Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Thursday, January 18, 2024

KUMBUKIZI. MISS TANZANIA AGAWA VIFAA VYA MICHEZO MOROGORO.

Sitti Mtemvu akimkabidhi vifaa vya Michezo aliyekuwa mwenyekiti wa chama cha soko Wilaya ya Morogoro   Joseph Challo ‘Mnyausi’ kushoto mwenye nguo nyeusi ni katibu Mkuu wa Chama hicho Kafale Maharagande.
Sitti Mtemvu’Kulia akipozi mbele ya kamera ya Mtandao huu na Mama yake Mzazi Bi, Mariam Mtemvu Mara baada ya kukabidhi Vifaa hivyo.

 Mwandishi wa Mtandao huu akiwa uwanja wa Saba saba Mara baada ya ziara ya Sitti Mtevumvu kutamatika Mkoani Morogoro.


 MISS Tanzania wa Mwaka 2015  Mrembo Sitti Mtemvu Mara baada ya kunyakua Ulimbwende wa Miss Tanzania moja kwa moja alitinga  nyumbani kwao Morogoro na kugawa vifaa vya Michezo kwa Chama cha Soko Wilaya ya Morogoro.

Lengo la Mrembo huyo ni kuinua vipaji kwenye Mkoa wake unaotajwa kuongoza kwa Vipaji Mbali mbali nchini.

Baadhi ya Vipaji vinavyoendelea kutawara mkoa wa Morogoro ni pamoja na Soka,Kina Dickson Job, Kibwana Shomari, Aishi Manula. Shiza Kichuya, Mzamiru Yassini. Zawadi Mauya.  Kwa upande wa Muziki,Stamina, Afande Sele. Bell 9.

Ngumi sasa wapo Mabondia,Twaha Kiduku. Franciss Cheka, Cosmas Cheka na Misumari Mlapakona.

Wasanii wa Vichekesho kina Stan Bakora ‘Mkunde Simba’ na Mwisho Mwampamba’aliyetwaa ushindi wa pili wa Shindano la Big Brother Afrika’BBA’ Mwaka 2003 kwenye jumba la Sanaa nchini Afrika Kusini.

 Maswara ya Urembo sasa yupo mwenyewe Mluguru Mrefu kuliko wote  Sitti Mtemvu  zao la Mji Kasoro BahariMorogoro’

lfahamike baba Mzazi wa Sitti Mtemvu Mwanasiasa Maarufu nchini Mzee Abass Mtemvu ni Mzaliwa wa Mkoa wa Morogoro, ambaye kwa sasa ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi’CCM’Mkoa wa Dar es salaam.

 Awari Mzee Mtemvu miaka hiyo ya 2015 alikuwa Mbunge wa Jimbo la Temeke kwa leseni ya chama chake hicho cha CCM.

                        

 

 

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...