Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Monday, January 30, 2023

WITO KWA WATANZANIA WENZANGU.




 


 

Tujitokeze kwa wingu kuchangia damu kwenye kituo chochote cha afya kwa lengo la kuimalisha Bank ya damu inayotumika kusambaza damu kwa ndugu zetu wagonjwa wenye uhitaji wa kuongezewa damu.

 

Tunafundishwa na Viongozi wetu wa dini kwamba tufanye matendo mema na ya huruma kwa ndugu zeru wenye uhitaji.

 

Kwamba kama unaviwili mgawie kimoja mtu mwenye uhitaji wa kituo hicho.Mwenyezi MUNGU Mwingi wa Rehema atufanyie wepesi tuwe na mioyo hiyo ya huruma na atuondolee ubinfsi na mioyo ya choyo.  .

 

 Kutoa kwako damu kutasaidia kuokoa maisha ya ndugu zetu hasa Wazazi na Majeruhi wa ajari mbali mbali zikiwemo za barabarani.

 

Kutoa ni moyo sio utajiri,nashukuru uongozi wa hospital umethamini mchango wangu huo baada ya kumalizi kugemwa damu hiyo iliyojaa kifuko cha kilo 2 wamenipa  zawadi ya Mirinda nyeusi na kadi  Maalumu ya damu salama.

 

Kwa mujibu wa maelezo yao kadi hii ni kitambulisho cha kuwa na hisa ya damu kwenye bank hiyo.

 

 Hivyo ikitokea mimi au ndugu yangu tukihitaji huduma hiyo nikionyesha kadi hii napatiwa huduma hiyo bure kutoka kwenye bank hiyo ya damu salama kwa uwekezaji wangu huo ilioufanya zaidi ya mara mbili kwa miaka miwili mfurulizo. .

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...