Shekidele Blogs

Shekidele Blogs
Karibuni sana wadau wa blog ya Shekidele kwa mawasiliano zaidi 0715 28 90 73

Tuesday, January 3, 2023

MKUU WA MKOA NAYE ATOA NENO MPANGILIO MBOVU WA MKOA WA MOROGORO.

Mkuu  wa Mkoa akizungumza na wajumbe halali wa Mkutano huo waliojazana kwenye ukumbi wa Bwalo.



Baadhi ya waandishi wa habari wakipiga Picha ya pamoja Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa. Mh Fatuma Mwassa, Miongoni mwao ni Mwandishi wa Mtandao huu aliyesimama nyuma ya Mkuu wa Mkoa Mstaafu Mzee Steven Joshua Mashishanga[mwenye skavu ya pendera ya taifa shingoni.
Mwenyekiti wa Chama hicho Nickson Mkilanya akimsindikiza Mkuu huyo wa Mkoa mara baada ya kufungua Mkutano huo.

 


                Na Dunstan Shekidele,Morogoro.

WIKI iliyopita Mtandao huu  ujitika kwenye  habari ya kiuchunguzi kuelekea Manispaa ya Morogoro kuwa Jiji.

 

Siku moja baada ya kukamilisha kwa habari hiyo iliyoruka hewani  takribani siku 3 mfurulizo, siku iliyofuata Disemba 30 Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mh Fatuma Mwassa aliarikwa kufungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama Cha Waandishi wa habari Mkoa wa Morogoro’MOROPC’.

 

 Kabla ya kufungua Mkutano huo Mkuu huyo wa Mkoa alipata wasaa wa kuzungumza Machache na Waandishi hao kutoka Wilaya zote za Mkoa wa Morogoro.

 

Miongoni mwa machache hayo Mh Fatuma alitema nyongo kuhusiana na mpangilio mbovu wa Majengo kwenye Mkoa huo  uliojaliwa kila aina ya rasrimali.

” Morogoro ni Mkoa pekee ambao watu wanajenga kiholera kwenye utawala wangu hili halina nafasi yaani mtu ana amka asubuhi ana mwaga tofati popote na kuanza kujenga bila  kibari cha ujenzi.

 

 Nimebahatika kuishi mikoa ya Dar es salaam, Dodoma, Tabora, Geita na Visiwani hilo la ujenzi holela nimeliona hapa Morogoro, Kwa hali kama hii mkoa wa Morogoro kuendelea ni shida sana”alipigilia msumari wa Moto Mkuu huyo wa mkoa aliyewahi pia kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mvomero miaka ya 2005.

 

Mkutano huo uliohudhuriwa pia na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro SACP Fortunatus Musilim, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Morogoro Fikiri Juma na Mkuu wa Mkoa Mstaafu Mzee Steven Mashishanga ambaye yeye na tajiri Aziz Abood ndio  walezi wa Chama hicho cha Waandishi wa habari.

 

Mtandao huu umekusanya matukio kadhaa kwenye Mkutano huo uliofanyika ndani ya ukumbi wa JKT Bwalo la Umwema hivyo endelea kuwa jirani na Mtandao Pendwa wa Shekidele Muda wote.

                         


 

 

No comments:

Post a Comment

MUUZA MAGAZETI ADAIWA KUJINYONGA MUDA MFUPI BAADA YA KUTOKA KWENYE KIKAO CHA MAZISHI YA DADA’KE.

                            Pili Sebuge Mama mzazi wa marehemu . ....Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ngoma B Rehema Matonya ...Miili ya m...