Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Thursday, August 31, 2023

AMINA KIANDO AZIDI KUPIGA MWINGI.

                                       Amina Kiando

 ...Amina Kiando akiongoza timu za Mtibwa na Mbeya City kuingia uwanjani, kulia ni mkufunzi wake Refa Martin Saanya

 

             Na Dustan Shekidele,Morogoro.

Mwamuzi Chipukizi wa kike  Amina Kiando Mkazi wa Mkoani Morogoro anazidi kupiga mwingi kwenye kazi yake ya Uamuzi wa mpira wa Miguu.

lkumbukwe mwaka 2017 Mtandao Pendwa wa Shekidele uliriripoti Makaka iliyomhusu refa huyo, baada ya Mmoja wa wakufunzi wake, Afande Martin Saanya Pichani [kulia mwenye beji ya FIFA kumpa nafasi ya kuchezesha mchezo mkubwa uliozikutanisha timu kubwa za ligi kuu Mtibwa Sugar na Mbeya City.

Licha ya kuwa madaraja ya chini wakati huo lakini aliaminiwa  na kupangwa kuchezesha mchezo huo mkubwa.

Gemu hiyo  Maalumu ilidhaminiwa na kanisa  la Baptist ulipigwa Julai 29 2017 kwenye tamasha la kanisa hilo lililofanyika uwanja wa Jamhuri Morogoro.

Kwenye mchezo huo Amina Kiando alichezesha vizuri hali liliyopelekea Mwandishi wa habari hizi kuvutiwa na uwezo wake na kumwandikia makalla hiyo iliyomtabilia kufika mbali kwenye kazi yake hiyo ya refa.

Hatimaye  refa Amina  ameanza kufika mbali baada ya sasa kupanda daraja na kuteuliza kuchezesha michezo migumu ya Ligi kuu Tanzania Bara.

Miongoni mwa michezo hiyo ni mchezo wa juzikati wa nusu fainali ya mchuano ya Ngao ya Jamii kati ya Simba na Singida Big Star uliopigwa Uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga na Simba kuibuka na ushindi.

Mtandao huu unazidi kumshauri Amina asibweteke na mafanikio hayo bali aendelee kupambana hadi kufikia hatua ya kuvishwa beji ya FiFA na kuchezesha michuano mikubwa barani Afrikani.

Hakuna lisilowezekana hapa chini ya jua kama utafanya kazi yako kwa kutenda haki na kusimamia amri za mwenyezi Mungu na sheria za nchini na sharia 17 za mchezo huo wa Soka.

 Vile vile Mtandao huu unasema ni kosa kubwa kukata tamaa kwa jambo ambalo hujui mwisho wake utakuaje.

Wao waweze wanani? wewe ushindwe unanini?

 

Wednesday, August 30, 2023

MTIBWA SUGAR WAFUNGUKA KIFO CHA KOCHA MUMBA.

Thobiasi Kifaru akihojiwa na Mwandishi wa Mtandao huu .
waombolezaji wakibeba jeneza lenye mwili wa Mpendwa wetu wakiliingiza kwenye gari  kuelekea kwenye nyumba yake ya Milele Makaburi ya Kolla.

                            Hayati Mumba enzi za Uhai wake
 


             Na Dustan Shekidele,Morogoro.

TIMU ya Mtibwa Sugar yenye Mskani yake katikati ya Mashamba ya Miwa eneo la Manungu Kata ya Mtibwa Tarafa ya Turiani Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro, wamefunguka mazito  kifo cha Mwalimu Maarufu wa Mpira wa Miguu Tanzania Kocha Ahmedi Mwarabu Mumba.

Baada ya kutokea kwa Msiba huo mzito,Uongozi wa Mtibwa uliotuma wawakilishi wawili kuja Morogoro Mjini kushiriki mazishi hayo.

Akizungumza  na Mtandao huu juzi  nyumbani kwa marehemu Kihonda Mbuyuni Kata ya Mafisa, Mkuu wa Kitengo cha habari na Mawasiliano cha Mtibwa Sugar Thobias Kifaru Ligarambwike amesema.

” Shekidele Uongonzi wa Juu wa timu yetu  umenituma  mimi na mwenzangu kuja kushiriki msiba huu mzito wa Kocha Mumba.

Ifahamike Kocha Mumba ndiye kocha aliyeipandisha daraja timu yetu  mwaka 1995 tukitokea ligi daraja la kwanza kuingia ligi kuu, miaka 4 mbele kwa maana ya 1999 na 2000 tulifanikiwa kutwaa ubingwa wa Tanzania bara mara mbili mfurulizo kocha Mumba akiwa na mchango mkubwa kwenye mafanikio hayo.

 Kama hiyo haitoshi toka tupande daraja 1995 hatujashuka daraja mpaka sasa tunaendelea kukipiga Ligi kuu miaka 28 mfurulizo kwa Mantiki hiyo ukitoa Simba na Yanga sisi mtibwa ndio timu kubwa ”alisema Afisa habari huyo mwenye maneno mengi.

 Mbali na Mtibwa Sugar Mwandishi wa Mtandao huu anazikumbuka timu nyingine alizozipandisha daraja Kocha Mumba  ni Mirambo ya Tabora, Nazareti ya Njombe, na Polisi Morogoro.

                      


 

 

Tuesday, August 29, 2023

MAMIA YA WANANCHI WAMEJITOKEZA KWA WINGI KUMZIKA MKUFUNZI WA MAKOCHA TANZANIA.



 Mh Fikiri akitabasamu baada ya kukumbushwa jambo na Mwandishi wa Mtandao huu ambapo kuna kijiweo chetu cha kunywa chai Pricens hotel imekufa kwa sasa tunakutana Bums nyakati za jioni.

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Morogoro Mjini Mhe Fikiri Juma ambaye pia ni mdau mkubwa wa Soka akitoa salamu zake za rambi rambi.

Kiongozi wa chama cha wachezaji wa zamani [UMSOTA Tanzania] Hamisi Malivedha kulia akimkabidhi rambi rambi Mwarabu Mumba ambaye ni mtoto wa marehemu Ahmed Mumba.[11] Mratibu wa Moro Kids Rajab Kindagule[kulia akikabidhi rambi rambi kwa niaba ya kituo hicho cha Moro Kids kinachoongoza kutoa wachezaji nyota wanaota,mba kwa sasa ligi kuu

Katibu Mkuu wa Chama Cha Soka Mkoa wa Morogoro'MRFA' Emmanuel Kimbawara akitoa saramu za rambi rambi." Kama mnavyojua Marehemu Mumba alikuw amkufunzi wa makocha hata Tanzania,hivyo Rais wa TFF Wales Karia amenituma kutoa saramu hizi za rambirambi kwa msiba huu mzito kwa familia ya wanasoka,"alisema Katibu huyo ambaye Mchungaji Mstaafu wa makanisani ya Sabato


Mwarabu Mumba mtoto wa kiume wa marehemu Ahmed Mumba akitoa neno la shukrani.

" Nawashukuru wote waliotukimbilia kwenye msiba huu mzito wa Mpendwa baba yetu, kipekee nimshukuru Mhe Abood Mbunge wetu wa jimbo la Morogoro ambaye ndiye aliyetoa gari lililobeba mwili wa baba kutoka Dar Mpaka hapa nyumbani,

 kama hiyo haitoshi kato sanduku lililobeba mwili pamoja na kilo 50 za mchele"alisema Mwarabu Mumba ambaye ni Mwamuzi Mwandamizi wa ligi daraja la kwanza taifa aliwahi pia kucheza ligi kuu


Afisa habari wa Mtibwa Sugar Thobias Kifaru Ligarambwike kitabasamu baada ya kumuona Mwandishi wa Mtandao huu, Picha no 2 Kifaru akiteta jambo na Mwamuzi Mstaafu

. Akizungumza na Mtandao huu Kifaru amedai ametumwa na Uongozi wa Mtibwa Sugar kuhudhuria msiba huo akidai marehemu Mumba anahistoria kubwa na timu hiyo

Historia hiyoitaruka hewani hivi punde hivyo endelea kuwa jirani na Mtandao huu muda wote

Kutoka kulia.

Hamis Kambi, Mwamuzi Mstaafu ambaye ni Askari Magereza wa gereza kuu la Manispaa ya Morogoro.Ally Jangalu. Kocha wa zamani wa Kagera Sugar. Mwalimu Mzigira kocha wa zamani wa Reli Morogooro.Thobias Kifaru Ligarambwike, Afisa habari wa Mtibwa Sugar. Hasani Gobosi’Gadagada’ Kocha wa zamani wa Reli ya Morogoro.Mwisho aliyesimama ni Athuman Matenga Katibu Msaizidi  Reli ya Morogoro ‘Kiboko cha Vigogo’.

 

Wadau wa soka kutoka Kushorto ni Afande Hamis Kambi, Afande Salum Mbaruku ambaye ni mchezaji wa zamani wa Mirambo ya Tabora na Polisi ya Morogoro. Thibias Kifaru Afisa habari Mtibwa Sugar, mwenye kofia nyeusi ni Mgosi mwalimu mwaafudu wa madereva akipiga kazi Morogoro Dreving School 

pembeni yake ni Afande Daud Salum huyu ananyazifa kibao. ni mwenyekiti Msaafu wa timu ya Polisi Mara, Katibu Mstaafu wa chama cha Soka Mkoa wa Mara, Mjumbe wa timu ya Polisi Morogoro,

Baada ya kustaafu Upolisi katimkia kwenye siasa na kufanikiwa kuwa diwani wa Kata ya Mafisa labla ya kuangukia pua kwenye uchaguzi mkuu uliopita akishindwa na Mh Kizomi Maarufu Dr wa Mifupa anayemiliki hospital ya Mifupa eneo hilo la Mbuyuni kata ya Mafisa.

Wa mwisho mwenye kofia nyeupe Mwandishi wa Mtandao huu hakuweza kumfahamu fasta.

 


Athuman Kairo kocha wa zamani ya Pamba ya Mwanza kwenye msiba huo alikuwa mratibu wa mambo yote loicha ya marehemu kuwa mwalimu wake wa Ukocha lakini pia wanatoka Mkoa mmoja wa Kigoma

Mmiliki wa shule za Mteule Open School zilizopo Uwanja wa Jamhuri Morogoro na Sanga sanga njia panda ya Mzumbe. Mteuke ni mdau mkubwa wa soka akiishabikia timu ya Simba










         Marehemu Mumba enzi za Uhai wake

                Na Dustan Shekidele,Morogoro.

MAMIA ya wananchi kutoka maeneo mbali mbali nchini wakiongozwa na msemaji mkuu wa timu ya Mtibwa Sugar Thobias Kifaru Ligarambwike, jana wamejitokeza kwa wingi kumzika Mkufunzi  wa Makocha Tanzania Marehemu Ahmed Mumba.

Marehemu Mumba ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Makocha Mkoa wa Morogoro’TAFCA’  amefariki dunia Jumamosi iliyopita hospital ya Mloganzira Jijini Dar es salaam alipokuwa akipatiwa matibabu na kuzikwa jana Makaburi ya Kolla Mkoani Morogoro.  

Mara baada ya Kocha Mumba kufariki  Mwili wake ulirejea nyumbani kwake Kihonda Mbuyuni Kata ya Mafisa ambapo wadau mbali mbali wa soka wakiongozwa na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Morogoro Mjini Fikiri Juma wamefulika nyumbani kwa marehemu kushiriki lbada ya kumuombea  iliyoongozwa na Mashehe zaidi ya 7.

Wingi wa Mashehe hao unatokana na Marehemu Mumba enzi za uhai wake kuwa jirani na Mwenyezi Mungu kwa kushiriki  swala 5 kwenye misikiti mbali mbali ya Mkoa wa Morogoro.

Baadhi ya Mashehe hao ni pamoja na Shehe Koba wa Msikiti wa I.G.P Mstaafu Alhaj Omar ldd Mahita ulipo Mafiga, Shehe Ally Omar wa Msikiti Mkuu wa Morogoro ulipo Boma Road.

Wengine ni Shehe Shaban Juma wa Msikiti wa Awayya Uliopo Mawenzi ambaye ndiye aliyepiga Adhana swala ya saa 10 iliyofanyika nyumbani kwa  marehemu akitanguliwa na swala ya kumuombea Marehemu yenye lakaa 4.

Enzi za uhai wake Marehemu Mumba akiwa katibu wa TAFCA huku mwenyekiti wake akiwa John Simkoko chama hicho kinatambuliwa na shirikisho cha Mpira wa Miguu Afrika’CA F’.

Hivyo Hayati Mumba na Simkoko mara kwa mara kupitia chama  hicho walitoa mafunzo ya ukocha yanayotambuliwa na CA F,makocha kibao wakiwemo wa Simba,Yanga Azam wameshiriki mafunzo hayo na kukabidhiwa leseni zinazotambuliwa na CA F na Shrikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF.

 Baadhi ya makocha hao ni Pamoja na Seleman Matola, Simba Abibu Kondo Mtibwa Sugar Mecky Mexime Kagera Sugar, John Tamba, Polisi Tanzania,Zuberi Katwira Ihefu.

Wengine ni Juma Kaseja, Ulimboka Mwakingwe, Athuman Kairo Ally Jangalu.na  Bi.Edina Lemma aliyekuwa kocha wa Yanga Princess

Kama kawaida Mwandishi wa Mtandao huu alizunguka kona zote kwenye msiba huo akisaka picha za watu maarufu alizosiona hapo juu


 

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...