Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Friday, August 4, 2023

KUELEKEA MCHAKATO WA KATIBA MPYA WAZIRI KASEMA HAYATI LUANDA ALIKUWA NGUZO MUHIMU KWENYE MCHAKATO HUO.

            Jeneza lililobeba mwili wa Mpendwa wetu Luanda.
                        Hayati Luanda enzi za Uhai wake

           Naibu Waziri Mh Pouline akitoa salamu za Rambirambi

 


                                 Na Dunstan Shekidele,Morogoro.
KUELEKEA Mchakato wa Katiba Mpya, Naibu Waziri wa Wizara ya Katiba na Sheria Mh Pauline Gekul amesema kifo cha Mkurugenzi wa Katiba na Ufuatiliaji Haki, Hayati Kharist Michael Luanda[57]alikuwa tegeo kubwa kwenye mchakato huo. 
 
Naibu Waziri Pauline aliyasema hayo alipotoa Salamu za Rambi rambi kwa niaba ya Wizara kwenye Mazishi ya Marehemu Luanda yaliyofanyika Julai 31 kijijini kwake Lukenge eneo la Dabwala Kata ya Kibungo Juu Tarafa ya Matombo Wilaya ya Morogoro Vijijini.
 
”Kama Wizara tumepoteza mtu muhimu sana kipekee nilikuwa na mtegemea sana kaka Luanda kwenye mambo mbali mbali ikiwemo ya kujibu maswali Bunge, tulimuhitaji Kaka Luanda kuliko wakati yoyote ule kama mnavyojua tunaelekea kwenye mchakato wa Katiba, kama Wizara tukimtegemea sana kwenye mchakato huo”alisema Naibu Waziri huyo na kuongeza
 
Hivi karibuni nikiwa Mbeya Waziri wetu wa Katiba na Sheria Mh Dkt Damas Ndumbaro aliniambia nikutane na Kaka Luanda tuanze kujadili swala hilo la Mchakato wa Katiba”alimaliza Naibu Waziri huyo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Babati Mjini. 
 
Baadhi ya Vigogo wengine wa Wizara hiyo walishiriki kwenye Mazishi hayo ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Mary Makondo.
 
Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Jaji Mstaafu January Msofe.
 
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro Mh Poul Ngwembe.na Wakurugenzi mbali mbali wa Wizara hiyo. 
 
Watoto wa Kiume wa Marehemu waliza watu Msibani Picha za tukio hilo zitaruka hewani hivi Punde, hivyo endelea kuwa jirani na Mtandao huu muda wote.



No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...