Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Sunday, September 14, 2025

MUNGU ANACHUKIZWA NA MWANAMKE ANAYE VAA NGUO ZA KIUME.


 Mwandishi wa Mtandao huu akionyesha mavazi hayo ya kiume.

 

Ujumbe wa neno la Mungu jumapili ya Leo Septemba 14,kupitia Maandiko Matakatifu kutoka kumbumbu ya Torati 22 Mstari 5.

 

“ Mwanamke asivae Mavazi  yampasayo  Mwanamume wala  Mwanamume  asivae mavazi ya Mwanamke  kwa maana kila afanyaye mambo hayo  ni machukizo kwa Bwana Mungu wako”

           UCHAMBUZI WA NENO HILO.

Kwa kipindi kirefu sasa baadhi ya wanawake wanavaa nguo za kiume Suluari, Kaptura, Mashati na kofia [Kapero] wanadunda mitaani bila wasi wasi wowote.

 

Wengine wanafika mbali zaidi wanaingia kanisani wakiwa na nguo hizo za kiume zilizo wabana makalio.nafurai makanisa mengi yamepiga marufuku wanawake kuingia kanisa na mavazi hayo.

 

Kama hiyo haitoshi wengine wanakwenda ukweli wakiwa wametinga mavazi hayo ya kiume, siku zote mavazi yanamdharaulisha mtu na mavazi hayo hayo yanamuheshimisha mtu  aliyevaa mavazi ya staha.’Heshima’

 

Wakishatoka huko ukweli kama familia husika ina hofu na Mungu moja kwa moja vikao vya kumjadili mkwe wao huyo vitaanza chapu kwa haraka.

Niwapongeze wanaume binafsi sijashuhudia Mwanaume amevaa nguo ya kike Mfano kavaa gauni anaendesha boda boda lakini nimeshuhudia Mwanamke kavaa suluari anaendesha boda boda.

 

Pia nimeshuhudia baadhi ya wanaume wakijipodoa kama wanawake,ingawa Kwenye maandiko hayo ya Mungu swala la Mwanaume kujipodoa halipo lakini naamini hilo nalo ni chukizo kwa Mungu.

 

 Mara nyingi wanaojipodoa ni wale ‘kuku watamu. Mtoto Si Riziki’ Makaka Poa a.k.a Mashoga. Majina yote hayo mabaya ni yao.

       


No comments:

Post a Comment

VITUKO VYA MWEZI JANUARI

  Mwezi uliopita tumeshehelekea Siku Kuu mbili X Mas na Mwaka Mpya.   Mwezi huu dume January tunashehelekea kulipa Ada za Shule na kod...