Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Monday, September 8, 2025

A-Z MWEZI KUFUNIKWA NA WINGI KWA MASAA 5







 

   

        Na Dunstan Shekidele Mogoro.

JANA Septemba 7 dunia ilishuhudia tukio adhimu la Mwezi kufunikwa na wingu  kwa muda wa masaa 5.

 

Tukio hilo lilianza saa 1 usiku mpaka saa 5 usiku huku Mwandishi wa habari hizi kulifuatilia tukio hilo Mwanzo Mwisho  kwa  muda wote wa masaa  matano akiwa  nje ya nyumba akipiga  picha tukio hilo akitumia kamera ya kisasa yenye uwezo wa kupiga picha umbari mrefu.

 

Katika hali ya kuondoa mashaka na makando kando ya tukio hilo, Mpiga picha huyo aliamua kuseti kamera yake tarehe na saa hivyo kila picha iliyopigwa ilionyesha tarehe muda [saa].

 

Baada ya wingu hilo kuukamata Mwezi huo kuanzia saa 1 mpaka saa 3,ilipotimu saa 4 usiku wingu hilo taratibu limeanza kuachia Mwezi kama vile Nyoka anayejivua gamba la zamani na kubakia na jipya.

 

Muda huo wa saa 4 Mpiga picha huyo Dunstan Shekidele alipiga picha kila dakika  mpaka mwezi huo ulipoachiwa saa 5,00 usiku, nimeamua kurusha baadhi ya picha hizo kuanzia saa 4 na dakika 34 mpaka  Mwezi huo ulipoachiwa saa 5.00 usiku angaia saa kwenye kila picha.

lfahamike Mwaka mkubwa unasiku 366 na  mdogo unasiku 365 hivyo kwenye moja ya siku hizo tukio hili hutoke mara nyingine hutokea mchana kwa Jua kufunikwa na Mwezi.

 

lkitokea mchana huwa na mvuto zaidi kwa sababu ya uwepo wa giza zito kufuatia Nuru kupotea kwa muda baada ya Jua kufunikwa na.

 

 Baada ya kazi hiyo kutamatika Mpiga picha huyo alizima kamera yake kisha akaingia kwenye kiota chake kulala. 

         ‘Mwacheni Mungu aitwe Mungu’

 

No comments:

Post a Comment

VITUKO VYA MWEZI JANUARI

  Mwezi uliopita tumeshehelekea Siku Kuu mbili X Mas na Mwaka Mpya.   Mwezi huu dume January tunashehelekea kulipa Ada za Shule na kod...