Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Friday, June 20, 2025

JOTO LA FAINALI YA PLANET NDONDO CUP LINAZIDI KUPANDA. DAMU CHAFU WANAKESHA WAKIPIGA DUA USIKU NA MCHANA.


   Na Dustan Shekidele,Morogoro.

JOTO la fainali ya Michuano ya Planet Ndondo Cup linazidi kupanda, baada ya wanafainali timu ya Damu Chafu kunaswa na Mtandao huu wakipiga dua  wakimumba Mwenyezi Mungu awajalie kutwaa kombe hilo linalokwenda sambamba na mkwanja kirefu cha pesa.

 

Mwandisha wa habari hizi akiwa kwenye pilika pilika zake za kusaka habari mitaani jana jioni alikatiza  maskani ya timu hiyo Mafisa jirani na geti la kuu la shule ya Msingi Mafisa A na kushuhudia Rais wa timu hiyo  mwamba Ayub[kati] mstari wa chini waliochutama akiwaongoza vijana wake kupiga dua la kumuomba Mungu awafanyie wepesi kwenye fainali.


 


 

Taarifa zilizopo  ambazo hazikuthibitishwa na waandaji wa michuano hiyo zinadai Bigwa  atanyakua kombe na pesa taslim Milion 3 huku mshindi wa pili akiondoka na milioni 2.

 Leo Ijumaa inapigwa nusu fainali ya pili kati ya Wakushi Fc  na Chaka Bovu Fc, kumtafuta mshindi atakayecheza fainali na Damu Chafu June 27 kwenye michuano hiyo  iliyoandaliwa na kituo cha  Planet  Radio.

Ifahamike michuano hiyo inayofanyika kila ijumaa uwanja wa Saba saba   Mkoani hapa haina mshindi wa 3, wala wa  wane.

No comments:

Post a Comment

MAKALA PLANET NDONDO CUP. SIRI DAMU CHAFU KUTWAA UBINGWA MARA MBILI MFURULIZO HII HAPA.

  Baadhi ya mashabiki waliofulika kwenye mashishindano hayo.                           .....Kikosi cha Damu chafu Mkuu wa Wilaya Mhe Kilakal...