Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Wednesday, January 1, 2025

KIBABAGE AIPELEKA ‘GUSA ACHIA TWENDE KWAO’ MOROGORO.

Nickson Kibabahe mwenye jezi nyeupe akiwa na baadhi ya wachezaji aliocheza nao utotoni.
.......Kibabage jezi no 3 akikiwasha kwenye gemu ya timu Kibabage na timu ya Mti Mchungu Fc
........Kibabage akizungumza na Mwandishi wa Mtandao huu mara baada ya gemu hiyo kutamatika




.....Kibabage akiendelea kukiwasha kwenye gemu hiyo




 Kibabage bakiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa timu zote mbili


                  Na Dustan Shekidele,Morogoro.
HABARI ya Mujini kwa sasa ni ‘Gusa AchiaTwende Kwao’ Mwendo wa 5G.

Beki kilaka wa Yanga Nickson Kibabage Mkazi wa Mawezi Kata ya Kiwanja cha Ndege Morogoro, ameipeleka Gusa Achia nyumbani kwao Morogoro. 

Mara baada ya Mabingwa hao wa kihistoria ‘Wazee wa Supu’ wenye Maskani yao Makutano ya Mitaa ya Twiga na Jagwani Kariako, kuichapa Fountain Gate mabao 5-0 Juzi uwanja wa KMC Mwenge Dar.

Kibabage aliyekuwa sehemu ya gemu hiyo alipiga gia gari yake na kuja nyumbani kwao Morogoro siku iliyofuata yaani Jana Kibabe aliwakusanya wachezaji aliocheza nao Mtaani kwao, Moro Kids na Mtibwa Sugar wakaunda timu waliyoipa jina Timu Kibabage.

Baada ya Kibabage kuunda timu hiyo wakacheza gemu ya kirafiki na timu ya Mti Mchungu Fc uwanja wa Shule ya Msingi Saba saba Kata ya Kiwanja cha Ndege. 

Kwenye gemu hiyo iliyojaza umati mkubwa wawatu waliofika kumshuhudi kijana wa Mtaa kwao anayefanya vizuri Yanga.
Timu Kibabage walipoke kichapo cha bao 2-0 toka kwa Mti mchungu Fc inayoungwa na wachezaji wengi wa timu ya Moro Stars inayoshiriki Ligi daraja la Nne Wilaya ya Morogoro. 

Mara kadhaa kibabage akipogusa Mpira mashabiki hao wake kwa waume waliipa ‘Gusa Achia Twende Kwao’.
Gemu ilipotamatika Mwandishi wa habari hizi alizungumza na Kibabage alipotakiwa kueleza dhumuni la mchezo huo alisema.
”Nimechi ya kirafiki nimekusanya wachezaji niliocheza hao utotoni hapa Mtaani kwangu na wale niliocheza nao Moro Kids na Mtibwa Sugar”alisema 

Alipoulizwa Yanga wanajiandaa na mchezo wa Ligi ya Mabigwa Afrika dhidi ya TP Mazembe utakaopigwa Januari 4 Uwanja wa Mkapa Dar iweje yeye yuko Morogoro?

Alijibu. “ Mara baada ya gemu ya jana na Fountain Gate kutamatika tulipewa ruhusa ya siku 2 kwa maana ya Leo na kesho tunahitajika kulipoti kambini Januari Mosi, hivyo baada ya kupewa off jana hiyo hiyo nimekuja nyumbani Morogoro na leo nimeandaa mchezo”alimalizia kusema Kibabage.

Baadhi ya Mastaa walioshuhudiwa na Mwandishi wa habari hizi wakiitumikia timu ya Kibabage ni pamoja na Omari Manga Maarufu ‘Adebayo’ anayeitumikia Mtibwa B na George Chota anayeitumikia timu ya Mtibwa ya wakubwa inayoongoza Ligi daraja la kwanza kwenye mchezo wa juzi Mtibwa iliibuka na ushindi wa bao 3-0 huku Chota akifunga bao la 2.





  • No comments:

    Post a Comment

    MAKALA PLANET NDONDO CUP. SIRI DAMU CHAFU KUTWAA UBINGWA MARA MBILI MFURULIZO HII HAPA.

      Baadhi ya mashabiki waliofulika kwenye mashishindano hayo.                           .....Kikosi cha Damu chafu Mkuu wa Wilaya Mhe Kilakal...