Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Saturday, January 21, 2023

TANZIA.DENT WA KIDATO CHA 6 AFARIKI DUNIA


 


Taarifa kwa hisani ya Radio Ukweli inayomilikliwa na kanisa Katoliki Jimbo na Morogoro ambapo pia shule hiyo ya Kigurunyembe inamilikiwa na kanisani hilo Taarifa hiyo inasomeka hivi.
"Mwanafunzi mmoja wa kidato cha sita Shule ya Sekondari Kigurunyembe mkoani Morogoro Namith Jackob Sayore amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika Hospitali ya Nanguji mkoani humo.
Akizungumza na Radio Ukweli Mkuu wa Shule hiyo Mwalimu Daniel Lameck Chipindula amesema kuwa afya ya Mwanafunzi huyo ilianza kutetereka siku za karibuni na umauti umemkuta usiku wa Januari 19 mwaka huu wakati yupo katika matibabu Hospitalini hapo.
Naye Mzazi wa Mwanafunzi huyo Jackob Sayore Mmbaga amesema ameupokea msiba huo kwa masikitiko makubwa
Kwa upande wao baadhi ya Wanafunzi Shuleni hapo wamebainisha kuwa Msiba huo ni mkubwa kwao kwani alikuwa ni Mwanafunzi ambaye Rafiki kwa kila mmoja Shuleni hapo hivyo watamkumbuka kwa mengi.
RAHA YA MILELE UMPE EE BWANA NA MWANGA WA MILELE UMUANGAZIE, APUMZIKE KWA AMANI....... AMINAA.

No comments:

Post a Comment

VITUKO VYA MWEZI JANUARI

  Mwezi uliopita tumeshehelekea Siku Kuu mbili X Mas na Mwaka Mpya.   Mwezi huu dume January tunashehelekea kulipa Ada za Shule na kod...