Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Monday, August 30, 2021

UNAPOKATISHA UHAI WA MTU AU KIUMBE CHOCHOTE, WAFIKILIE PIA WATU WANAOMTEGEMEA.


 


Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

 WADAU wa Mtandao wa shekidele nawasalimu katika Jina la Jamhuri ya Mungano Tanzania.

 

Ama baada ya salamu tumekutana tena kwenye ukurasa wetu Pendwa wa Makala za Kijamii,Michezo na Mapenzi.

 

Mada  ya leo ni ya kijamii ishu ikiwa ni Ukatili. Na dhuruma

 

Hivyo ungana nami na bila kupoteza muda nakudadavulia Mada hiyo.

 

UNAPOTOA Uhai wa mtu kwa namna yoyote ile kwa uonezi iwe kumpiga risasi, kumuua kwa kumpiga ngumu au kumuua kwa nguvu za giza wafikilie pia watu viumbe wanaomtegemea miongoni mwa viumbe hivyo wako watoto wake wakiwemo wachanga, wapo wazazi wake pamoja na ndugu na jamaa wanaomtegemea.

Pia  kumdhurumu mjakazi wako  Jasho lake hapa namaanisha ujira wake fikiria mara mbili watu wanaomtegemea.

 

Hii si kwa binadamu tu hata kwa wanyama na Ndege, mfano picha hii Mtu amemua huyu ndege ili hali alikwenda kusaka chakula cha Makinda’Watoto wake’ inauma sana watoto wanalia njaa huku mama yao emeuwawa kikatia jirani na kiota chake kilichojaa watoto wake.

 

Ukati kama huu si kwa mauaji tu hata unapomdhumu mtu haki yake Pesa na n.k huo nao ni ukatili kama ukati  huo wa mauaji, katika kudhibitisha hili Mungu kupitia vitabu vya dini alitoa onyo kwenye tukio hili la dhuruma au kucheleweza malipo ya Mjakazi wako akisema

 

”Ukimpa Mjakazi wako kibarua cha kulima Mraba  akimaliza kazi  kwa usahihi kabla jasho halijakauka mwilini mwake mlipe ujira wake”

 

Zama hizi baadhi ya waajiri wanachuma dhambi kwa kukiuka agizo hili la Mungu tunapozungumzia waajiri ni pamoja na wewe mama au baba ulioajiri dada wa kazi’House Girl’ au kaka wa kazi’House Boy’.

 Mwisho wa mwezi ukifika mlipe ujira  wake na usimletee rongo rongo kwa sababu anakura ugari wako na kulala kwenye nyumba yako hayo hayahusiani na ujira wake.

 

Mwandishi wa Makala hii anajua ugumu wa maisha pia anajua wafanyakazi pia ni binadam wanauelewa hivyo kama ikitokea bosi umepata matatizo mwezi husika kayumba kiuchumia, kuugua, nk ni vyema ukazungumza na mfanyakazi wako mapema ukimuomba kusogeza mbele malipo yake.

 

 Kama akilidhia naamini ataridhia kwa vile stretion husika ameishuhudia atakubali ombi lako, akikubali namini hapo nakuna tatizo ila dhambi itakupata ukitumia ubabe wa ubosi wako kumdhurumu mfanyakazi wako.

 

Kwa vile anashida na bado anahitaji hiyo kazi na hana sehemu nyingine ya kupata kazi atakubali shigo upande huku kila siku akinung’unika moyoni, naamini naye kuna watu kawakopa kwa ahadi kwamba mwisho wa mwezi akipokea haki yake atalipa hayo madeni hivyo kitendo cha bosi kutomlipa kwa wakati au kumdhurumu kabisa unamsababishi matatizo  itaradhimika achume dhambi kuwadanganya wanaomdai naamini dhambi hiyo haipati yeye utaipata wewe bosi au mdaiwa.

 

Kwa leo naishia hapa tukutane wiki ijayo kwa Makala Moto moto ya Mahusiano, kwa ushauri au Maoni wasiliana nami kwa namba 0715 20 90 73.

Sunday, August 29, 2021

KUELEKEA KILELE CHA YANGA DAY, MASHABIKI SIMBA WATUPA DONGO.

                      YANGA Daya Simba watupa dongo

 


                          Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

JANA ni kilele cha Siku ya Mwananchi’Yanga Day’ambapo takribani wiki nzima wananchana na wapenzi wa timu hiyo kote nchini waliadhimisha wiki hiyo ya Mwananchi kwa kufanya shughuli za kijamii ikiwemo kutoa misaada kwa watu wenye uhitaji.

 

Kilele cha siku hiyo ya Mwananchi kiliadhimishwa jana kwa wanachama na mashabiki wa timu hiyo kuzajana uwanja wa Mkapa Temeke jijini Dar.

 

Kwenye Tamasha hilo lilipambana na burudani mbali mbali wakiwemo msanii Mkongwe kutoka DR Congo  Papaa Koffi Olomide na Msanii nyota nchini wa kike Nandy ambaye aliingia uwanjani hapo jana aliwanda ndani ya sanduku lwenye langi za Njano na Kijana na Mwisho wa burudani hizo Mabingwa hao wa kihistoria walitest mitambo yao Mipya’Wachezaji’ kwa kukipiga na Zanako ya Zambia na kuambulia kichapo cha bao 2-1.

 Wakati hayo yakiendelea Jijini Dar Mwandishi wa Mtandao huu alikatiza Maeneo ya Mji Mpya kwenye tawi kuu la Simba la Mkoani Morogoro na kushuhudia bango hilo likiandikwa maneno ya Shombo .kama linavyosomeka pichani hii ni kuendeleza utani wa Jadi wa timu hizo kongwe nchini.   

 

Mtandao huu haujang’amua Mara Moja vibwenge kwenye Tamasha hilo ni kinanani.

 

lkumbukwe  viongozi wawili waandamizi wa Simba  Mkuu wa kitengo cha habari na Mawasiliano Haji Manara na Afisa Mtendaji Mkuu’C’E’O Senzo Masingi raia wa Afrika Kusini waliihama timu hiyo na kujiunga na Yanga kwa nyakati tofauti na jana walikuwepo kwenye Tamasha hilo.

Saturday, August 28, 2021

MUNGU AWATUA MIZIGO WATU WALIOMUAMINI

Mungu Kupitia Mtumishi wake Shekidelea alimkabidhi kitita cha Laki 6 Mlemavu Msafiri Jeremia aliyegongwa na tren na kukatwa Mguu na mkono wakati akifanya biashara kwenye stesheni ndogo ya Kilosa Morogoro
Matama akishuhdua Mafundi wakipima leman ya Nyumba yake baada ya kufanikiw akununulia kiwanja na Mungu
                     Ujenzi wa nyumba hiyo ukiendelea
Nyumba hiyo ikikalibia kukamlika, ambapo kwa sasa imeshakamilika na Athumani Mohamed Matama amepewa kibari na Mungu kuhamia kwenye Mjengo wake huo wa kisasa baada ya kupitia changamoto nyingi kwenye nyumba ya kupanga
Mungu Kupitia Mtumishi wake Shekidele akinunua kilo mia za Unga kwa lengo la kuwapelea watoto Yatima wa Kituo cha Mkitunda Kihonda Morogoro ambao kwa mujibu wa Mlezi wao walikabiliwa na njaa ya kukosa chakula Mungu akasikia kilio chao na kuwapatia Unga huo
Mungu kupitia Mtumishi wake Shekidele akimkabidhi unga huo mkurugenzi wa kutuo hicho huku baadhi ya watoto hao watima wakishuhudia tukio hukio hilo
..Mzifo Mzito wa changamoto ya Kimaisha aliyoipitia Matama kwenye nyumba ya kupanga kabla ya Mungu kumjengea Nyumba ya Kisasa na kumtua Mzigo huo Mzito

 Mwandishi wa Mtandao huu akiwa na Matama siku walipoend  kununua Kiwanja maeneo ya Kichangani

MATHAYO 11-28-30

“Njoo kwangu nyinyi nyote  Msumbukao na wenye  kulemewa na mizigo, nami nitawapunzisha.

Jitieni nira yangu,mjifunze kwangu,kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo nanyi mtapata raha nafsini mwenu. Kwa maana nira yangu ni laini na Mizigo yangu ni Mwepesi”

 

Hilo ndilo neon letu leo Jumapili ya Agost 29.

           


Friday, August 27, 2021

TWAHA KIDUKU AWASHUKURU WAKAZI WA MORO KWA MAPOKEZI MAKUBWA, C.E.O MSJ AIBUKA KWENYE SHANGINGI LAKE NA KUFANYA KAZI YA UPAPARAZI.

Bondia Twaha kiduku akiwashukuru wananchi wa Mkoa wa Morogoro
Diwani wa Kata ya Mkundi Mh Seif Chomoka akishiriki mapokezi hayo akichomoka juu ya ndinga yake ya bei mbaya Shangingi V8

 Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mhe Aziz Abood akiongoza mapokezi yake akichomika juu ya Shangingi lake Titota V8 Wanasisi hao wawili Abood na Chomoka ndio ambao walitisha na magari yao ya kifahari akishiriki maandamano hayo ya kuchomoka juu ya magari yao


 

                          Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

Bondia Maarufu  nchini asiye na Mpinzania kwa sasa kufuatia  kuwatwanga Mabondia Maarufu na wengine kukacha kupigana naye Twaha Kassim ‘Twaha Kiduku’ amewashukuru wananchi wa Mkoa wa Morogoro kwa mapokezi makubwa waliyompatia baada kumtwanga kwa mara ya Pili bondia  Abdallaha Pazi Dulla Mbabe Mkazi wa Dar.

 

Baada ya kushuhudia Umatia Mkubwa wawatu hasa alipofika katikati ya Mji wa Morogoro Kiduku alishangwaza na Umati huo na akaamua kunyoosha mikono yake kisha akaiunganisha ikiwa ni ishara ya kuwashukuru.

Mara baada ya kuwasili maeneo ya Mikese akiwa ndani ya gari yake Mpya ya zawadi Crown akitokea Dar Kiduku alishuka kwenye gari hilo na kupanda kwenye gari la wazi pamoja na Mwandishi wa Mtandao huu na kuanza safari ya kuelekea Moro Mji kutoka Mikese umbali wa kilomita 25.

 

Katika Msafara huo walikuwepo watu wengi Maarufu wakiongozwa na  Afisa Mtendaji Mkuu [C’E,O] wa Chuo Cha Uandishi wa Habari Morogoro’MSJ’ Seif Chomoka ambaye pia ni Mh Diwani wa Kata ya Mkundi kwa leseni ya CCM.

 

Mwandishi wa habari hizi alimshuhudia Big Boss huyo wa MSJ akiibuka kwa juu kwenye Shangingi lake ‘Totota V8’ na kuanza kupiga Picha Msafara huo akitumia kamera ya simu huku akitinga Flana nyeupe yenye Picha ya Twaha Kiduku.

 

Mh Chomoka mbali ya kuwa Mwanasiasa pia ni Mwanamichezo Mzuri ambapo juzikati kwenye uchanguzi  Mdogo wa kujaza nafasi za Viongzi wa chama cha Soka Mkoa wa Morogoro’MRFA’ Mh Chomoka aligombea nafasi ya Katibu Mkuu kwa mshangao wawengi jina lake lilikatwa dakika za mwisho kuelekea kwenye mchaguzi huo ambapo Mchungaji Emmanuel Kimbawaya Mkazi wa Tubuyu aliibuka kidedea kwenye nafasi hiyo ya Katibu Mkuu.

 

lkumbukwe Mh Chomoka pia kwenye Uchaguzi wa Umeya awari alishinda kwa kura 20 zidi ya 19 za Mpinzani wake Pascal Kihanga aliyekuwa akitetea kiti chake.

Siku chache mbele uchaguzi huo uliludiwa kwa maelezo kwamba Chomoka ahakuvuka nusu ya kura za wajumbe 42 waliopiga kura.

 

Hivyo goma likaludiwa  huku mgombea wa 3 aliyepata 3 aliamua kujitoa wakabaki Kihanga na Chomoka kura zikapigwa zaidi ya mara 2 wawili hao walifungana kwa kupata kura 21 kwa 21 baadae majina yote 2 yakapelekwa Dodoma na majibu yakaludi Mh Kihanga ambaye ni Diwani wa Kata ya Mazimbu  katangazwa Mshindi hivyo akaendelea na nafasi yake hiyo ya Umeya.

Wednesday, August 25, 2021

MAPOKEZI YA KISHINDO YA TWAHA KIDUKU, KWA WAKAZI WA MORO SIO STORI AMEFUATA NYAYO ZA WATANGULIZI WAKE.

 
Twaha Kiduku akiwapungi mashabiki waliojitokeza kwa wingi kumlaki
..Gari ambalo amekabidhiwa baada ya kumtwanga Dulla Mbabe likiwasili Mkoa Morogoro eneo la Nane nane

..Mh Abood akiongoza Manimia ya wananchi wa Mkoa wa Morogoro kumlaki Twaha Kiduku
Msafara huo ukiwa eneo la Kingolwira jirani na Kituo cha Polisi
Msafara huo ukiwa Mkambarani jirani na baa ya Afande Zombe
Mc wa shughulia hiyo Calvin Ponela 'Zombi' akiwajibika kuamsha amsha
..Heka heka gari la Samora Mwarabu Maarufu Samora Simba Oil liliganga na gari lingine kwenye heka heka hizo za aMapokezi ya Twaha

Twaha Kiduku akizungumza na Mwandishi wa Mtandao huu aliyekuwa ndani ya gari hilo la Wazi akuchukua matukio mbali mbali
Twaha Kiduku akiwa na Kocha wake Chaaz Mbwana'Power lranda'
Twaha Kiduku akiiwa ndani ya studio za Planet Redio Morogoro
Bondia Francsi Cheka akiwa na Mwandishi wa Mtandao huum siku chache baada ya kumtwanga Thomas Mashali
Afande Sele akiwa na wattoto wa Mwandishi wa Mtandao huu Kulia Tumain Dustan Shekidele, ambaye alisoma darasa Moja na mtoto wa Afande Sele Tunda shule ya Msingi Nguzo Eglish Mediam[ kushoto ni Neema Dustan Shekidele.
                       Mwishi Mwampamba


 

Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

 

TAKRIBANI Mwezi mzima Wananchi wa Dar[Wazalamo] na wenzao Moro[Waluguru] walikuwa wakitambia huku wakipigana vijembe kila Moja akidai Bondia wake ataibuka kidedea na kunyakua zawadi ya Gari.

 

Agost 20 Promoto Maarufu wa ngumi nchini ‘Mjeda’ Kanali Seleman Semunyu ambaye pia asili yake ni Morogoro aliisimamisha nchini na kwa kuandaa Mpambano wa Ngumi uliowahusisha wapinzani wa Jadi Twaha Kassim’ Twaha Kiduku Kutoka Morogoro na Abdallah Pazi’ Dulla  Mbabe Mkazi wa Dar.

 

Katika Mpambano huo usio wa ubingwa wa kugombea gari aina ya Crown ambapo mpambano huo umepewa jina la ‘Crown toa Roho’ulipigwa Ukumbi wa Ubongo Plaza jijini Dar nyumbani kwa bondia Dulla Mbabe.

 

Kwenye tambo hizo wananchi wa Dar Wazalamo waliwatania wenzao wa Moro’Waluguru kwamba gari hilo la kifahari litabaki Dar kwa vile Morogoro hakuna barabara za kupiga gari hilo.

 

Huku wananchi wa Moro wakijibu mapigo wakiwaeleza Wazalamo kwamba maisha yao siku zote yanategemea wananchi wa Morogoro, wakitolea Mfano Maji ya kunywa na Umeme wananchi hao wanategemea kutoka Moro pia Mkuu wa wa Mkoa Mh Amos Makalla ni Mwana Morogoro.

 

Mwandishi wa habari ambaye naye ni Mkazi wa Morogoro anawaongezea nyama wananchi hao wa Moro kwa kuwaeleza kwamba Promota wa Pambano hilo Kanali Semunyu ni Mwanamorogoro kwao ni Msamvu Magodoroni na Meneja wa Ukumbi wa Ubungo Plaza lilipofanyika pambano Mr Sozi ni Mwanamorogoro ambaye alisoma shule ya Msingi na Mwandishi wa Mtandao huu. 

HII NI MARA YA 4 WASANII WA MORO WANANYAKUA GARI MBELE YA WASANII WA DAR.

 

Kwa wakazi wa Morogoro kukusanyika kwa wingi kuwapokea wasanii walionyagua magari mbele ya wasanii wa Dar hii si Mara ya kwanza kwa Kiduku’. Mara ya kwanza ni Mwaka 2003 ambapo umati Mkubwa wawananchi wa Moro walijitokeza Maeneo ya Mikese kumpokea Mwisho Mwampamba aliyeibuka mshindi wa Pili kwenye jumba kubwa la Afrika Kusini Big Brother Afrika’BBA’na kuzawadi Milion 50 kwenye shindano hilo wasanii wa Dar na wamataifa mengine walitolewa hatua za awari huku Mwampamba akiin’alisha Tanzania na Mkoa wake wa Morogoro,

 

Kama hiyo haitoshi Mwaka 2004 Msanii wa muziki wa kizazi Kipya Selema Msindi ‘Afande Sele’ alipokelewa na Umati Mkubwa wawananchi wa Morogoro waliojipanga toka Mikese Mpaka Mo Town baada ya Msanii huyo kunyakua zawadi ya gari kwenye shindano la  kumsakali mkali Vina Mfalme wa Rhymes lililofanyika Ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar.

 Mwandishi wa Mtandao huu alikuwa ndani ya Nyumba ambapo Shindano hilo liliwashirikisha wasanii 10 nyimbo zao kwenye mabano 1.Afande Sele[Dalubini Kali]

2.Inspector Harun[Bye Bye]

3.Man dojo na Domokaya[Nikupe Nini]

4.Mwana-FA[Umenitega]

5.JayMo[[ Kama Unataka]

6. Solo Thang[[Mtazamo]

7.Madee [Kazi yako Mola]

8. Soggy Dogg[Kulwa na Dotto] .

9. Prof J [Goma lake limenitoka kichwani]

10. Dully Sykes ambaye alijitoa kwenye shindani hilo dakika za Mwisho huenda akihovia Moto wa Afande Sele. Haikuishia hapo ndio maana tunasema Mapokezi makubwa kwa wasanii wa Moro sio habari kubwa inaweza kuwa habari kubwa kwa wananchi wa Dar ambao hawajawahi kushinda zawadi ya gari mbele ya wasanii kutoka Moro kama Mwaka 2017 Bondia Francsi Cheka mbali ya kuingwanga Familia ya Masumbwi ya Matumla alimtwanga Mwana Dar nyumbani kwake Dar  Thomas Mashali kwenye Pambano la kugombea gari aina ya Noah, ambapo umati Mkubwa wawananchi wa Moro walijipanga toka maeneo ya Mikese Mpaka Mo Town wakilisukuma gari halo umbali wa takribani kilometa 25.

 

Juzi Twaha Kiduku hapo hapo Dar amempiga kwa mara ya Pili Dulla Mbeba na kuzawadiwa Gari ambapo mapokezi yake ya kufana ndio hayo Pichanim huku Dulla Mbabe na wazalamo wake wakiwa Dar wakishuhudia Mapokezi hayo kwenye Mitandao ya Kijamii huku wakienda kununia kwao kwa hasira. Wana Moro wanasema Bendera Chuma, Mlingoti Chuma Show Show kituoa kinachofuatani Where? Tanga au ila Tanga sio powa kama mnavyozani.

 

 
 

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...