Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Thursday, October 3, 2024

WANANCHI MORO WAJITOKEZA KWA WINGI KUMZIKA MWANAMUZIKI RHUMBA BOY.

Rhumba Boy akicharaza Drum za band ya Mikumi Sound.
Azazi Seleman Kondo Mtoto mkubwa wa marehemu
                      Mwili ukiwasili nyumbani kwa marehemu
......ukiwa kwenye gari tayari kw akuelekea Mmbete
  umati wawatu uliofurika jana kushiriki mazishi ya Mpendwa wetu Rhumba Boy.

Rhumba Boy enzi za Uhai wake akicharaza Tumba za band ya Waluguru Og.


                    Na Dustan Shekidele,Morogoro.

WANANCHI Mkoa Morogoro  wamejitokeza kwa wingi jana kumzika Msanii Maarufu wa Muziki wa Dansi nchini Kondo Seleman Rhumba Maarufu ‘Rhumba Boy’.

 Marehemu Rhumba ambaye miaka ya 90 alifanikiwa kutwaa ubingwa wa kusakata Disko Mkoa wa Morogoro, alifariki dunia juzi Octobar 1 na kuzikwa jana kwenye makaburi ya familia yao  yaliyopo eneo la Mmbeta Keleka Juu ya  Milima ya Uluguru.

Baada ya kuachana na kusakata Disko hayati Rhumba  aliyejaliwa vipaji vingi na Mwenyezi Mungu alitimkia kwenye muziki wa Dansi na kuzitumikia band mbali mbali za Mkoani Morogoro kama vile Waluguru Original, Maisha Mapya Misic Band na Mikumi Sound, band aliyoitumikia hadi umauti unamkuta.

Kwenye band hizo Rhumba  alikuwa akitunga nyimbo  na kuziimba yeye mwenyewe miongoni mwa nyimbo hizo ni wimbo wa Ua jekundu. Kama hiyo haitoshi Rhumba Boy akikuwa na uwezo wa kupiga Drum huku anaimba, kupigaTumba, Gitaa la Bass na kucheza shoo’ kudensi’

Kwa sasa band  ya Mikumi Sound inayotamba na kibao chake cha ‘Mama Mkwe Kisa gani’inayomilikiwa na Mgos Josse Kigenda imehamia Turiani Wilaya Mvomero. 

Mwandishi wa habari hizi aliyekuwepo msibani  nyumbani kwa marehemu Mitaa ya Mafisa [4 Ways] jirani na daraja la Kichangani alishuhudia mastaa kibao wakijitokeza kumzika Staa mwenzao.

Kama kawaida Mpiga Picha wa Mtandao huu alifanikiwa kuwachapa mapicha Mastaa hao ambapo picha zao zitaruka hewani hivi punde hivyo endelea kuwa jirani na Mtandao huu muda wote. 

                       WASIFU WA MAREHEMU.

Kwa bahati mbaya wasifu wa marehemu haukusomwa kwa sababu za ufinyu wa muda, baada ya mwili kuwasili majira ya saa 6 mchana ukitokea Moswari uliswaliwa hapo hapo nyumbani kisha kuingizwa kwenye gari tayari kwa safari ya  kuelekea Mmbeta kumpunzisha kwenye nyumba yake ya Milele.

Ili kukamilisha habari hii kwa kupata historia ya Marehemu,Mtandao huu ulizungumza na Aziza selema Kondo ambaye ni Mtoto mkubwa wa marehemu.

 Alipotakiwa kuelezea wafisu wa mpendwa  baba yake alisema.

”Kwa niaba ya familia  tunakushukuru SANA Shekidele kwa sapoti yako kwenye msiba wa Mpendwa baba yetu.

             Wasifu wa baba.

Alizaliwa miaka 50 iliyopita na alisoma shule ya Msingi Mwembesongo, alipomaliza elimu ya Msingi alijihusisha na sanaa ya kucheza Disko  hadi umauti unamkuta alikuwa Mwanamuziki wa band ya Mikumi Sound..

Marehemu baba ameacha watoto 6 na wajukuu 11” alisema Aziza.

Siku chache kabla ya kuanza kuugua Rhumba Boy alikutana na Mwandishi wa Mtandao huu maeneo ya Mji Mpya  akasema. 

"Shekidele ngoja niwaandae watoto zangu 6 na wajukuu zangu 11 nikuite unipige nao picha ya pamoja kama kumbuku"  tamanio lake hilo halikutimia hadi mauti inamkuta

                     

 

 



 

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...