Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Friday, October 10, 2025

BABU KICHUYA AKAGUA UJENZI WA DARAJA,

           Muonekano wa daraja la zamani baada ya kukatika
             Babu kichuya akikagua daraja hilo jana mchana



Jengo  linaloonekana kwa  mbali lenye paa la vigae vyekundu ni eneo a Stesheni ya Morogoro
Babu Kichuya kushoto akiwa na Mwandishi wa habari hizi wakijiandaa kuelekea darajani

                             .......Safari ya kuelekea darajani akianza


              Na Dustan Shekidele,Morogoro,  

Mzee Ibrahim Mohamed  Mangwende Almaarufu ‘Babu Kichuya’  amekagua ujenzi wa daraja la Relwe Maarufu daraja la Ng’ombe lililopo mtaa wa Makaburi ‘A’ Kata ya Mji Mpya Mkoania hapa.

 

Jana majira ya mchana Mzee huyo akiwa na Mwandishi wa habari hizi wakitumia usafiri wao wa baiskeri walitinga kwenye daraja hilo na kushuhudia Mkandarasi akiwa Site akiendelea na kazi kwa kasi ya kuridhisha.

 

Akizungumza na Mtandao huu mara baada ya kukagua daraja hilo ambalo lipo mto Morogoro mzee huyo alisema.

 

” Mimi ni mwananchi wa Morogoro niiyekulia Mji Mpya nimeamua kuja kukagua ujenzi wa daraja letu ama kwa hakika nimefurahishwa na kazi nzuri inayondelea kwenye mradi huu,kipekee naipongeza serikali yetu kwa ujenzi wa daraja hili litakalofungua barabara hii muhimu ya kuelekea kichangani”alisema babu kichuya ambaye ni fundi bomba mstaafu wa Mamlaka ya Maji safi na Maji taka Mkoa wa Morogoro’MORUWASA’

 

Ifahamike Mzee huyo mmoja wa wamjuu zake ni mchezaji nyota wa Maafande wa JKT Tanzania Shiza Ramadhan Kichuya aliyewahi kutamba na Simba kabla ya kutimkia Misri kucheza Soka la Kulipwa.

 

    KWA NINI LIITWE DARAJA LA NG’OMBE?

Miaka ya nyumba wakati Mwandishi wa habari hizi anasoma shule ya Msingi Kaloleni iliyopo  jirani kabisa na daraja hilo,walishuhudia Makundi ya Ng’ombe yakivushwa kwenye daraja hilo dogo linaloonekana pichani yakitokea Machinjio ya Morogoro yaliyopo Mtawara wakipelekwa Stesheni ya Morogoro inayoonekana kwa mbali yenye vigae vyekundu.

 

Baada ya kufika stesheni hapo Ng’ombe hao hupakiwa kwenye Treni ya Mizigo na kupelekwa Machinjio ya Ng’ombe  Vingunguti Jijini Dar es salaam.  

 

Takribani miezi 5 iliyopita daraja hilo lilikatika na kukata mawasiliano ya pande mbili, huku Mtandao huu ukiwa wa kwanza kuripoti habari hiyo.

 

Baadae Mkandarasi wa daraja hilo alijenga daraja a muda linaloonekana pichani sambamba na Mkandarasi huyo kuanza kwa  kwa kasi  ujezi wa daraja kubwa huku akiwa kwenye hatua za mwisho za kulikamilisha kama.

 

 

 

 

 

No comments:

Post a Comment

VITUKO VYA MWEZI JANUARI

  Mwezi uliopita tumeshehelekea Siku Kuu mbili X Mas na Mwaka Mpya.   Mwezi huu dume January tunashehelekea kulipa Ada za Shule na kod...