Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Saturday, July 22, 2023

MAAJABU YA YESU KRISTO[NABII ISSA]KAUSHIBISHA MKUTANO WA WATU ELFU 4 KWA MIKATE 7.

 Nikiwa na Mabinti zangu Tumani Dustan Shekidele[kushsoto] na Neema Dustan Shekidele.Tukila vipande vya Samaki Pori[Mdudu]


 . Nikiwa na Mwanafunzi wangu Neema D. Shekidele shule ya Sekondari. Kigurunyembe.

 

MARKO 8.1-10

”Katika  siku zile  kwa vile ulivyokuwa Mkuu tena ule Mkutano, nao wamekosa kitu cha kula, akawaita wanafunzi wake akawaambia.

Nawahurumia mkutano  kwa sababu yapata siku tatu wamekaa nami,wala hawana kitu cha kula.

Nami nikawaagiza waende zao nyumbani  kwao hali wanafunga watazimia njiani na baadhi yao wametoka mbali.

Wanafunzi wake wakamjibu je ataweza wapi mtu kuwashibisha hawa mikate hapa nyikani?.

 Akawauliza mnayo mikate Mingapi?wakasema saba.

Akawaagiza Mkutano waketi chini,akaitwaa ile mikate saba, akashukuru akaimega akawapa wanafunzi wake wawandikie,wakawaandikia  mkutano.

Walikuwa na Visamaki Vichache,akavibariki akasema waandikieni na hivyo pia.

Wakala, wakashiba wakakusanya mabaki ya Vipande vya Mikate makanda saba.

 Na watu waliokula wapata elfu nne, akawaaga.

Mara akapanda chomboni pamoja na wanafunzi wake,akaenda pande za Dalmanutha.”

Hilo ndilo neno la Mungu jumapili ya leo Julai 23.

Ifahamike watu hao nne waliohesabiwa kula hiyo mikaye sana na wanaume pekee, wanawake na watoto hawakuhesabiwa ingawa walishiriki kwenye mkutano huo na kula Mikaye hiyo.

                     

 

.


No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...