Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Thursday, May 15, 2025

TWAHA KIDUKU ATEMA NYONGO VITASA KUTOONYESHWA AZAM TV.



Twaha Kiduku[Mwenye Flana ya Kijana akichapa  kweli kweli na mchezaji mwenzie wa  Club ya Moro Boxing











   Kocha Pawa lranda [kulia akisimamia mazoezi hayo Picha zote na Dustan Shekidele,Morogoro.


     Na Dustan Shekidele,Morogoro.

WADAU  wengi wa Ngumi Tanzania kwa sasa wameingia kwenye dibwi kubwa la si mtofahamu baada ya Luninga Maarufu Afrika Azam Tv kusitinga kuonyesha mchezo huo pendwa.

 

Kundi kubwa la mashabiki wa ngumi  hawajua sababu za  Azam Tv  ‘Wazee wa Burudani kwa wote’kutoonyesha mchezo huo hali iliyopelekea  kila mmoja kusema lake.

 

Taarifa zilizopo zinadai Azam Tv ambao kwa asilimia 90 ndio walioinua mchezo huo  wamesitisha kuonyesha masumbwi baada ya bondia mmoja kuishitaki  Mahakama.

 

Kufuatia hali hiyo Mwandishi wa habari hizi amemtafuta  bondia maarufu nchini Mwana Morogoro Twaha Kassimu Maarufu Twaha Kiduku  ambaye pia ni balozi wa Azam Media kwa lengo la kusikia kauli yake baada ya mabosi wake kusitisa  kuonyesha  ngumi.

 

 Akizungumza  jana jioni mara baada ya kumaliza  mazoezi na Klabu yake ya Moro Boxing ndani ya Ukumbi wa Urafiki uliopo Saba saba Mkoani hapa  Kiduku ‘Morogoro Finest’ alisema.

 

”Ni kweli mimi ni balozi wa Azam Media ninamkataba wa miaka 3, kiukweli kitendo cha Azam kutoonyesha mapambano yetu kimetuumiza mabondia wengi hasa mimi  balozi.

 

Hii ni baada ya bondia mwenzetu [anamtaja lina]kuishitaki Azam Media, hali iliyopelekea mabosi wangu wao kusitisha kuonyesha ngumi ”alisema Kiduku

 

Alipoulizwa kama hivi karibuni ana pambano lolote?, alijibu” Ndio tarehe 24 mwezi huu na cheza na bondia kutoka Malawi jijini Dar es salaam’ Shekidele karibu sana kwenye pambano hilo”alisema Mjuu huyo wa Mamaa wa Misuli Mc Rukia Ndege.

 

Kwa upande wake Chanzi Mbwana Maarufu ‘Pawa lranda’ambaye ni kocha mkuu wa Bondia Kiduku alisema.

 

“Azam tv kutoonyesha ngumi kumeathiri wengi wakiwemo Mapromota, mabondia na sisi makocha,  bondia  anapocheza mechi nyingi mbali na kocha kupata kipato, bado kuna faida ya bondia kupata umaarufu baada ya kuonekana kwenye Tv,

 

 Mfano hapa kwenye klabu yetu ya Moro Boxing tuna vijana wengi wanachipukia wanahitaji sapoti kubwa ya Azam Tv”alisema kocha huyo.

                   

No comments:

Post a Comment

MAKALA PLANET NDONDO CUP. SIRI DAMU CHAFU KUTWAA UBINGWA MARA MBILI MFURULIZO HII HAPA.

  Baadhi ya mashabiki waliofulika kwenye mashishindano hayo.                           .....Kikosi cha Damu chafu Mkuu wa Wilaya Mhe Kilakal...