Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Monday, March 10, 2025

MAMA ASIMULIA MAZITO BAADA YA KUTOKA CHUMBA CHAUPASUAJI NA MWAE ALIYEANGUKIWA NA UKUTA.

Gresi Kaloli akizungumza na Mtandao huu huku akiwa na  na Mwane
       Dent Mwahawa Mohamed baada ya kutoka hospital
                           Mwenyekiti wa Mtaa Marry Kachale

                  Shuhuda Mariamu Athuman akiangalia ukuta huo


   Na Dustan Shekidele,Morogoro.

MAMA wa Dent wa  la 3 aliyeangukiwa na ukuta Bi. Gresi Fred Kaloli, amefunguka mazito baada ya kutoka  chumba na upasuaji[Thieta]na Mwanae Mwanahawa Mohamed Mkumba[10laliyeangukiwa na ukuta wiki iliyopita.

Juzi Mtandao huu uliripoti tukio hilo na kuahidi kuendelea na habari hii kwa kuzungumza na Mama mzazi wa Dent huyo ambaye wakati habari hiyo ikienda mitamboni Mwanafunzi huyo anayesoma dasara la tatu shule ya Msingi Mtawara Mkoani hapa alikuwa Thieta akipigania uhai wake.

Kwa Rehema za Mwenyezimungu Dent huyo aliyefanyiwa upasuaji mara mbili wa kutolewa damu chafu iliyoganda mwilini baada ya kuangukiwa na ukuta uliopo jirani na nyumbani kwao Alhamisi ya Februari 21.

  Baada ya kutoka Thieta mahojiano  na Mama huyo yalikuwa hivi.

Mwandishi. Awari ya wote pote kwa mkasi mzito uliomkuta Mwanao, ama baada ya salamu na pole kwa faida ya wasomaji wa Mtandao pendwa wa Shekidele naomba ujitambulishe majina yako kisha utueleze A-Z tukio hilo.

Mama wa Dent. Asante kwa kutupa pole pia tunashukuru kwa sababu umekuwa Mwandishi wa habari wa kwanza kuja kutupa pole na kutuhoji kuhusiana na ajali hiyo iliyompata mtoto wangu.

Siku ya tukio Alhamis kama kawaida Mwanangu Mwanahawa Mohamed Mkumbwa mwenye umri wa miaka 10 anayesoma darasa la tatu Shule ya Msingi Mtawara aliamka saa 12 kufanya maandalizi ya kwenda shule.

Wakati huo mimi nilikuwa kitandani nimelala, ghafra nasiki vilio na makelele nikakarupuka  nilivyotoka nje nimemshuhudia mwanangu ameangukiwa na ukuta wa jirani,

Kama mzazi baada ya kushuhudia kundi la watu wakihangaika kumchomoa mwanangu kwenye kifusi tumbo la uzazi lilinikata nikaanguka chini kwa bahati wasamalia wema hao walifanikiwa kumtoa mwanangu akiwa hai tukakodi boda boda boda tukamkimbiza hospital.

Baada ya masaa 3 mbele nilimuona mwanangu akizidi kuregea nilipomtazama zaidi nilishuhudia macho yake yakiwa meupe kama pamaba, baada ya kumchunguza madaktari wamebani damu imefia ndani ya mwili, hivyo waliamua kumfanyia upasuaji kutoa damu chafu iliyoganda na kumuweka damu mpya”alisema Mama huyo na kuendelea

“Mwanangu alitoka Thieta siku iliyofuata ambayo nasiki ulikuja hapa hospital kutuona aliingizwa tena Thieta kufanyiwa upasuaji wa pili baada ya sehemu ya mgongoni nayo kuvia damu chafu.

Nashukuru jana tumetoka hospital kama unavyoona muda huu nimetoka kumsafisha kwenye majeraha” haya ndio maelezo yangu

Mwandishi. Umetumilia shilingi ngapi kwenye matibanu  na huyo mwenye ukuta amechangia kiasi gani?

Mama wa Dent. Mpasa sasa gharama zote ni Laki 7 na nusu nab ado tunatumia usafiri wa kwenda hospital kila siku kuchukua dawa na kusafisha vidonda, huyo Mwenyeukuta baada ya kubanwa sana ametoa laki moja toka atoe hiyo laki sijamuona tena kuja kutuona,kipekee na washukuru madaktari na wauguzi wa hospital ya Mkoa kwa kupigania uhai wa mwanangu pili  nawashukuru watu mbali mbali walionichangia kwenye matibabu hasa Mama Nyau mke wa diwani wetu pamoja na Mwenyekiti wa Mtaa Mama Marry Kachale wamejitoa sana mwisho niwashukuru wananchi waliopambana kumchomoa mwangu kwenye ule ukuta.

Mwandishi. Taarifa nilizozipata eneo la tukio zinadai ukuta ule wa Tofari za kuchoma ulikuwa hatarishi muda mrefu kwa nini uliruhusu Mwanao mara kwa mara akasugue miguu kwenye jiwe lililopo chini ya ukuta huo hatarishi?

Mama Dent. Ni kwelie ukuta ule ulikuwa unaufa mkubwa na ulikuwa umepinda tulimjulisha  huyo jirani yetu mwenye nyumba[Anamtaja jina] lakini hakuchukua hatua yoyote wengine waliamua kwenda kumshitaki kwa mwenyekiti lakini bado hakuufanyia matengenezo mpaka ulivyomuangukia mwangungu.

Kuhusu kumuacha mwangu asugue miguu pale kama ambavyo nilikuambia awari wakati tukio linatokea mimi nilikuwa ndani nimelala hivyo sikumuona akisugua miguu pale.

Mwandishi Ok asante kwa ushirikiano.

Mtandao huu kwa sasa unahifaddhi jina la Mmiliki wa ukuta huo kwa sababu haja patikana kuzungumzia jambo hilo juhudi za kumtafuta zinaendelea.

Baada ya kumsikia Mama huyo Mwandishi wa habari hizi aliludi tena kwa Mwenyekiti wa Mtaa Mama Marry Kachale na Mahojiano yetu yalikuwa hivi.

Mwandishi. Samahani Mwenyekiti swala hili awari ulisharizungumzaia lakini baada ya kuzungumza na Mama wa Mtoto nimepata maswali ambayo nahitaji majibu kutoka kwako.

 Je kama mkuu wa ulinzi na Aman kwenye    Mtaa wako  tukio hili umelipoti polisi?

Mwenyekiti. Ndio baada ya tukio nilimpigia OCD sikumpata nikampigia RPC nikamueleza akaniambia ataniunganisha na Askari wa chini yake aje eneo la tukio.

Mpaka muda huu sijamuona huyo Askari kwa sasa tuko bize na mgonjwa Mungu akisaidia akipata nafuu tutalifuatilia jambo hilo nitakupa mrejesho Shekidele.

Mwandishi. Ok asante na hongera kwa kujitoa kwenye shida za wananchi wako.

Mwenyekiti. Asante hongera na wewe kwa kazi nzuri unayoifanya ya kuripoti habari za kijamii.

 

No comments:

Post a Comment

LIGI YA MABIGWA BARA LA ULAYA.ARSENAL AMFANYIA KITU MBAYA BINGWA MTETEZI

              Na Dustan Shekidele. WASHIKA Bunduki wa Jiji la Maraha la London nchini England Arsenal   usiku wa leo imeishangaza duni...