Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Monday, October 30, 2023

MWAKA MPYA MAMBO MAPYA. MWONEKANO MPYA KILAKALA SECONDARY


 


  Na Dustan Shekidele,Morogoro.

WAKATI Imebaki takribani miezi miwili  kuuga Mwaka 2023 na kuingia Mwaka Mpya wa 2024,Jumuiya ya Wazazi wa Wanafunzi wa Shule ya sekondari ya wasichana [Kilakala Girls Secondary School] ‘KILASEPA’ chini ya Uongozi wa Mwenyekiti wa Jumyiya hiyo  Dr. Kelvin Njunwa wamefanya Ukarabati wa uzio na  Gate kuu la kuingia shuleni hapo na lile Geti la pande wa  Nyuma.

Wazazi hao wameamua kufanya ukarabati huo kwa lengo la kuipa hadhi shule hiyo kongwe na Maarufu nchini Tanzania ambapo baadhi ya viongozi wengi maarufu nchini wamesoma  shule hiyo iliyopo chini ya Milima ya Uluguru Kata ta Kilakala Manispaa ya Morogoro.

 lfahamike pia Upendo Shekidele ambaye ni Mdogo wake Mwandishi wa habari hizi. alihitimu kidato cha sita katika shule hiyo.

Uongozi wa KILASEPA Umesapoti  Juhudi za Rais Dr. Samia Suluu Hassan chini ya Uongozi wake  Umejenga Mabweni Mapya 3 na Madarasa Mapya 8 yenye uwezo wa kubeba wanafunzi 450.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi mageti hayo kwa uongzo wa shule hiyo,Mwenyekiti wa Jumiya hiyo Dr Njunwa aliushukuru  Uongozi wa Shule ya Kilakala kwa kusimamia  Vizuri

ukarabati huu.

“Kwa niaba ya Jumuiya wa Wazazi wa shule hii tunaushukuru Uongozi wa shule kwa kusimamia kwa kwa weledi kazi hii,Kipekee tumshukuru Mkuu wa Shule Madam  Mary Lugina  na Makamu wake Mr. Mkangwa” alisema Dr Njunwa Msomi anayemiliki PHD ya Chuo Kikuu Cha Kilimo Cha Sokoine’SUA’ 

Wakati akitunukiwa PHD hiyo huku akisindikizwa na Matarumbeta takrinani miaka 3 iliyopita Mpiga Picha Maarufu wa Mtandao huu anayemiliki Kamera za Kisasa ambaye pia ni ’Photo Journalist’ ndiye aliyepewa tenda na familia ya Profesa Njunwa kupiga Picha matukio yote ya hafra hiyo iliyofanyika ukumbi wa Chuo cha Uandishi wa habari Morogoro’MSJ’uliopo Mkundi Manispaa ya Morogoro.

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...