ya kumuona Mwandishi huyo Mchungaji Tengeneza alimtania akisema” Shekidele Jumapili sijakuona  Kanisani ulisari wapi”?

Mwandishi alimjibu “ Siunajua huu ni Mwezi wa Maokoto nilisari KKKT Usharika wa Mji Mwema kwa mchungaji Simba  kulikuwa na Kipa lmara;”

Baada ya maongezi hayo  Mtandao huu aliwaacha Wachungaji hao na kuingia Ofisi ya Mwinjilisti Nyange na kuzungumza naye juu ya kifo cha Noela.

lfahamike Mwandishi huyo anaye sari kanisani hapo aliamua kumruka Mchumbani Dunia na kwenda kuzungumza naMsaidizi wake,hii ni kwa sababu ya ukaribu wa Mwinjilisti huyo na hayati Noela.

Kwa kudokeze tu siku ya harusi ya Mwinjilisiti Nyange iliyofungwa takribani miaka 2 iliyopita hayati Noela alikuwa mstati wa mbele kwenye harusi hiyo iliyofanyika ukumbi wa Tanzanate Msamvu.

Mara baada ya Noera kufariki dunia Novembar 28 na kuzikwa Desemba 2, Mwandishi wa habari hizi alichungulia  Profari la Mtandao wa WhatSap  na kushuhudia  Mwinjilisti Nyange aliweka Picha ya Noela.

Hadi juzi wakati Mwandishi wa habari hizi anachati na Mwinjilisiti huyo kupitia Mtandao huu wa Whatsap alishuhudia Picha ya Noera ikiendelea kusalia eneo hilo.

Alipowasili ndani ya Ofisi ya Mwinjilisti Mahojiano yalikuwa hivi.

Mwandishi. Habari Mtumishi wa Mungu na Poleni kwa msiba Mzito.

Mwinjilisti. Asante Msiba ni wetu sote hata wewe pia pole kwa kuondokewa na Mwana kwaya mwenzenu.

Mwandishi.Asante najua fika wewe ni mtu wakaribu sana na hayati Noela ndio maana nimemruka Mchungaji hapo Nje nimekuja kuongea na wewe nikiamini nitapata madini mengi juu ya kifo hicho cha Mpendwa wetu  aliyezimika kama Mshumaa.

Mwinjilisti. Ni kweli Shekidele Noela alikuwa ni mtu wangu wa karibu sana na siku anaanza safari nilichati naye akinifahamisha kwamba ameniombea Lifti kwenye gari la Mke wa Mchungaji wa KKKT Usharika wa Bungo nielekea kwenye harusi yake.

Baada ya kuchati naye hiyo asubuhi nilikuja hapa ofisini nilipoingia tu nilipata homa la ghafra nikaomba ruhusa nikaenda kulala nyumbani, unajua mtu wako wa karibu akipata tatizo nawe kuna ishara unaziona.

Majira ya jioni napigiwa simu nikielezwa  Noela amefariki dunia homa lilipona muda huo huo nikampigia mchungaji kuthibitisha akaniambia ni kweli hayo uliyosikia Noela natunaye tena amepata ajali .

Mwandishi. Je ulifanikwa kwenda kumzika na amezikwa lini na wapi?

Mwinjilisti. Mungu alinipa kibari cha kwenda kumzika Noela, tumemzika Desemba 2 Kijijini Kwao Moshi, siku tuliomzika ndio ilikuwa siku ya harusi yake.

Mwandishi. Tunajua Kabla ya harusi alivishwa pete ya Uchumba na Mchumba’ke je amezikwa na Pete hiyo au amevuliwa na kurejeshwa kwa mchumba’ke?  kiimani jambo hilo likoje?

Mwinjilisiti. Lile lilikuwa agano la Noela na Mchumba’ke Aman Molen sasa kwa kuwa Noela amefariki agano hilo limevunjika, Kavuliwa Pete imerejeshwa kwa aliyemvisha.

 Kiimani angezikwa nayo ingekuwa na maana kwamba agano hilo halijavunjika na huyu Mchumba’ke asingepata nafasi ya kuchumbia tena kwa kuwa agano lake la awari hajalivunja.

Ifahamike Pete inamaana kubwa sana kwenye maagano ndio maana kabla ya Maharusi au wachumba kuvishana pete  ni lazima zibarikiwe na Mtumishi wa Mungu.

Mwandishi Asante Mtumishi kwa ushirikiano wako.

Mwinjilisti  Asante na wewe kwa kuja   

 

 

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...