Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Saturday, March 16, 2024

MAAJABU MAWILI YA TREKTA.





 


           Na Dustan Shekidele,Morogoro.

Haya ndio Maajabu mawili ya gari aina ya Trekta ambalo shughuri zake kubwa ni kulima mashabani na mara nyingine mkulima anapovuna mazao yake anayatoa  majembe na kufunga Tella kusomba mazao yake kutoka shambani kuyapeleka nyumbani. 

    HAYA NDIO MAAJABU 2 YA TREKTA.

Juzikati Mwandishi wa habari hizi akiwa kwenye Pilikapilka zake za kusaka matukio alikatiza maeneo ya Mji Mpya na kushuhudia mafundi wakitengeza Trekta nje ya nyumba yao iliyopo Mtaa wa Makaburi ‘A’ jirani na Soko kuu la Kata y Mji Mpya.

Mafundi hao waliokubari kuzungumza kwa sharti la kutotajwa majina yao Popote walitaja  maajabu hayo.

Mosi. Trekta halina Chessis,ukilifungua linajigawa vipande vitatu, kwa maana ya mataili ya mbele, lnjini na mataili ya nyuma kama inavyoonekana Pichani likiwa na vipande hivyo 3 baada ya taili za mbele kutolewa.

Ajabu la Pili. Taili kubwa ya nyuma  licha ya ukubwa pengine kuliko taili la gari lolote chaajabu ujazo wa taili hilo ni  upepo 20 tu likibeba Tella ndio unaongeza kidogo  upepo 25, huku taili dogo la mbele linajaa upepo 60.

“ Kana unavyoshuhudia mwenyewe hapa tumeanza kutoa taili za mbele zile pale muda huu tunafungua injini ambapo kukishafungua inajitenge na taili za nyuma.

Trekta ni tofauti na magari mengine halina Chessis,Pili hili taili la nyuma ujazo wake wa upepo ni 20 ukibeba tella unajza 25, taili dogo la mbele ujazo wake wa Upepo ni 60”alimalizia kusema fundi huyo.

 Ujazo wa Pikipiki ya Mwandishi wa habari hizi taili la mbele ni 40 na taili la nyuma ni 50 hii ni kwa sababu ya kubeba watu na mizigo kwenye siti hiyo ya nyuma.

Pichani Mwandishi wa Mtandao huu akimbeba Meneja wa Uwanja wa CCM Kirumba wa Jijini Mwanza Mzee John Tegete, akimtembeza  Mitaa mbali mbali ya Mji wa Morogoro.

 lfahamike Mzee Tegete ni baba mzazi wa aliyekuwa mchezaji nyota wa Yanga na timu ya Taifa ya Tanzania’Taifa Stars’ Jerrson John Tegete.

 Kama hiyo haitoshi Mzee Tegete  alikuwa kocha Mkuu wa timu ya Tofo Afrika ya Mwanza wakati ikiwa ligi Kuu na baadae ligi daraja la kwanza.

 Kwa sasa taarifa zinadai timu hiyo ipo tena kwenye madaraja ya juu yamebaki majego yanayodaiwa kusababisha mvutano mkali baina ya Viongozi na Wanachama wa timu hiyo yenye undugu na Yanga .

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...