Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Monday, October 14, 2024

UDAKUZI SPESHO. MAMA AMSHANGAA MWANAE ALIYETOA SADAKA NYINGI KANISANI

Mwandishi wa habari hizi akimhoji Askofu Jacob Ole Maneo wa KKKT Dayosisi ya Morogoro.  

 

 Mdakuzi akizungumza na Askofu Teresphori Mkude wa Kanisa la Roman Dayosisi ya Morogoro. 

Kwa sasa Askofu Mkude amestaafu cheo hicho cha Uaskofu.


  Mdakuzi akimhoji Mwimbaji Maarufu wa nyimbo za lnjiri nchini Stara Thomas

              

  Na Dunstan Shekidele,Morogoro. UKISTAAJABU ya Mussa, hutoyaona ya Firahuni.

 Msemo huo umetimia jana  kwenye lbada ya Sakrameti ya Ekaristi kufuatia Mzazi kumshangaa mwanae aliyetoa kiwango kikubwa cha sadaka.

Tukio hilo limetokea Jana Jumapili Mkoani hapa,kwenye lbada hiyo iliyofanyika kwenye moja ya kanisa Kongwe nchini, jina linahifadhi kwa sababu za kiudakuzi.

            ISHU ILIKUWA HIVI.

Mdakuzi aliyekuwepo kanisani hapo mara baada ya kutamatika kwa lbada hiyo iliyojaza umati mkubwa wawatu kufuatia uwepo wa tukio hilo la madent zaidi ya 100 kupokea  Sakrameti hiyo Takatifu yenye msingi wa kulijenga kanisa la kesho kwa lmani ya Dhehebu hilo.

Mara baada ya kutamatika kwa lbada hiyo mmoja wawahitimu hao alilakiwa kwa basha na Mama yake  huku akimvisha taji baada ya kumaliza masoma hayo ambayo ni dira kwenye maisha yake ya kiimani.

Baada ya kutamatika kwa zoezi hilo la pongezi Mama huyo aliyesindikizwa na kundi la Mashosti zake waliong’ra kwa sare  za madera ya rangi ya mawingi,alimuamulu bint yake huyo amkabidhi ile  elfu 10 ya usafiri ili aite Bajaj warejea nyumbani kuendelea na sherehe.

 Bint huyo alimwambia Mama yake  kwamba elfu 20  aliyomkabidhi  ya sadaka na usafiri ameitoa yote sadaka.

”Ngoja kwanza nicheke, shoga zangu  huyu Mtoto asubuhi tumemkabidhi elfu 20 kwa mgawanyo kwamba elfu 5 ni zawadi ya padri, elfu 5 nyingine ni Sadaka na elfu 10 ni nauli ya Bajaj.

 chaajabu elfu 20 yote kaitoa sadaka sasa ataludi nyumbani na miguu”alisema Mama huyo.

Kufuatia kauli hiyo mmoja wa mashoga wa mama huyo alibeba jukumu la kumhoji mtoto huyo akimuliza ni kwa nini amekiuka maagizo ya Mama yake.?

Kwa ujasili mkubwa huku akijiamini mtoto huyo alijibu.”Nimekiuka maagizo hayo kwa sababu ya msimamo wa imani yangu iliyojengwa na mafundisho haya ya Ekaristi.

Kama hiyo haitosho leo kwa mara ya kwanza   nimeungama  baada ya kuungama tumetangazima kwamba kuna sadaka ya ziada ya kuwapa motisha makatekista wetu waliotufunisha zaidi ya mwaka hapa kanisani.

Hivyo kwa kuwa sikuwa na pesa nyingine zaidi ya ile elfu 10 ya nauli niliamua kuitoa  kwa lengo la kuilinda  imani yangu niko tayari kutembea kwa Miguu kuludi nyumbani”alisema Mtoto huyo.na kupokea zawadi ya Makofi na Vigeregere kutoka kwa kundi la watu walimshangaa kwa kutoa sadaka hiyo.

Maneno hayo yaliyojaa uzito mkubwa yalimgusa  Mama mzazi wa binti huyo, mdakuzi alimshuhudia mama huyo  akiluika huka kwa furaha sambamba na  akimbeba juu juu mwanae huku akisema kwa kiwango hicho cha lmani amefanya vizuri kutoa hiyo elfu 10 kuwapa zawadi waliofanya kazi kubwa ya kumuimalisha kiimani.  

Kwa furaha Mama huyo alifungua pochi na kutoa elfu 10 nyingine akaita Bajaj wakapanda na kuondoka zao

                    

 

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...