Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Sunday, October 15, 2023

ACHENI MUNGU AITWE MUNGU. UCHAFU UNAOFANYWA HAPA DUNIANI, NINGEKUWA MUNGU NISINGEVUMILIA.

Mwandishi wa Mtandao huu Dunstan Shekidele akizungumza na Mtumishi wa Mungu Kiongozi Mkuu  wa KKKT Dayosisi ya Morogoro  Askofu Jacob Ole Mameo nje ya kanisa la KKKT Usharika wa Mji Mpya
 


Na Mtumishi Dunstan Shekidele,Morogoro.

 AMANI ya Mwenyezi Mungu na iwe juu yenu, ama baada ya salamu moja kwa moja tuingia kwenye ujumbe wetu wa neno la Mungu leo Jumapili ya Octobar 15.

Leo sitanukuu mstali wowote katika biblia bali nitatema nyongo iliyojaa ndani ya moyo wangu kwa dhambi zinazoendelea kufanywa hapa duniani.

Ama kwa hakika Mungu ni Mvumilivu sana hakika kama mimi Dustan Peter Shekidele’D.P.S’ ningekuwa Mungu nisingeweza kuvumilia haya ninayoyaona na kuyasikia hapa duniani.

Utasikia na kuona Mwanaume anajiuza’Shoga’ Mimi ningekuwa Mungu nisingelivumilia hili.

Utamuona Mwanaume baba mtu mzima amepima na kubainika kuwa na virusi vya HIV ‘UKIMWI’anameza dawa za kurefusha Maisha kila siku.

Baba huyo mwenye nyumba anayejijua  anagonjwa hilo la hatari ‘Taa ya oil inawake kwenye Bashibord lake’ anamrubuni mfanyakazi wake huyo ’House Girl’ anatembea naye na kumuambukiza maradhi hayo yasio na tiba kwa makusudi akitumia ufukara wa bint huyo  tegemo kwa wazazi wake waishio Kijijini.

Mimi ningekuwa Mungu mwanaume huyo ningemuangamiza kabla  hajafanya dhambi hiyo.

Tunasikia na kuona Mwanadamu anashonwa tumbo lake kama gunia anasafirisha Madaya ya kule ili awe tajiri, Shekidele ningekuwa Mungu nisingevumilia hili.

Juzi nimesikia kwenye vyombo vya habari Mama kawapeleka mabinti zake Mapacha kwa Mganga wa kienyeji kuwakuza matiti  yakue haraka  ili waooze kwa wanaume apate mahali.

 Masikini ya Mungu  mabinti hao wadogo wasio na hatia baada ya kunywa dawa hiyo kwa amri ya Mama yao wote wawili wamefariki duania, mimi ningekuwa Mungu nisingekubali hili.

Pia unasikia kwenye vyombo vya habari mtumishi wa serikali anayelipwa mshahara mnono kwa kodi za walala hoi.

Huyo huyo mtumishi utasikia  kala pesa za Ujenzi wa Zahanati ya kijiji zilizotolewa na serikali .

Baada ya mtumishi huyo kutafuna Pesa hizo za ujenzi wa Zahanati,siku chache mbele unasikia Mama Mjamzito Mlala hoi amejifungua njiani na kupoteza maisha baada ya kukosa huduma ya Zahanati kwenye kijiji hicho.

lnauma sana mimi ningekuwa Mungu nisingemvumilia mtumishi huyo wa Serikali aliyepewa dhamana na Rais kusimamia kimanilifu Miradi ya wananchi.

Baada ya kutafakari kwa kina mambo hayo machafu nimebaini  Mungu anakusudi  jema kwetu,anatupenda watu wake licha ya kumkosea ama kwa kujua ama kwa kutokujua anaendelea kutupa nafasi ya kujitasmina kwa lengo la kujirekebisha na kutubu makosa yetu kabla ya kuingia kaburini ambako huko hatutapata tena nafasi ya kuziungama dhambi zetu.

 So Wenye masikio na wasikie wasio na masikio[……]

                   


No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...