Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Tuesday, July 29, 2025

MTOTO WA MWAKA 2000 HAWEZI KULIJUA HILI

                  Soko Jipya la Kisasa a Manispaa ya Morogoro

                                   Soko la zamani

 


       Na Dustan Shekidele,Morogoro.

 HII inaweza kuwa ni kichekesho, wakati wafanyabiasha wa Soko kuu la Morogoro wengi wao wakifanya biashara zinazuhusiana na Kilimo kinacho hitaji mvua nyingi zitakazomweshesha Mkulima huyo  kuvuna mazao Mengi na kuyaingiza sokoni.

 

Wakati huo huo wafanyabiashara hao wa Soko kuu la Morogoro unapofika msimu wa Mvua[Masika] baadhi yao huchukizwa na msimu huo kufuatia mafurika yanayosababishwa na mvua hizo kuvamia kwenye Soko hilo mara nyingi nyakati za usiku wakati wafanyabiashara ha hawapo.

Wanapfika asubuhi wanakutana na mafuriko yariyosomba  bidhaa zao huku baadhi yao huku baadhi yao wakiendesha biashara hizo kwa mitaji ya Mikopo.

 

 Hii nilikuwa ni Mwaka 2015 kushuka chini, mafuriko hayo yalizalishwa na mto kikundi uliokatiza katikati ya Mji kando ya Soko hilo ambalo limejengwa Mwaka 1953.

 

Nakumbuka kufuatia kero ya Mto huo Mbunge mmoja wa Jimbo la Morogoro[tunamuhifadhi jina] kwenye moja ya michango yake bungeni aliiomba serikali kuhamisha mto huo usikatize katikati ya Mji wa Morogoro.

 

Mwaka 2017 Serikali ililivunja soko hilo nakujenga Soko la Kisasa la Ghorofa kama linavyoonekama pichani,baada ya kukamilika   lilipewa jina la Chifu wa Kabila la Waluguru [Soko Kuu la Chifu Kingalu]

Kwa sasa Mtandao huu umeshuhudia mafundi wakiendele na kazi ya kuutanua Mto huo wa Kikundi sambama na kuujenga kwa maweze lengo kuu  kuthibiti mafuriko yanayozalishwa na mto huo unaopokeka maji toka juu ya Milima ya Uluguru.

 

 

Mtoto wa 2000 unajua kwamba kwenye soko hilo la zamani upande wa Bank ya NMB la kuu la kuingia sokoni hapo lilikuwa likiitwa lako la Jiji?.

lkumbukwe unapoingia kwenye lako hilo kushoto alikuwepo bingwa wa kuchoma Mishikaki aliyefahamika kwa jina la  [Jeta Mishikaki]

 Huyu jamaa mishikaki yake ilikuwa mitamu sana jioni wahindi na waarabu wakifunga maduka ya mtoko wao ulikuwa kwa Jeta Mishikaki wakifuata mishikaki, Chipsi, Ndizi Choma na chachando  tamu tamu.

 

Kwa sasa mkali wa kuchoma Mishikaki,Chipsi na Ndizi Choma Mkoa wa Morogoro ni Rafiki yangu Mzige Makamba huyu jamaa anapatikana chini ya Mkungu nje ya baa ya Kambarage iliyopo mzunguko wa barabara ya SUA.

 

Kufuatia utamu wa Mishikaki ya Mzinge Makamba miezi ya hivi karibuni amefungua ofisi nyingine Jijini Dodoma,akitekeleza maombi ya wateja wake wakiwemo waheshimiwa wakiongozwa na Mbunge wa Bumbuli Mhe January Makamba, ambao wengi wao wanapotoka Dodoma kwenda Dar  ukatiza kambarage kutafuna mishikaki hiyo.

 

Akizungumza na Mtandao huu ‘Big Boss’ Nzinge Makamba amesema baada ya kufungua gori Dodoma kwa sasa yuko mbioni kufungua ofisi nyingine Dar es salaam.

Friday, July 25, 2025

KILA LENYE KHERI MWANA MOROGORO KARIM MANDONGA.


 

 

    Na Dustan Shekidele Morogoro,

MWANA Morogoro Bondia Karim Mandonga a.k.a ‘Mandonga Mtu kazi’ Mkazi wa Kata ya Mkundi Manispaa ya Morogoro, kesho Juai 26 anatarajia kupanda ulingoni kuzichapa na mpinzani wake mkubwa Shabani Kaoneka

Kuelekea pambano hilo la Dar Boxing Derby wana Morogoro wanamsapati  Mandonga huku baadhi ya wakijiandaa kupanda Tren ya mwendokasi [SGR] kuelekea Dar es salaam kumsapoti Mwana Morogoro huyo ‘Salange’ wa Stend ya Msamvu Karim Mandonga[pichani] anayetamba na ngumi yake ya Kilumbilumbi.

 

Je Mandonga baba Kharid ataibuka kidede na ngumi yake hiyo ya Kilumbilumbi au atachezea Vitasa vikari vya Shabani Kaoneka? Swali hili itajibiwa kesho usiku wa Vitasa.

Tuesday, July 22, 2025

YARIYOJIRI STEND YA MABASI MSAMVU.POLISI MORO WAPONGEZWA.


 Morgoro Mji kasoro Bahari. ndiyo kauli ya Waluguru wa Mkoa wa Morogoro.

Hii sio Meli na wala sio Uwanja wa Ndege  'Air Port' ni stend ya mabasi ya Mikoani ya Msamvu Morogoro. Picha na Dustan Shekidele.


    Na Dustan Shekidele,Morogoro. 

WANANCHI  Mkoa wa Morogoro wamelipongeza Jeshi la Polisi kupitia kitengo  cha Usalama barabara kilichopiga marufuku wakatisha tiketi wa stend ya Mabasi ya Msamvu  kuwakatia tiketiki abiria wakati basi husika halijafika ndani ya stendi.

 

 Awari baadhi ya wafanyakazi wa mabasi,Mawakala, wakatisha tiketi na wapiga debe’Masalange’ wamekuwa na tabia ya kuwakatia tiketi abiri wakati wanajua fika basi husika halijafika stend huenda liko Gereji au bado liko safarini likitokea mikoani.

 

Kufuatia kero hiyo  hivi karibuni Maafisi wa kikosi cha Usalama barabarani Mkoa wa Morogoro walitinga kwenye stend hiyo ya kisasa na kupiga marufuku abiria kukatiwa tiketike wakati basi husika halijafika stendi,

 

Vijana hao wa IGP Wambura wamewakata wakatishaji tiketi hao kumkabidhi tiketi abiria wakati basi husika lipo stend hivyo na kwamba abiria anapokabidhiwa tiketi  moja kwa moja anaingia kwenye basi.

  Mtandao huu unaungana na wananchi hao kulipongeza Jeshi la Polisi kukomesha kero hiyo kwa wananchi

Ifahamike mara kwa mara msimulizi wa habari hii hukatiza kwenye stendi hiyo kwa shughuri zake mbali mbali alishuhudia ‘Live’ kero hiyo huku wanaofanya jambo hilo wakiambizama maneno haya ya kejeri.

“ Twenda tukasake abiria mwingine Yule nimeshamnyofoa mbaya hanauwezo tena wa kuruka atasubiri mpaka chuma lifike”

Kauli zao nyingene “Yule abiri nimeshamkata miguu hatembei tena tukatafute abiri mwingingine tuingize posho kwa tajiri”

Wapigadebe hao wanamaanisha kwamba abiri huyu hawezi kupanda basi lingine kwa sababu tayari wameshamuzia tiketi hivyo hata kama basi litafika baada ya masaa matatu au manne mbele  atasubiri tu ndio maana wanakauli zao hizo za kumnyofoa mbaya na kumkata miguu.

Wapiga debe hao wanajisahau kwamba kuna wasafiri wengine wanaharaka, mfano wengine wanakwenda msibani, wengine wanakwenda kwa wagonjwa na wengine ni wanafunzi .

 

 

Saturday, July 19, 2025

MUNGU ANASEMA WATU WABAYA NI KAMA BAHARI ILIYOCHAFUTA,HUTOA TOPE NA TAKATAKA.

Dustan Shekidele akifanya mahojiano na Watumishi wa Mungu Askofu Jacob Ole Mameo wa KKKT Jimbo la Morogoro.

 

......Shekidele akiungana kwenye lbada ya kuusubiri Mwaka mpya KKKT Usharika wa Mji Mpya
Teresphori Mkude wa Roman Katoliki Jimbo la Morogoro

Maaskofu hao kwa sasa wamestaafu Mameo akistaafu mwezi uliopita na Mkude alistaafua takribani miaka 5 iliyopita.


 

  

ISSA 57.18-21

“Nimeziona njia zake nami nitamponya nitamuongoza pia nitamrudishia  faraja zake yeye na hao wanaomlilia.

 

Mimi nayaumba matunda ya midomo,Aman,amani kwake yeye aliye mbali na kwake yeye aliye karibu aseme Bwana nami nitamponya.

 

Bali wabaya wanafanana na bahari iiyochafuka maana haiwezi kutulia na maji yake hutoa tope na takataka.

 

Hapana Amani kwa wabaya asema Mungu wangu[There is no peace saith  my God  to the wicked]”

Huu ndio ujumbe wetu wa Neno la Mungu Leo Jumapili ya Julai 20-2025.

Mwenye masikio na alisikie neno hili la Mwenyezi Mungu Muumba wa mbingu na Ardhi.           

                           

Friday, July 18, 2025

MTETEZI WAWANYONGE AKALIA VUMBI AKISIKILIZA SHIDA ZA WANANCHI WAKE.

                            Mhe Abood akiketi chini ya vumbi


 

                             Na Dustan Shekidele,Morogoro.

MTETEZI wawanyonge Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini,Mhe Abdulazizi Mohamed Abood Maarufu [ Azizi Abood] Mara zote ameoneka kuwa jirani na wananchi wa Jimbo lake kwenye shida na raha.

 

Mhe Abood ambaye  anatajwa kuwa tajiri namba moja mkoa wa Morogoro akimiliki Viwanda, Maduka, Vituo vya Mafuta, Vyombo vya habari[Abood Media] Malori na Mabasi yanayofanya safari  mikoa mbali mbali ya Tanzania.

 

Mbali na Utajiri  huo lakini linapofika swala la wananchi wa jimbo lake utajiri wake anauweza kando na kujichanganya na wananchi wao, kama wamekaa kwenye vumbi naye anakaa kwenye vumbu kama wanafanya ujasiria mali wa kusokota Chapati naye anasokota chapati kama wanacheza Ngoma naye anasakata Rhumba.

 

Hivi karibuni katika hatua ya kutekeleza wa Ilani ya chama cha Mapinduzi [CCM] ya uwezeshaji wananchi Kiuchumi 2000-2025.

 

Kuelekea utekelezaji wa ilani hiyo kiasi cha shilingi Bilion 2,171,359,000,00 zimetolewa kwa vikundi mbali mbali vya Jimbo la Morogoro kama asilimia 10 ya Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

 

Vikundi vilivyofaidika na pesa hizo ni Vikundi 127 vya wanaume vilivyokopeswa Bilion 1,298,496,000,00.

 

Vikundi 56 vya Vijana vimekopeswa Milion 723,013,000,00 na Vikundi 19 vya Walemavu nimekopeswa Milion 149.850.000.00.

 

Kama hiyo haitoshi Mtandao huu ulimnasa Mbunge huyo akizunguka mitaani na miguu akisikiliza changamoto za wananchi wanaofanya shughuri ya kuomba omba mitaani siku za ljumaa na jumapili.

lfahamike hata kabla ya hajawa Mbunge wa Jimbo hilo Mhe Azizi kwa zaidi ya miaka 20 mfurulizo amekuwa akitoa mabasi yake kwenye shughuri za misiba kwa wananchi wa Jimbo la Morogoro huduma hiyo alianza kuitoka  Mwaka 2000 mpasa sasa inaendelea.

 

VITUKO VYA MWEZI JANUARI

  Mwezi uliopita tumeshehelekea Siku Kuu mbili X Mas na Mwaka Mpya.   Mwezi huu dume January tunashehelekea kulipa Ada za Shule na kod...