Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Thursday, May 30, 2024

DIWANI VITI MAALUMU AGAWA KADI 100 OFISI YA CC KATA YA MAFIGA AKITEKELEZA MAAGIZO YA UWT TAIFA.


Mhe Latifa Kulia akimkabidhi kazi 100 za CCM Mwenyekiti wa UWT Kata ya Mafika Tabitha Justo
......Mhe Latifa akizungumza na wana wajumbe wa UWT Kata ya Mafiga


 Baadhi ya wajumbe wakimsikiliza kwa umakini Mhe Latifa


                            Na Dustan Shekidele,Morogoro.

MIKAKATI ya kukiimarisha chama, Diwani  Viti Maalumu kwa leseni ya CCM Mhe Latifa Ganze juzi amegawa kadi 100 kwa Uongozi wa UWT Kata ya Mafiga, ikiwa ni maagizo ya UWT Taifa kuwataka viongozi wa Kata zote nchini kusaka wanachama wapya kwenye maeneo yao. 

Akikabidhi kadi hizo kwa Mwenyekiti wa UWT Kata ta Mafiga Tabitha Justo, Mhe Latifa alisema kwenye moja ya Vikao vya UWT taifa Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo taifa Marry Chatanda aliwaagizo viongozi wote walioshiriki kwenye kikao hicho kugawa kazi kwa Viongozi wa Kata kwa lengo la kusaka wanachama wapya.

“ Hii ni maagizo ya Viongozi wetu wa juu, kwenye moja ya vikao vilivyofanyika Dodoma walituagiza kuhamasisha viongozi kata na matawi kusaka wanachama wapya, leo nimewakabidhi kadi hizi 100 kwa lengo la kuzigaw akwa wanachama wapya kama zitakwisha mapema nipigieni simu muda wowote nitawaletea nyingine hata mkitaka kadi elfu moja nawaleta lengo letu ni kuzidi kukiimalisha chama chetu”alisema Mhe Latifa.

Kwa upande wake Mwenyekiti Tabitha mara baada ya kupokea kadi hizo alimuahidi Mhe Latifa kutekeleza maagizo hayo ya chama kwa kusaka wanachama wapya kwenye kata yao na kuwakabidhi kadi hizo.

Ifahamike kwamba Mhe Latifa kabla ya kunyakua nafasi hiyo ya Udiwani wa viti Maalumu Jimbo la Morogoro alikuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana [UVCCM] Wilaya ya Morogoro akiitumikia Jumuiya hiyo ya kwa Weledi Mkubwa kabla ya kutoka kwenye jumuiya hiyo kwa kanuni za Umri.

Kwa mafanikio aliyoyaonyesha UVCCM Wapiga kura wa Viti Maalumu hawakusiti kupiga tiki kubwa kwenye jina la Mhe Latifa na kuibuka kidedea kwenye nafasi hiyo .

Moto aliouwasha UVCCM anauendelea kwenye Udiwani  huku wachambuzi wa mambo wakimtabilia makubwa kwenye safari yake hiyo ya Uongozi wakitembea kwenye historia yake ya nyuma na sasa.

Tuesday, May 28, 2024

HII IMEKAA POA SANA. DIWANI VITI MAALUMU ATENGENEZA AJIRA KWA WANANCHI.

Diwani wa Viti Maalumu jimbo la Morogoro Mhe Latifa Ganzel akizungumza na wana UWT Kata ya Mafika leo jioni.

Mgeni Rasm kwenye hafra hiyo Diwani wa Kata ya Mafiga Mhe Mchungaji Thomas Butabile akizunguna
Mwenyekiti wa UWT Kata ya Mafiha Tabitha Justo naye akizungunza kwenye hafra hiyo.

Baadhi ya wajumbe wa UWT Kata ya Mafiga wakimsikilzia Mhe Latifa kw aumakini mkubwa
.....Mhe Lafika kulia  akishirikiana na Viongozi wa tawi la Misufini kufungua Cherahani hiyo

....Mzingo sio mtumba ni mpya kabisa Mhe Latifa akichana manaironi kwenye cherehani hiyo


.....Mhe Latifa akimkabdihi cherehani Mwenyekiti wa tawi la Misufini Johan Ahmed Mahimbi mwenye frana ya mistari stari

.... kkwa furaha wana UWT Kata wakimuao Mhe Latifa baada ya kuwakabidhi cherehani hiyo
.....Mwenyekiti wa tawi la Misufini Jahari akimshukuru Mhe Latifa kwa kuwakabidhi Cherehani hiyo
Kutoka kulia ni Katibu wa UWT Kata Farida Rajabu, Mwenyekiti wa UWT Kata Tabitjha Justo. Mhe Diwani Latifa Ganzel na Mwisho kushoto ni Mhe Diwani wa Kata ya Mafiga  Mhe Mchungahi Thomas Butabile


Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

DIWANI wa viti Maalumu kwa leseni ya Chama Cha Mapinduzi’CCM’ Jimbo la Morogoro Mhe Latifa Ganzel, ameitendea haki lrani ya chama chake kwa kutengeneza ajira zaidi ya 100, baada ya kugawa mitambo ya kutengeneza sabuni na cherehani kwa matawi manne ya UWT Kata ya Mafiga,

Msaada huo umechangia kwa kiasi kikubwa kutoa ajira kwa wanachama hao wa Matawi ya Manzese, Tanki la Zamani.na tawi la Zahanati ambapo matawi hayo siku za nyuma aliyakabidhi mitando hiyo ya kutengeneza sabuni,na kwamba leo Mei 28 Mhe Latifa ambaye pia ni Mrezi wa UWT kata ya Mafiga amehitimisha ahadi yake kwa kuwakabidhi cherehami Mpya tawi Misufini.

Akizungumza kwenye hafra hiyo iliyofanyika kwenye viwanja wa CCM Kata ya Mafiga Mwenyekiti wa U.W.T Kata ya Mafiga Tabitha Justo, alimshukuru Mhe Latifa kwa kutimiza ahadi yake kwa asilimia mia moja.

” Kwenye ziara yako ndani ya kata yetu ulihadi kutoa Vifaa maalumu vya kutengeneza sabuni kwa matawi 3 , hukuchukua muda mrefu ukatekereza hadi hiyo na kwamba kwa sasa kwenye kata yetu tuna mradi wa kutengeneza sabuni uliotoa ajira kwa watu mbali mbali hata wasio kuwa wana CCM.

Leo umekamirisha hadi yako kwa kuwakabidhi Cherehani tawi la Misufini hongera sana Mhe Latifa hatuna chahakulipa ila hadi yetu kwako ni mitano tena kwako” alisema Mwenyekiti huyo.na kupokea zawadi ya makofi kutoka kwa wanachama wa UWT Kata ya Mafiga huku wakiendeleza wimbo huo wa mitano tena kwa Mhe Ratifa.

Naye Diwani wa Kata ya Mafiga Mchungaji Thomas Butabile aliyekuwa mgeni rasmi kwenye hafra hiyo awari alimpongeza Mhe Latifa kwa kutekeleza ahadi yake kwa matawi yote manne ya CCM Kata ya Mafiga.

“ Mhe Ratifa anakipawa cha uongozi hata kwenye vikao vyetu vya baraza la Madiwani michango yake mingi imekuwa na tija kwa Jimbo letu la Morogoro,wana U.W.T kata ya Mafiga hongeni sana mmepata mrezi bora mwenye viwango wa TBS na mimi kama Diwani wa kata hii najivunia Mhe Latifa kuwa mrezi kwenye moja ya Jumuiya zangu za kata”alimalizaia kusema Mhe Mch, Butabile.

Akizungumza mara baada ya kumkabidhi cherehani hiyo mwenyekiti wa Tawi la Mifusuni Johari Ahmed Mahimbi Mhe Ratifa ambaye kitaaruma ni Mwandishi wa habari aliwapongeza viongozi wote wa matawi ya Manzese, Tanki la zamani na Zahanati kwa kuendeleza kwa weledi mradi huo wa Sabuni unaoendelea kukua siku hadi siku.huku akiwaomba viongozi wa tawi la Misufini kuiga mfano wa wenzao kwa kuendelea kwa weledi Mradi huo wa ushanaji nguo kupitia Mtambo huo wa Cherehani.

Mwisho Mhe Ratifa alitoa maelekezo aliyopewa na Mwenyekiti wa UWT Taifa Marry Chatanda kwa wanachama na Viongozi wa UWT Kata ya Mafiga. kwenye maelekezo hayo Mhe Latifa aliwakabidhi na dhana za maelekezo hayo wa Big Boss wa UWT Taifa zana hizo na maelekezo hayo kwa pamoja vitaruka hewani hivi punge hivyo endelea kuwa jirani na Mtandao huu muda wote kujua maelekezo hayo.

Saturday, May 25, 2024

SALA YA LEO JUMAPILI YA MEI 26.

 

“ Bwana nifanye  chombo cha amani yako.Palipo na Chuki,nipande Upendo,palipo na madhara nipande Msamaha.

Palipo na shaka nipande lman,palipo na kukata tama nipande tumaini,palipo na giza nipande Mwanga.

Palipo na huzuni nipande furaha,kwa jina la Mwenyezi Mungu ninaomba hiv.

Sote tuseme Amen”.

Jumapili ya Leo nimekuja kivingina sikunukuu mstari wowote kwenye kitabu kitakatibu cha Biblia badala yake nimekuja na sala hii inaotupa faraja watu wote wenye changamoto mbali mbali za kimaisha na kiimani.

Kwa msaada wa MUNGU naamini sisi wenye changamoto hizo sala hii itatupa Tumaini na faraja mpya tumtegemee na kumuamini Mungu siku zote za maisha yetu.


 

Friday, May 24, 2024

KOCHA WA WACHEZAJI NYOTA WA SIMBA, YANGA NA AZAM, ATOA NENO KWA KIPAJI CHA DOGO MACHUMA.

Mwandishi wa Mtandao[kati]akizungumza na Ticha Mau[kushoto] huku dogo Abdallah Omary Machuma [kulia] akisikiliza mahojiano hayo.

 Machuma akizungumza na Mtandao huu majuzi mara baada ya kufunga mabao 2 kwenye mchezo wa robo fainali ya michuano ya Ramadhan Cup dhidi ya JL Academy ya Kihonda Maghorofani.

 

      Na Dustan Shekidele,Morogoro.

KOCHA Maarufu nchini anayetajwa kwa sasa kuongoza kuibua na kuendeleza vipaji vya wachezaji wengi nchini, wakiwemo wachezaji wa Yanga, Simba na Azam.Ticha Hussein Mau amefunguka mazito juu ya kipaji cha mchezaji Abdallah Omary Machuma.[16].

 Mtandao huu jana  uriripoti habari za mchezaji huyo na kuahidi  kuendelea na stori hiyo Leo kwa kuzungumza na kocha Mkuu wa taasisi ya kuibua na kukuza vipaji ya Morogoro Tanzanite Soccer Academy ticha Hussein Mau.

Kwenye mahojiano hayo yaliyofanyika juzi ndani ya Uwanja wa Saba saba wakati michuano ya Ramadhan Cup ikiendelea, Mwandishi wa habari hizi alitaka jua namna kocha Mau alivyokiona Kipaji cha mchezaji huyo na kukizungumzia kwa undani.

Kocha Mau alijibu Maswali hayo kama ifuatavyo.

”Taasisi yetu kila Mwaka tunazunguka kwenye Wilaya zote za Mkoa wa Morogoro kusaka Vipaji, tulikwenda Kilosa eneo la Dumila tukapata wachezaji kadhaa wakati tukiwa kwenye Scaut Dumila Abdallah Machuma hakuwepo, eneo la tukio.

Siku iliyofuata baba yake kapata taarifa kwamba tulikuweo Dumila kusaka vipaji, kanipigia simu kaniambia anakijana wake anakipaji nikamueleza zoezi hilo kwa eneo hilo limeshapita hivyo kama anataka amlete mwenyewe hapa kituoni.

Kweli mzee huyo kamleta mwanaye kampangia chumba eneo la Chamwino baada ya kufanya naye mazoezi wiki moja tu  mimi na wenzangu tumebaini mchezaji huyu anakipaji, hivyo kama utaratibu wetu wa kituo tumempa fomu ya mkataba wa kujiunga na taasisi yetu kasaini”alisema ticha Mau na kuongeza.

“Toka ajiunge na kituo chetu mwaka 2020 licha ya kucheza nafasi ya kiunga mshambuliaji lakini ameshafunga mabao mengi, Shekidele wewe ni shahidi umeshuhudia juzi Machuma katupeleka nusu fainali baada ya kufunga mabao 2 yote kwa mipira ya faulo nje ya 18, yaani huyu dogo  ni fundi sana wa kufunga mabao ya faulo”alimalizia kusema ticha Mau na kumtabilia makubwa mchezaji huyo kwamba atafika mbali kisoka. 

Ticha Mau ambaye awari alikuwa taasisi ya Moro Kids kabla ya kujiondoa na kuanzisha taasisi yake hiyo ya Moro Tanzanite Soccer Academy, anaongoza kwa kuibua nakuendeleza vipaji vya wachezaji wengi nchini wakati akiwa Moro Kids, baadhi ya wachezaji hao ni pamoja na Dickson Job, Kibwana Somary, Nickson Kibabage, na Kipa Abuutwari Mshery[Yanga]. Mzamiru Yassin na Somary Kapombe[Simba] na Pascal Msindo Azam Fc.

Wengine ni Shiza Kichuya[JKT Tanzania] Masenga[Tanzania Prisons] Hamad Waziri ‘Kuku’[Singida Fountain Get] Hassan Kessy’Kidingile’[Tabora United] Zuberi Daby[Mashujaa ya Kigoma]  Nassir Kombo’Scobb’[Mtibwa Sugar] na Juma Abdul [aliyewahi kuzitumikia Yanga na Singida United kwa sasa sijui niite sigida gani kwani tayari kuna timu 2 za Singida zilizomeguliwa menguliwa na kuwa timu mbili tofauti].

                      

 Wachezaji wote hao kwenye simu zao huwezi kukosa namba za ticha Mau na wanapokuja rikizo Morogoro lazima walipoti kwa kocha wao huyo.

                      


 

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...