Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Saturday, June 14, 2025

NUSU FAINALI NDONDO CUP. DAMU CHAFU YAIFANYIA KITU MBAYA BLACK PEOPLE.

Winga wa Black People Said Zanda anayecheza moja ya timu za Ligi Kuu akitafuta mbinu za kumtoka beki wa Damu Chafu Sady Mapuya ambaye anakipiga timu ya Moro Kidsi inayoshiriki ligi daraja la Pili.


Nyomi ya watu iliyofurika jana uwanja wa Saba saba kwa kiingilio cha elfu 2



Beki wa Black baada ya kuiga kichwa mira uliteleza na kutambaa kwenye mkono ndani ya boksi hata hivyo Mwamuzi wa mchezo huo Selemani Kingu gani na msaidizi wake Line One Rajabu Yek yeke hawakuona tukio hilo.

Ama wameona wametafsiri mpira umefuata mkono na kuamua kuimeza firimbi kazi ikaendelea.


 Shabiki wa Damu Chafu wakiwa na bango lao lenye jumbe mbali mbliai

 

    Na Dustan Shekidele,Morogoro.

TIMU ya Damu Chafu yenye maskani yake Pande za  Mafisa Kata ya Mwembesongo mkoani hapa, wametinga Fainali ya Michuano ya Ndondo Cup, baada ya kuwadhibu Mahasimu wao wakubwa Black People’Taifa la Watu weusi’ kutoka Jijiga Kaloleni Kata ya Mji Mpya.

Vijana hao wa Damu Chafu wanaopigwa tafu na  Mtanzani anayecheza Soka la Kulipwa barani Ulaya Kelvin John’Mbappe’wamefanya hivyo baada ya kuibuka na ushindi wa pelnati 3 dhidi ya 2 za Black People baada ya timu hizo kutoka suluhu -0-0 kwenye  mchezo huo uliopigwa jana Uwanja wa Saba saba.

Ifahamike Kelvin John amezaliwa na kukulia eneo hilo la Mafisa ambapo nyumbani kwao ni jirani kabisa na maskani ya  Damu Chafu,inayoongozwa na Rais Ayub.

Ikumbukwe  Damu chafu ndio mabingwa watetezi wa michuano hiyo ya Planet Ndondo Cup, baada ya kutwaa ubingwa huo mwaka jana wakiwa na  beki kisiki wa Simba Abdulrazack Spear Hamza aliyetokea timu ya Super Sport inayoshiriki Ligi Kuu ya  Afrika Kusini.

Mara baada ya mchezo huo wa fainali kutamatika Hamza alitimkia  Dar na kusajiriwa na Simba anayoitumikia mpaka sasa akiwa  beki kitegeo.

 Kama kawaida Mtandao huu umekusanya matukio kibao kwenye mchezo huo wa jana hivyo endelea kuwa jirani na Mtandao huu muda wote kuangalia matukio hayo ya ndani na nje ya uwanja ikiwemo tukio la uhodari wa makipa wa timu zote mbili kudaka Pelnati .

No comments:

Post a Comment

VITUKO VYA MWEZI JANUARI

  Mwezi uliopita tumeshehelekea Siku Kuu mbili X Mas na Mwaka Mpya.   Mwezi huu dume January tunashehelekea kulipa Ada za Shule na kod...