Na Dustan Shekidele,Morogoro.
MPENDWA Msomaji leo tunaingia sehemu ya pili ya stori kali ya kitaa iliyoanza kuruka hewani juzi.
Kwenye stori hiyo tuliishia kipengele cha kuwaomba Viongozi wa dini Mikoa yote Tanzania kuweka wataalamu wa Lugha za alama kwenye lbada zao ili kuwapa haki ya msingi walemavu ’Viziwi’ kusikia Mahuribi, Mawaidha na Matangazo muhimu yanayotolewa kwenye lbada.
MANUNG’UNIKO YA BAADHI YA VIZIWI.
Mwandishi wa habari hizi amejaliwa na Mungu kupata kibanda cha kuishi ambapo kwenye kibanda hicho pia amejaliwa kupata Mpangaji Baraka Simon na mkewe Blenda Martin wote ni ’Viziwi’ hawasikii wala kuongea
Mwanaume ni mfanyakazi wa SUMA JKT kItengo cha Ujenzi na mkewe ni Mama wa nyumbani, wamejaliwa kupata mtoto mmoja wa kike waliyembatiza kwa jina la Glory ambaye kwa ukuu wa Mungu sio ‘kiziwi’ anaongea na kusikia.
Wanandoa hao waliofunga ndoa kwao Dodoma takribani miaka 7 iliyopita ni waumini wa kanisa kuu la Anglikana lililopo ’Round-About’Mzunguko wa barabara za SUA.Kenyata. Madaraka na Kingo katikati ya Mji wa Morogoro kila Jumapili hungana na waumini wenzano kumuabudu Mungu kwenye kanisa hilo.
Mara baada ya mtoto huyo kubatizwa baadae Devary Martin ambaye ni shemeji wa Baraka alitoka Dodoma kuja Morogoro kumsalimia dada yake hivyo, Mwandishi wa habari hizi alimtumia kama mkalimani kwenye mahojiano na Baraka.
Akisimulia ugumu walioupata kwenye mchakato wa kumbatiza Mwanae Baraka alisema.
“Mimi na mkewe wangu kama unavyotushudia kila jumapili tuna kwenda kanisani, bahati mbaya sana kwenye kanisa letu hakuna mtu tunayewasiliana naye kwa alama za Vidole lakini hilo halituzuii kwenda kumuabudu Mungu wetu ambaye huwa tunawasiliana naye kmya kimya.
Kwa kutokuwepo mtaamu wa Lugha za alama hakuna tunachosikia kwenye lbada huwa tunafuata mkumbo tu watu wakisimama na sisi tunasimama wakiinuka kutoa sadaka na sisi tunainuka.
Changamoto kubwa ni kwenye matangazo mara nyingi huwa tunapitwa na vitu vingi kanisa mfano linaweza kutoka tangazo la mabadiliko ya saa ya ibada jumapili ijayo sisi hatujui tunakuja muda ule ule wa kawaida hatukuti mtu basi tunaludi nyumbani”alisema Baraka na kuongeza
Kubwa zaidi tumejaliwa kupata huyu mtoto tangazo la ubatizo limetoka siku za nyuma licha ya sisi kuweo kanisa hatukusikia kwa sababu hakuna wa kutuambia jumapili iliyofuata tumeshuhudia wenzetu wanabatiza watoto wao.
Tukaomba kwa wazee wa kanisa bahati nzuri tumekubaliwa mtoto wetu kabatizwa bila sisi wazazi wake kufanya maandalizi ya tukio hilo kubwa kiimani, mfano amekosa kumbukumbu ya picha kama tungelijua mapema tungekuambia wewe uje kumpiga picha”alimalizia kusema Baraka.
Kwa upande wake Devary alisema”Kwanza nakushukuru sana kwa hili unalolifanya ya kuwaseme wasio nasauti Shemeji yangu ana Tv kila siku wanasikilia Mwamposa ambaye kwenye Tv yake amuweka mtaalamu wa Lugha za alama, wakiwa peke yao wanatoa sauti kwenye Tv wanamtazama mkalimali tu.”alisema
Ifahamike Baraka anajimudu kidogo kifedha tunaamini kama angesikia tangazo hilo mapema angefanya maandalizi ya tukio hilo ikiwemo kuwaalika ndugu zake kutoka kwao Dodoma.
Ili kupata ufafanuzi wa jambo hili mtetezi wawanyonge aliwatafuta Viongozi wa dini Msaidizi wa Askofu Wilson Mafumbi na Shehe Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Shehe Jafar Thinei ambao kwa pamoja wamefunguka mazito.
Majibu yao yatarukam hewani hivi punde hivyo endelea kuwa jirani na Mtandao huu muda wote.
No comments:
Post a Comment