Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Wednesday, December 29, 2021

HAPPY BIRTHDY TO YOU KIONGOIZI




 

Happy Birthday Mirs Flan.
"Nimemtuma Njiwa Mweupe kama roho yako akuletee zawadi ya Ua Jekundu".

WAMACHINGA MORO SIKIO LA KUFA?


 Wamachinga wakipiga shoo bila wasi wasi wowote barabara ya Makongoro iliyopo katikati ya Mji wa Morogoro, Vionavyoonekana Mbele ni Vibanda vipya vya Wamachinga.

                        

                            Na Dunstan Shekidele,Morogoro. 

WAHENGA wana msemo wao unaosema’Sikio la Kufa halisikia dawa.’ Licha ya Serikali ya ya Mkoa wa Morogoro kwa kushirikiana na Uongozi wa  Wilaya ya Morogoro Mjini ikiongozwa na Mpambanaji kipenzi cha wana Morogoro Mkuu wa Wilaya Mh Albeth Msando.

Kuwaondoa barabarani kistaarabu Wafanyabiashara dogo dogo’Wamachinga’ na kuwahamishia kwenye Vibanda vya kisasa vilivyojengwa nje ya Soko Kuu la Morogoro kwa nguvu binafsi za Mkuu wa Wilaya.

Chaajabu  wiki iliyopita Mtandao huu uliwashuhudia baadhi ya wamachinga  wamerejea tena barabarani  wakipanga bidhaa zao kwenye barabara zilizopo jirani kabisa na Vibanda hivyo.

 

Baadhi ya wananchi waliohojiwa na Mtandao huu walitema nyongo zao wakisema.

 

”Hawa wamachingana ni Sikio la Kufa licha ya serikali ya Mkoa na wilaya kuwatoa juani walipokuwa wakifanya biashara barabarani na kuwatengenezea Vibanda Vizuri baadhi yao wamegawa biashara zao mara mbili nyingine wamebakiza kwenye vibanda wakiendelea kufanya biashara na nyingine wamekuja kupanga huku barabarani eneo la watembea kwa miguu.

 

Baadhi ya waswahiri hata uwafanyie ustaarabu kiasi gani hawalidhiki mpaka washurutishwe kibabe hawa wamachingana wamezoea kufukuzwa msobe msobe na Mgambo huku wakitandikwa vilungu na kunyang’anywa bidhaa zao ndio Maisha waliyozoea hawakuzoe maisha haya ya kistaarabu”alisema Hamis Juma.

 

Miezi kadhaa iliyopita Rais Samia Suluhu Hassan alimtumbua Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mh Bakari Msulwa na Mkurugenzi wa  Manispaa ya Morogoro Bi, Sheila Lukuba, baada ya Mama Samia kuona Clip Video ya Magambo wa Manispaa ya Morogoro wakiwatandika Vilugu Wamachinga waliofanya biashara barabarani eneo la lslam’Maarufu Ghorofa Chafu’ kisha Mgambo hao kumwaga Vyakula vya Mama N’itiliye. 

Clip Video hiyo ilipigwa na Mwandishi wa habari Mkoani Morogoro anayepiga Kazi TBC Taifa jina nalihifadhi kwa sababu za kiuwanaume.

 

Baada ya Viongozi hao kutumbuliwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mh Martin Shigella alipiga Marufuku Mgambo wote wa Wilaya zote za Mkoa wa Morogoro kufanya Oparesheni ya kuwaondoa Wamachinga barabarani.

                   


Monday, December 27, 2021

KUMBUZI YA MIAKA 2 YA KIFO CHA BIBI ALIYEAGA DUNIA AKIWA NA UMRI WA MIAKA 103

                       Bibi Kete Abdallah[103] enzi za Uhai wake
,,,,Bibi Kete akiwa na Mwanaye wa kwanza Tumain Samwel Juma 'Mrs Shekidele'Kulia' kushoto ni Mjukuu wake wa kwanza, William Shekidele ambaye ni Mtoto wa kwanza wa Tumaini.

William anaishi Kigamboni jijini Dar ana watoto 5 na wajukuu 4.

Mwandishi wa Mtandao huu kiulia akipa zawadi ya Rozari Mama yake Mzazi Bi Tumaini Shekidele, ambaye ni Mtoto wa 5 kwenye uzao wa Tumaini aliyejaliwa kuzaa watoto 7. 

Wakwanza William, Wapili Elice'Mrs Riwa' wa tatu Richard, wa nne Rehema'Mrs Magessa. watano Dunstan, 6 Elisante na 7 ni Upendo'Mrs Muchunguzi.

Vicky David Juma 'Mrs Mwambola' akimsaidia bibi yake kukata Keki siku ya Birthday yake ya kutimiza miaka 101 mwaka 2017. sherehe hizi zilifanyika nyumbani kwa bibi Gongolamboto Mombasa Mtaa wa Moshi Baa jijini Dar
...Baada ya kukata keti hiyo akimrisha Mwandishi wa Mtandao huu
Bi Neema Samwel Juma 'Mrs Mulokozi' ambaye ni Mtoto wa tatu wa bibi Kette akimuaga Mpendwa Mama yake aliyefariki dunia Desemba 22 akiwa usingizini akiwa mzima wa afya
Baadhi ya Majirani wakimpa mkono wa Pole Bi Neema ambaye ndiye aliyekuwa akiishi na Mama yake huyo Mtaa wa Moshi Baa Dar
,,, Baada ya lbada fupi ya kumuombea marehemu iliyofanyika ndani ya hospital ya Amana jijini Dar ambapo marehemu baada ya kufariki dunia mwili wake ulihifadhiwa hapo kwa siku 3 kabla ya kusafirishwa kuelekea Kijijini kwake Mlalo Wilaya ya Lushoto Mkoani Tanga kumpunzisha kwenye nyumba yake ya Milele.
....Jeneza lililobeba mwili wa mpendwa bibi yetu likiingizwa kwenye gari tayari kwa safari ya kuelekea Lushoto
... Msafara huo ukijianda akuondoka hospital ya Amana
... Msafari huo ukikatiza mitaa ya jiji la Dar kupitia Bagamoyo Road kuelekea Lushoto ambapo Mwandishi wa Mtandao huu aliyeketi siti ya Mbele ya Coaster ya Pili alikuwa bize kupiga Picha matukio yote yakiwemo ya barabarani kutoka Dar Mpka Lushoto
....Msafara huo umetinga daraja la Ruvu Mkoa wa Pwani  barabara kuu ya Chalinze Segera
.... Msafara huo umefika Tarafa ya Mlalo Wilaya ya Lushoro stendi ya Mkongoroni
....David Samwel Juma[aliyeketi ndani ya gari] ambaye ni mtoto wa Pili wa Marehemu Bibi Kette aliyesafiri kutoa Marekani anakoishi  Mpaka Tanga kumzika Mpendwa  Mama yake akizungumza na Mjomba wake William Shekidele kulini ni lkunda Riwa Mtoto wa kwanza wa Elice Shekidele.



Kanisa Kuu la KKKT Usharika wa Mlalom Picha ya hapo juu ni David Juma akiwa nje ya ghorofa la Marehemu baba yake Mzee Samwel Juma mara baada ya Mwili wa Marehemu bibi kette
Mwandishi wa Mtandao huu kushoto kwenye nguo nyekundu, William Shekidele[Kati] na Elisante Shekidele kwa pamoja wakiwa kwenye kaburi la Mpendwa baba yao Mzee Peter Shekidele aliyezikwa kwenye makaburi yaliyopo nje ya Kanisa la KKKT Usharika wa Mlalo.
...David Juma na Mkewe wakitoa heshima za mwisho kwa Mpendwa mama yao mara baada ya lbada ya kumuombea Marehemu kukamilika kwenye Usharika huo wa Mlalo ambapo enzi za Uhai wake Marehemu Bibi Kette alikuwa Mwimbaji wa Kwaya kuuu ya Usharika huo kabla ya kuhamia jijini Dar kwa watoto zake
Elisante Shekidele na Willia Shekidele wakimbembeleza Mjomba wao David Juma aliyekuwa akimlilia Mpendwa Mama yake
Neema Juma Mrs Mulokozi akitoa heshima za mwili kwa Mpendwa Mama yake Kipenzi, Bi Neema ambaye ni Mstaafu wa hospital ya Hushen Road jijini Dar ndiye aliyekuwa akiishia na Mpendwa Mama yake
,,,,Mwili wa Mpendwa wetu ukitolewa ndani ya kanisa la KKKT Usharika wa Mlalo Lushoto
...ukielekea nyumbani kwake kwa Maandamano yaliyoongozwa na Kwaya ya Matalumbeta
          Mpendwa bibi kette alizikwa nje ya nyumba yake

David Juma akipanda msibala kwenye kaburi la Mpendwa Mama yake
               David Juma na mkewe wakiweka shada la Maua
Daviid Juma na mkewe wakipiga Picha mara baada ya kuweka shada la Maua kwenye kaburi la Mama yao
                   Neema Mulokozi akiweka shada la Maua
Kitukuu cha kwanza cha Bibi Kette lkunda Riwa akiweka shada la Maua kwenye kaburi la Mama yake Mkubwa, lkunda ana watoto 2 kama yeye ana mwita bibi Mama Mkubwa sijui watoto zake wanamwitaje bibi Kette wajuzi wa mambo hayo tujuzeni tafadhari
....Baada ya kumpunzisha Mpendwa bibi Kette waombolezaji wakirejea jijini Dar wakiwa katikatika ya Msutu wa Milima ya Usambara wakitokea Lushoto Mjini kuelekea Mombo


 Msafara huo umetua Mombo wakanunua chakula na kuendelea na Safari Picha zote na Dunstana Shekidele.

Friday, December 24, 2021

HAPPY BIRTHDAY YESU, HAPPY BIRTHDAT SHEKIDELE

Picha ya Mfano Yesu akizaliwa katika Zizi la Ng'ombe Decemba 25 miaka kadhaa iliyopita

            Mwandishi wa Mtandao huu Dunstan Shekidele

HAPPY BIRTHDAY TO ME.

Leo Desemba 25 Wakristo duniani kote wanasheherekea siku kuu ya kuzaliwa Mesiha Yesu Kristo ambaye kwa somo la Mungu kwetu aliluhusu Mtumue huyo aliyekuwa kuukomboa Ulimwengu azaliwe katika zizi la kufungia Ng’ombe kama picha ya mfano inavyoonyesha Mtoto Yesu akizaliwa katika Zizi hilo la Ng’ombe.

Leo Pia Decemba 25 ni kukumbizi ya Kuzaliwa kwa Mwandishi wa Mtandao huu ambaye yeye hakuzaliwa Katika Zizi la Ng’ombe amezaliwa katika Hospital ya Rufaa ya Bombo iliyopo kando kando ya Bahati ya Hindi Jijini Tanga.

 

              SHUKRAN.

Kipekee na Msukulu Mungu kwa kuendelea kunipa zawadi ya Uhai na leo hii kwa Neema zake ameniongezea Mwaka Mwingine.

Pili nawashukuru wazazi wangu Marehemu Baba yangu Mzee Peter Shekidele Mungu amepe punziko   la Aman.

Na Mama yangu Kipenzi Tumaini Shekidele anayeendelea na Matibabu jijini Dar na Muombea kwa Mungu apone upesi.

Tatu nawashukuru Viongozi wote wa dini zote kwa kuendelea kutupa mahubiri na Mawaidha yenye lengo la kutuweka karibu na Mwenyezi Mungu.

 

 Nne nawashukuru Viongozi wote wa Serikali ya Jamhuri ya Mungano wa Tanzania kwa kuenzi na kudumia Amani inayopelekea mimi na wananchi wengine kuishi kwa amani.  

Tano Nawashukuru ndugu zangu Marafiki zangu na wadau wa Mitandao yangu ya Kijamii hasa Facebook.                        MSAMAHA.

Kupitia siku yangu hii ya kuzaliwa naomba Msahama wa dhati kutoka kwenye sakafu ya Moyo wangu kwa mtu yoyote niliyemkosea kwa kujua au kwa kutoa kujua naomba anisamehe kwani mimi ni kiumbe dhaifu si Malaika.  

 

Pia kupita siku hii nimewasamehe kwa dhati watu wote walionikosema kwa namna yoyote ile.

Happy Birthday Yesu Kristo, Happy Birthday Dunstan Shekidele, Happy Birthday watu wote waliozaliwa siku kama ya leo Desemba 25.

SIKU KUU NJE,MA


 

Thursday, December 23, 2021

KERO YA MTAA. WANAOPIGA PINI MAGARI WALALAMIKIWA NA UPENDELEO.

Gari la kwanza kupigwa Pini saa 5 na dakika 32 angalia kwenye Picha saa na na tarehe.

Mita kama 30 mbele takribani dakika 3 mbele gari hili la serikali liliegesha sehemu isiyo ruhusiwa kisheria, wakamataji walipouna ni la serikali walilipita hawakulikamata.

Dakika 4 mbele baada ya kuliacha gari la serikali walimekamata gari hili huku dereba akiw andani ya gari kama anavyoonekana Pichani akiwaomba msaada wakamataji hao bila mafanikio

 


Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

Wiki iliyopita baadhi ya madereva wa Magari binafsi Mkoani hapa, walitoa kero yao kwa Mtandao huu wakilalamikia kitengo kilichopewa jukumu la kusimamia alama za barabarani kwa kuyakamata na kuyafunga Nyororo Magari yote yanayokiuka alama za Usalama barabarani ikiwemo kuegesha Magari maeneo yasiyoruhusiwa’Long Paking’

 

 Lalamiko kuu la Madereva hao wanadai wahusika wanaufanya kazi hiyo kwa Upendelea kwa kuyakamata magari ya watu binafsi huku yale ya serikali yanayovunja sheria wakiogopa kuyakamata.

Baada ya kupokea Malalamiko hayo Jana Mwandishi wa Mtandao huu aliingia kazi kufanya uchunguzi wa malalamiko hayo kama yana ukweli au la.

 

Majira ya Mchana Shushu wa Mtandao huu alitinga katikati ya Mji wa Morogoro akawaona Wakamataji hao wakiwa kwenye Bajaj yenye rangi nyeusi, Shushu  akiwa kwenye Pikipiki yake ya Mwendo Kasi akaifuatilia Bajaj hiyo kwa nyuma kila ilipokatiza.

 

Mara paa Bajaj hiyo ikasimama barabara ya Madaraka jirani na Msikini wa wahindi ‘Jamati’wakashuka na kuipiga Cheni gari iliyoegeshwa  eneo lisiloruhusiwa.

 

Kweli dereva huyo alistahili kukamatwa ambapo licha ya uwepo wa alama ya kuzuia kuegesha gari eneo hilo  alikaidi na kupack gari lake na kuondoka zake kufanya shoping za X Mas Madukani.

 

Uwepo wa gari hilo eneo hilo kulisababisha usumbufu kwa madereva wengine sambamba na foleni kwenye barabara hiyo yenye msongamano mkubwa wa magari hasa nyakati za jioni.

 

 Kwa vile muhusika hakuwepo kwenye gari hilo  Mabaunsa hao walilipiga pini kasha wakaondoka zao,Shushu wa Mtandao huu baada ya kupiga Picha gari hilo fasta akapiga gia Chombo yake na kuendelea na uchunguzi wake  kwa kuendelea kukifuatilia Kibajaj hicho.

 

Chaajabu mbele kidogo takribani mita 50  toka lilipofungwa gari la kwanza kulikuwa na gari la Serikali ambalo pia limeegeshwa eneo lisiloruhusiwa bila kujua kama wanafuatiliwa na Shushu Wakamataji hao walipunguza mwendo  Kibajaj chao wakalitazama gari hilo baada ya kusoma namba na kubaini ni gari la serikali waliliacha wakaondoka zao.

 

Mita 30 tena wakakuta gari binafsi limeegeshwa eneo lisiloruhusiwa huku dereva wa gari hilo akiwa ndani ya gari amewasha End keta Double Azad wakalipiga pini.

 

Mzee aliyekuwa ndani ya gari hilo kwa hekima aliomba Msamaha huku akijitetea kwamba aliegesha mbele ya duka lake kwa dakika chache ashushe mzigo,  Mabaunsa hao hawakumsikiliza badala yake waliendelea kulipiga cheni.

 

Baada ya ombi lake kukataliwa Mzee huyo alishuka kwenye gari akazama kwenye duka  lake hilo la Vifaa vya Shule na Maofisini’Stationery’ akavuta droo akakunya elfu 50 akalipa Cash faini hiyo wakamfungulia.

 

Mwandishi wa Mtandao huu aliwafuata Mabaunsa hao na kuwaeleza “Makamanda Mambo Vipi hongereni mnafanya kazi nzuri baadhi ya madereva walikuwa wakiegesha hovyo magari utakuta kulia mwa barabara kuna gari zimeegeshwa, kushoto mwa barabara hivyo hivyo, hali hiyo husababisha folezi zisizo za lazima kwa watumiaji wengine wa barabara.

 

Mimi kama Mwandishi wa habari nilipokea malalamiko kutoka kwa wananchi kwamba kazi yenu mnaifanya kwa upendeleo kwa kukamata magari ya watu  binafsi huku yale ya serikali mkiyaacha, mfano hapo nyuma mita kama 30  kuna gari la serikali  mmeliona hamkulifunga mpaka sasa naliona lile pale bado lipo tena kwenye kibao cha No Paking”.

 

Walijibu kwa Mkato ‘Kanunue cheni ukalifunge wewe”baada ya majibu hayo ya shombo wakapiga gia Kibajaj chao wakaondoka zao.

 

Mwandishi wa Mtandao huu aliingia kwenye Stationery na kuzungumza na Mzee huyo ambaye alijitambulisha kwa jina la  Buruhani Manyisa Maarufu Mzee Manyisa.

 

“ Yaani nimesimama kwa dakika kama 1 au 2 nikiwa ndani ya gari kama ulivyonipiga Picha nimewaita Vijana wangu wanipokee hili boksi la karatasi mara na stuka gari langu linafungwa, licha ya kujitetea sana  Vijana wale hawakunielewa.

 

Nilikata kwenda kwenye Kibajaj chao kuzungumza nao nikawaita hapa mbele za watu nikalipa cash faini elf 50 nika changia mapato ya serikali yangu”alisema Mzee Manyisa ambaye ni Mstaafu wa Jeshi la wananchi wa Tanzania’JWTZ’.

 Kufikia hapa shushua wa Mtandao huu alikamilisha kazi aliyotumwa na wananchi na imeifanya kazi hii kwa welezi kwa takribani dakika 20 tu na kubaini Magugu na Ngano Mchele na Pumba Maji na Mafuta.

Angalia Picha za magari matatu tofauti mawili ya watu binafsi yamepigwa Pini na Moja la serikali limeachwa huru

 

lli kudhibitsha hili na kuondoa makando kando Mwandishi wa Mtandao huu aliamua kuseti kamera yake Tarehe na Saa kama inavyoonekana inavyosomeka kwenye Picha hizo.

 

Hivi karibuni baada ya magari ya serikali kudaiwa kuendeshwa kwa Mwendokasi na kusababaisha ajari na kuuwa watumishi wengi wa serikali Viongozi mbali mbali wakiwemo Mawaziri walikemea jambo hilo huku wakiwaagiza Askali wa kikosi cha Usalama barabarani kuwakamata madereva wa magari ya serikali wanaovunja sheria.

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...