Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Tuesday, January 31, 2023

MAAJABU YA MJI KASORO BAHARI MGOMBA WAZAA MIKUNGU 2 YA NDIZI.


 

Na Dustan Shekidele,Morogoro.

 

 Ukistaajabu ya Musa hutoyaona ya Filahuni, Mgomba uliombandwa ndani ya uzio wa nyumba ya Mzee Mongi iliyopo Kihonda Maghorofani umezaa Mikungu miwili ya ndizi kwa mpigo.

 

Baada ya kuona hali hiyo Mmiliki wa nyumba hiyo Mzee Mongi alimtwangia simu Mwandishi wa Mtandao huu kumwalika nyumbani kwake kuchukua tukio hilo adhimu kutokea kwenye Jamii yetu.

 

Kwenye mahojiano Maalumu Mzee Mongi Mchaga wa Moshi Mkoani Kilimanjaro alipoulizwa kama ndizo hizo zikikomaa atazivuna na kuzila na familia yake au atazipiga bei? Jibu lake lilikua hili.

 

” Shekidele ndizi hizi zimekuwa kivutio hapa nyumbani kila siku watu wanakuja kwa wingi kuzishangaa hivyo zitabaki kuwa kivutio mpaka zitakapokomaa na kuivia mtini”.


 

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...