Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Thursday, June 19, 2025

MBUZI WA MJINI NI KAMA BINADAMU, WANAVUKA KWENYE ZEBRA

Mbuzi na wanae amefika kwenye Zebra akisuburi kagari zipite
.....kbala ya kuvuka kaangalia kulia na kushoto kama kuna gari linakuja
....Baada ya kuona hakuna gari wala boda boda Mbuzi hao wakivuka kwenye Zebra
....Baada ya kufika katikati ya Zebra Bajaj na Boda boda zilisimama kusubiri Mbuzi hao wavuke


            Na Dustan Shekidee,Morogoro

 

 UKISTAAJABU ya Mussa huto yaona ya Firahuni.

 

Msemo huo umetimia  juzi baada ya wananchi wa Mtaa wa Manzese Kata ya Misufini Mkoani hapa.kushuhudia Mbuzi wanaojichunga wenye kivuka kwenye kivuko cha watembea kwa miguu Zebra  wakitii sharia bila shuruti.

 

Tukio hilo la kushangaza liloshuhudiwa  Live bila chenga na Mwandishi wa habari hizi  limetokea Jumanne iliyopita kwenye Zebra hiyo iliyopo barabara ya Kenyata.

 

Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo  Asha Athumani na Joseph Msimbe walipo hojiwa na Mtandao huu walisema

 

“ Kila siku tuna washangaa hawa Mbuzi  Wanaoishi Manzese jirana na kilabu cha Pombe za kienyeji cha Manzese, wanapotoka Mjini kwenye mihangaiko yao ya kusaka riziki  majira ya jioni wanaporejea nyumbani kuna njia nyingi za  kufika kwao wanakwepa kugongwa na Magari  wanakuja hapa kwenye Zebra kana unavyowaona wanaangalia kulia na kushoto kisha wanavuka  kama unavyoshuhudia vyombo vya moto vimesimama kuwapisha wapite”wamesema mashuhuda hao huku wakiangua vicheko

 

Uongozi wa serikali ya Mkoa wa Morogoro umeamua kuweka zebra eneo hilo kufuatia mzongamano mkubwa wa magari,Bajaji, Boda boda na watu wanaotembea kwa Miguu.

 

 Barabara hiyo  inatoka Mnada wa kikundi unapofanyika Mnada mkubwa kila Jumamosi ikielekea Mnada wa   Saba saba unaofanyika kila Jumapili.inapofanyikia minada hii njia ya Kikundi na Saba saba inafungwa kupisha minada hiyo inyaonza saa 1 asubuhi mpaka saa 1 jioni

 

Siku ya Minada hiyo  kuna kuwa na msongamano mkubwa wawatu, magari. Bajaj na Boda boda, kufuatia hali hiyo serikali ya Mkoa iliamua kuweka vivuko Zebra kwenye maeneo hayo.

No comments:

Post a Comment

MAKALA PLANET NDONDO CUP. SIRI DAMU CHAFU KUTWAA UBINGWA MARA MBILI MFURULIZO HII HAPA.

  Baadhi ya mashabiki waliofulika kwenye mashishindano hayo.                           .....Kikosi cha Damu chafu Mkuu wa Wilaya Mhe Kilakal...