Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Tuesday, April 30, 2024

MAONI YANGU MWENENDO MTIBWA SUGAR.



 

 

Baada ya jana Mtibwa Sugar kuokea kichao cha bao 2 kwa 1 dhidi ya JKT Tanzania mchezo ambao Mtibwa walikuwa na uwezo wa kuondoka hata na alama moja lakini kwa mshangao dakika ya 9o nikiwa kwenye Luninga naifuatilia timu yetu ya Morogoro.

Wana Morogoro  tumeumia  sana tukishuhudia Mtibwa ikufungwa  bao la 2 dakika ya 9o huku chanzo cha bao hilo ikiwa ni makosa ya mlinda mlango aliyetoa boko kwa kichuya na kuacha gori wazi.

 Kichuya baada ya kuona lango liko wazi kafumua shuti lililounganishwa wavuni na Six Sabilo.

Binafsi kuguza Mgonjwa siwezi, kwenye ukweli nasema ukweli  unaona kabisa Mgonjwa kazidiwa hata macho habwenzi, uji unamshinda kunywa,  kuhema kwake kama maji yanayotokota jikoni.

Wewe unayemuuguza nafsi yako inakushuhudia kabisa kwamba Mgonjwa wako  anakaribia kukata roho, unamtia moyo kwa kumwambia maneno ya Tumaini kwamba.

Mgonjwa wangu kuugua sio kufa, kweli hayo ni maneno ya faraja kwa mgonjwa   lakini hayatamsaidi kwenye safari yake ya kuelekea kwa Mungu.

kwangu mimi nikiona hivyo na mwambia ukweli, kwamba kila nafsi itaonja umauti na hakuna atakayeishi Milele  chini ya jua.

Hata mimi ninayekuugua muda wangu utafika nitaiacha hii duniani na kurejea kwa muumba wangu.

Hivyo ushauri wangu kwako mgonjwa wangu kwa hali ilivyo, tumia muda huu kutubu dhambi zako kwa mwenyezi Mungu, ili wakati wowote akikuita  maombi hayo yenye  toba. Yakusaidie mbele ya safari

            TIMU YA MTIBWA SUGAR.

Kwa mtibwa Sugar yenye Maskani yake katikati ya Mashamba ya Miwa eneo la Manungu Kata ya Mtibwa, Tarafa ya Turiani, Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro.

Kwa sasa taa ya Oil inawaka kwenye Dash Bord la gari lao, muda wowote gari lina Nock na kuzimika.

Kama ni boda boda Mtibwa wamevuta juu Chock  wanatembelea mafuta  ya Lizevu kwenye Kabreter ambayo hayajai hata kwenye kile kikombe cha kahawa muda wowote boda linazima kwa kukosa wese .

Mtibwa kwa msimu huu  imebadili makocha zaidi ya watatu,  walinda mlango zaidi ya 3,Kama hiyo haitoshi Mtibwa  msimu huu katika kuhangaika kujinusuru na janga la kushuka daraja kwenye usajiri wa dirisha dogo wamesajiri  wachezaji  zaidi ya 8,

Juhudi zote hizo hazikuza matunda bado timu inafungwa huku wakiukaribia mlango wa kushuka daraja wakikusanya alama  17 akiburuza mkia kwenye ligi hiyo yenye timu 16 huku wakibakiwa na michezo 7.

Kati ya michezo hiyo 7 kuna Simba watakao chezo nao keshokutwa Mei 3, bado na Yanga. Bado na Azam, bado na Tabora United.na Mashujaa ya Kigoma.

Mimi na hisi Mtibwa wanahangaika kunjoosha kivuli cha Mti ili hali Mti ndio wenye shida, tiba  ni kuukata huo mti.

  Mara baada ya mchezo wa jana kutamatika, Afisa habari wa Mtibwa Sugar Thobiasi Kifaru Ligalambwike akizungumza na Waandishi wa habari sehemu kubwa ya maelezo yake limtaja kiongozi wa zamani wa Mtibwa  Jamal Baizer akidai toka kiongozi huyo aondoke timu hiyo haina mwenendo mzuri.

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...