Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Monday, June 30, 2025

TUKIO LA DABI YA YANGA NA SIMBA LAIBUKIA KWENYE NDONDO CUP







                                                Mshasha

 
                            Na Dustan Shekidele Morogoro.
 
HII ni kama ile Pelnati aliyosababisha kipa wa Simba Mussa Kamara kwenye mchezo wa Dabi kati ya Yanga na Simba uliopigwa Jumatano iliyopita uwanja wa Mkapa Dar na mnyama simba kupokea kichapo cha bao 2-0. 
 
Kwenye tukio hilo Kipa wa Simba Kamara akiwa ndani ya boksi aliacha mpira na kuuvaa mwili wa Kiungo ‘fundi’ wa Yanga Pacome na Mwamuzi wa mchezo huo kutoka Misri aliamulu mkwaju wa pelnati.
 
Pacome aliyekuwa mwiba mchungu kwa Simba kwenye mchezo huo alibeba jukumu la kupiga Pelnati hiyo aliyoipiga kiufundi na kuipatia timu yake bao la kwanza. 
 
Tukio kama hilo limetokea kwenye mchezo wa Fainali ya Planet Ndondo Cup kati ya Damu Chafu Fc na Chaka Bovu Fc
Mshambuliaji hatari wa Damu Chafu Johasson Clement Mshasha aliingia ndani na boksi na mpira ukiwa kwenye himaya yake akijiandaa kufunga Kipa wa Chaka bovu Tobah Kutisha anayeitumiki Mtibwa Sugar kwa kushilikia na na beki wake waliacha mpira na kumvaa Mshasha, refa wa mchezo huo Afande wa jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro Athuman Lazi ambaye ni mwamuzi wa zamani wa Ligi Kuu alimeza filimbi akimaanisha hakuna faulo
Ifahamike Mshasha alikuwa mchezaji nyota ya Mawenzi Market ya Mkoani hapa, baada ya timu hiyo kushuka daraja kutoka la kwanza kwenda la Pili wamiliki wa timu hiyo wafanyabiashara wa Soko la Matunda la Mawenzi waliamua kuiuza timu hiyo kwa Mwanasiasa maarufu mkoani Singida.
Mshasha alihamishiwa kwenye timu ya DTB Fc baadae ikabadilishwa jina ikaitwa Singida Big Stars wakati huo ikiwa daraja la pili, yeye na Hamis Tambwe waliipandisha Ligi kuu, Tambwe akiwa klnara wa ubachikaji mabao na Mshasha akishika nafasi ya pili.
Baada ya kupanda Ligi Kuu ,Mshasha na Tambwe waliachwa kwenye timu hiyo iliyosajiri wachezaji wengi nyota kutoka mataifa mbali mbali ikiwemo mataifa yanayoongoza kwa ubora wa Soka Duniani Brazil na Argentina

 

No comments:

Post a Comment

MAKALA PLANET NDONDO CUP. SIRI DAMU CHAFU KUTWAA UBINGWA MARA MBILI MFURULIZO HII HAPA.

  Baadhi ya mashabiki waliofulika kwenye mashishindano hayo.                           .....Kikosi cha Damu chafu Mkuu wa Wilaya Mhe Kilakal...