Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Sunday, April 14, 2024

MORO KIDS MUDA HUU WA SAA 8 MCHANA INACHEZA NUSU FAINALI HAUSUNG YA NJOMBE.

              Kikosi kabambe cha Moro Kids. 

 Msimamo wa makundi hayo kabla ya gemu zao za mwisho.


          Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

 Moro Kids ‘Wana wa pakaya’ kutoka Mji Kasoto Bahari Morogoro] leo saa 8 mchana huu wanacheza mchezo  wa Nusu fainali za ligi ya mabigwa wa Mikoa dhidi ya Hausung Fc ya Njombe kwenye uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.

Vijana hao wa Moro Kids kutoka Taasisi ya kukuza na kuibua Vipaji mkoa wa Morogoro inayotajwa kuongoza nchini  kutoa wachezaji wengi wanao ng’ara  timu mbali mbali za Ligi Kuu zikiwemo timu kubwa za Simba, Yanga na Azam.

Wakifanikiwa kushinda kwenye mchezo wa leo moja kwa Moja wanapanda Ligi daraja la Pili,  ikitokea kwa bahari mbaya wakifungwa  watabeba mabegi yao na kupanda basi la Shabiby Line na kurejea nyumbani   Milima ya Uluguru Vijiji vya Kinole, Mkuyuni,Kiloka Matombo, Mgeta, Nyandila, Dumila.Turiani Gairo.Kisaki.Mvua.Mikese Ngerengere, Kizuka na Bwawani .

 Kuwasaidia wazazi wao kuchimba  Magimbi na Mihogo huku wakisubiri  kujiuliza kwa mara ya pili kwenye mchezo wa Play Off dhdi ya timu zilizofanya vibaya  Ligi daraja la Pili.

Nusu fainali ya pili itapigwa leo hii saa 10 jioni kwenye uwanja huo huo wa Jamhuri kati ya wenyeji Gunnes Fc ya Dodoma wakipepeta na Arusha City macharii kutoka Jijini la kitalii la Arusha. [A-Town]

Ifahamike timu 4 zilizoshika nafasi mbili za juu kwenye kundi A na B zimetinga hatua hiyo ya 4 bora.

Timu hizo ni Gunnes na Moro Kids kutoka kundi A na Hausung na Arusha City kutoka kundi B.

 Kila lenye kheri kwa Wana wa Pakaya Moro Kids kwenye mchezo wa leo dhidi ya walima Maparachichi hao kutoka Mkoa wa Njombe unaoongozwa na Mkuu wa Mkoa Rafiki yangu Anthony Mtaka.

Kama kawaida matokeo ya Michezo hiyo miwli ya Musu fainali itaruka hewani kwenye mtandao huu hivyo uchekae mbali na Mtandao Pendwa wa Shekidele.

                   


No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...