Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Tuesday, July 25, 2023

KUMBUKIZI

Watoto hao wakiwa hospitarini hapo  siku chache baada ya kuzaliwa.

 Mwandishi wa Mtandao huu [kulia] akizungumza na mmoja wawananchi wa kijiji cha Berega nje ya hospital ya kijiji hicho.


 Na Dustan Shekidele,Morogoro.

Tukio hili la watoto mapacha wote  jinsi ya kike kuzaliwa huku wakiungana miili yao limetokea Julai 21-2017 katika hospital ya Misheni ya Berega Wilaya ya  Gairo Mkoa wa Morogoro.

 

 

 

Baada ya kupokea taarifa za tukio hilo kutoka kwa  wawananchi wa Kijiji  hicho kilichopo takribani kilometa 15 kutoka Makao makuu ya Wilaya ya Gairo, Mwandishi wa habari hizi alipiga gia Pikipiki yake ya Mwendo kasi kutoka Morogoro Mjini hadi kijijini hapo na kufanikiwa kuwaona watoto hao sambamba na kuzungumza na baba yao Lucas Chomolo.

 

Akizungumza na Mtandao huu Chamola alisema mkewe Bi. Rebecca Mwendi[42] alijifungua kwa njia ya upasuaji mapacha hao  wakiwa wameungana kifua na tumbo huku akiiomba Serikali kumsaidi gharama za kuwatenganisha.

Serikali ya Tanzania ni sikivu llisikia ombi la Mzazi huyo na kubeba jukumu la kumsaidia kwa kuwahamishia watoto hao kwenye hospital kubwa na kufanyiwa upasuaji wa kutenganishwa.

Hadi leo Julai 25-2023 ni miaka 6 imepita toka watoto hao watenganishwe,hivyo kwa kuwa nilikuwa Mwandishi wa habari wa kwanza kuripoti tukio hilo kwenye Magazeti ya Global Publishers.

 Siku mbili hizi najitafuta nikifanikiwa kupata Pesa ya mafuta ya Pikipiki nitaelekea kijijini hapo kujua maendeleo yao.

Hivyo endelea kuwa jirani na Mtandao huu muda wote kwa mwendelezo wa habari hii ya kijamii zaidi.

                     


 

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...