Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Sunday, December 8, 2024

BAADA YA KUSOTA KWA MISIMU KADHAA HATIMAYE KILO NET IMENYAKUA UBINGWA WA SOKA MKOA WA MORO 24-25,


Mfungaji wa mabao hayo D Maria akizungumza na Mtandao huu.

 

  

 

Mh Kihanga akimkabidhi kombe Nahodha wa Kilo Net Carles Mrichi.

 Mh Kihanga akiwa katika picha ya pamoja na mabingwa hao wa mkoa.

  

      Na Dustan Shekidele Morogoro.

Subra ni lbada na Mvumilivu hula mbivu.misomo hiyo imetimia jana kwa timu ya Kilo Net Fc kutwaa Ubingwa wa Ligi daraja la Tatu Mkoa wa Morogoro, baada ya kukosa kwa  misimu miwili ikifungwa kwenye faibali.

Kilo Net  Fc inayomilikiwa na Taasisi ya kukuza na kuibua Vipaji ya Kilombero Soccer Net Academy yenye maskani yake lfakara Wilaya ya Kilombero, imenyakua ubingwa huo kwa mara ya kwanza baada ya kuwafunga majirani zao Usalama  Fc kutoka Wilaya ya Ulanga.

Katika mchezo huo wa fainali uliopigwa  uwanja wa Jamahuri Manispaa ya Morogoro Kilo Net waliwanyuka Wanausalama hao kwa chuma 2-0.

 Huku mbao yote  yakifungwa na Haroun Tumbagani Maarufu D. Maria bao la kwanza akifunga dakika ya 10  kipindi cha kwanza na la pili alilifunga dakika 88 ya kipindi cha pili na kupeleka majonzi kwa wanausalama hao.

Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Mkoa wa Morogoro’MRFA’ Jimmy Lengwe alisema timu 8 kutoka Wilaya zote 7 za mkoa wa Morogoro zilishiriki fainali hizo zilizoanza kutimua vumbi Novemba 29 uwanja wa Saba saba Manispaa  ya Morogoro na kutamatika jana Desemba 5  uwanja wa Jamhuri.

” Awari Ligi hii ilichezwa kwa kanda 4  wilaya zote za Mkoa wa Morogoro kila kanda ikitoa timu 2  ambazo  ni Usalama kutoka Wilaya ya Ulanga.Challenge Fc na Cypilian Fc kutoka Wilaya ya Malinyi, Wallers Fc, Mang’ura Fc na Kilo Net kutoka Wilaya ya Kilombero  nyingine ni Mafisa United na   Morogoro Tanzanite Soccer Academy’MOTASO’ kutoka Wilaya ya Morogoro Mjini yenye muunganiko na Wilaya ya Morogoro Vijijini”alisema Lengwe.

Kwa upande wake Mgeni rasmi wa fainali hiyo  Mstahiki Meya wa Mji wa Morogoro Mh Pascal Kihanga ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Mazimbu na Mwenyekiti wa chama cha Soka Mkoa wa Morogoro.

Kwenye hotuba yake aliwataka mabingwa hao  kuanza mapema maandalizi wa michuano ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa na kuuwakilisha vyema mkoa wa Morogoro.

Mtandao huu umekusanya matukio mengi kwenye fainali hiyo hivyo usicheze mbali na mtandao huu.



No comments:

Post a Comment

MAKALA PLANET NDONDO CUP. SIRI DAMU CHAFU KUTWAA UBINGWA MARA MBILI MFURULIZO HII HAPA.

  Baadhi ya mashabiki waliofulika kwenye mashishindano hayo.                           .....Kikosi cha Damu chafu Mkuu wa Wilaya Mhe Kilakal...