Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Wednesday, December 29, 2021

WAMACHINGA MORO SIKIO LA KUFA?


 Wamachinga wakipiga shoo bila wasi wasi wowote barabara ya Makongoro iliyopo katikati ya Mji wa Morogoro, Vionavyoonekana Mbele ni Vibanda vipya vya Wamachinga.

                        

                            Na Dunstan Shekidele,Morogoro. 

WAHENGA wana msemo wao unaosema’Sikio la Kufa halisikia dawa.’ Licha ya Serikali ya ya Mkoa wa Morogoro kwa kushirikiana na Uongozi wa  Wilaya ya Morogoro Mjini ikiongozwa na Mpambanaji kipenzi cha wana Morogoro Mkuu wa Wilaya Mh Albeth Msando.

Kuwaondoa barabarani kistaarabu Wafanyabiashara dogo dogo’Wamachinga’ na kuwahamishia kwenye Vibanda vya kisasa vilivyojengwa nje ya Soko Kuu la Morogoro kwa nguvu binafsi za Mkuu wa Wilaya.

Chaajabu  wiki iliyopita Mtandao huu uliwashuhudia baadhi ya wamachinga  wamerejea tena barabarani  wakipanga bidhaa zao kwenye barabara zilizopo jirani kabisa na Vibanda hivyo.

 

Baadhi ya wananchi waliohojiwa na Mtandao huu walitema nyongo zao wakisema.

 

”Hawa wamachingana ni Sikio la Kufa licha ya serikali ya Mkoa na wilaya kuwatoa juani walipokuwa wakifanya biashara barabarani na kuwatengenezea Vibanda Vizuri baadhi yao wamegawa biashara zao mara mbili nyingine wamebakiza kwenye vibanda wakiendelea kufanya biashara na nyingine wamekuja kupanga huku barabarani eneo la watembea kwa miguu.

 

Baadhi ya waswahiri hata uwafanyie ustaarabu kiasi gani hawalidhiki mpaka washurutishwe kibabe hawa wamachingana wamezoea kufukuzwa msobe msobe na Mgambo huku wakitandikwa vilungu na kunyang’anywa bidhaa zao ndio Maisha waliyozoea hawakuzoe maisha haya ya kistaarabu”alisema Hamis Juma.

 

Miezi kadhaa iliyopita Rais Samia Suluhu Hassan alimtumbua Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mh Bakari Msulwa na Mkurugenzi wa  Manispaa ya Morogoro Bi, Sheila Lukuba, baada ya Mama Samia kuona Clip Video ya Magambo wa Manispaa ya Morogoro wakiwatandika Vilugu Wamachinga waliofanya biashara barabarani eneo la lslam’Maarufu Ghorofa Chafu’ kisha Mgambo hao kumwaga Vyakula vya Mama N’itiliye. 

Clip Video hiyo ilipigwa na Mwandishi wa habari Mkoani Morogoro anayepiga Kazi TBC Taifa jina nalihifadhi kwa sababu za kiuwanaume.

 

Baada ya Viongozi hao kutumbuliwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mh Martin Shigella alipiga Marufuku Mgambo wote wa Wilaya zote za Mkoa wa Morogoro kufanya Oparesheni ya kuwaondoa Wamachinga barabarani.

                   


No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...